Pages

 

Thursday, May 31, 2012

OKWI ANA THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2-SIMBA

0 comments
 Klabu ya Simba imewataka baadhi ya timu kuacha tabia ya kutaka
kutangaza kuwa wanamchukua mchezaji Emmanuel Okwi wakati wakijua ni mchezaji halali wa klabu hiyo.
 
Ofisa habari wa Simba Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa kuna baadhi ya watu wameanza kutumia jina la Okwi kama njia ya kupata uongozi au kuonekana bora katika klabu zao huku zikiwa hazijawahi hata siku moja kufanya maongezi na klabu ya Simba.
 
Alisema kama kuna klabu inataka kumsajili mchezaji huyo ifuate utaratibu wa kuongea na viongozi wake kwa kuwa mchezaji huyo bado ni mali ya Simba.

Aliongeza kuwa kama kuna  klabu inataka imsajili Okwi inatakiwa kutumia zaidi ya bilioni 2 ili iweze kumchukua.
 

Alisema mchezaji huyo anatakiwa katika barani  Ulaya na iwapo kuna timu Tanzania inauwezo wa kutoa fedha hiyo, klabu ya Simba ipo tayari kumuuza kwa pesa hiyo.
"Tupo tayari kumuuza.Na kama kuna klabu hapa nchini ina bilioni 2, sisi tunamuachia, kwa kuwa bado mchezaji wetu na anaendelea kuitumikia klabu yetu ya Simba kwa zaidi ya miaka miwili"alisema Kamwaga.
Klabu ya Yanga kupitia wadau wake ilitangaza nia yake ya kumchukua mchezaji huyo raia wa Uganda kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.
Read more...

Wednesday, May 30, 2012

MTOTO ALIYEHARIBIWA MUHIMBILI BADO HOI INDIA

0 comments

 MTOTO Imrani Mwerangi (3) ambaye alipelekwa nchini India kwa matibabu baada ya kudungwa sindano iliyomsababishia mtindio wa ubongo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Dar es Salaam, bado amelazwa katika Kitengo cha Wagonjwa Mahututi (ICU) cha Hospitali ya Hyderabad, India.

Taarifa iliyotolewa jana na wazazi wa mtoto huyo kutoka nchini India, ilisema hali ya Imrani bado ni mbaya.

Machi mwaka huu Imrani alipelekwa nchini India na Serikali baada ya kulazwa katika ICU ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili tangu Julai 28, 2011.

“ Tangu kipindi hicho madaktari wamekuwa wakipigania kuokoa maisha yake lakini bado amelazwa katika ICU ya Hospitali ya Hyderabad,India,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilisema madaktari wanaomhudumia wamesema mtoto huyo ataendelea kutegemea matibabu katika  maisha yake yote.

“ Asante Mungu kwa kuendelea kumpigania mtoto wetu Imrani, leo anatimiza miezi kumi tangu alazwe katika ICU za Muhimbili na hapa India,” ilisema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo ya wazazi ilisema maisha kwao yamekuwa yenye changamoto kubwa lakini jambo kubwa sasa ni kutanguliza maombi kwa Mungu.

Kwa mara ya kwanza mtoto huyo alifikishwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Julai 28, 2011 kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa nyama zilizokuwa puani ambapo alipokewa na kufunguliwa jalada IP.No.A586301.

Kesho yake Julai 29, 2011 mtoto huyo aliingizwa katika chumba cha upasuaji mdogo wa nyama za puani lakini kabla ya upasuaji huo alidungwa sindano ya usingizi ambayo ndiyo iliyomsababishia matatizo mtindio wa ubongo.
Read more...

Friday, May 25, 2012

SIR ALEX FERGUSON KUSTAAFU MWISHONI MWA MSIMU UJAO

0 comments
Kocha wa timu ya soka ya Manchester United, Sir Alex Ferguson  huenda akaachana na kazi yake ya ukocha mara tu baada ya kuisha kwa msimu wa 2012/2013,kutokana na kuanza kusumbuliwa na matatizo ya kiafya.


Kwa mujibu wa rafiki yake wa karibu ambae pia ni mmiliki wa timu ya Wigan Athletic,Dave Whelan,Ferguson anafikria kuachana na ukocha baada ya kupata matatizo ya kiafya Ijumaa iliyopita,amabapo alipatwa ghafla na ugonjwa wa kutoka damu puani mfululizo bila kuacha na kusababisha akimbizwe Hospitali ya Glasgow


Whelan alikuwa alikiambia kituo cha televisheni cha  ESPN:
"Baada ya msimu ujao,Sir Alex atabwaga manyanga.Msukumo wa mambo unataka iwe hivyo,hasa unapokuwa uko juu kwa muda mrefu.Umri unapokuwa umeshakwenda inakuwa ngumu kupambana namsukumo wa majukumu,na ipo siku lazima itakuathiri.Sir Alex ni mgumu kukubali kushindwa na najua atataka aendelee na hadi siku atakayodondoka na pia naheshimu mafanikio aliyofikia kama wengine wanavyoheshimu.Najua lengo lake lilikuwa kuendelea kwa miaka miwili au mitatu zaidi,pengine zaidi ya hapo,lakini alipata matatizo kidogo ya kiafya wiki iliyopita,hiyo inaniambia kuwa lazima afikirie kwa kina maamuzi yake na atagundua kuwa hakuna ulazima wa kuendelea kwa miaka mingine mitano na kujiweka katika hatari.Ningependa niseme yeye ni kocha bora kabisa kupata kutokea.Kama ataamua kweli kufunga virago, basi litakuwa ni pigo kubwa katika mchezo wa soka.Nina hakika.Jinsi mafanikio yake yasivyo lingana na ya mtu (kocha) yeyote,jinsi anavyochagua wachezaji kwa usahihi na kupata mavuno zaidi kutoka kwao,inamfanya awe kocha bora kabisa,bora zaidi ya tuliowahi kuwaona"
Read more...

Wednesday, May 23, 2012

TEH TEH TEH...SOMA STORI,ONA PICHA UCHEKE KAMA MWEHU

0 comments
ETI  EEEENH?


Read more...

MLINZI ALIEKUWA ANATETEA MCHORO WA ZUMA USIHARIBIWE AKAMATWA NA KUFUNGULIWA MASHTAKA

0 comments

Picha za televisheni zikionedsha Lowie Mabozela akishambuliwa
Mlinzi aliekuwa akitetea mchoro wa Rais wa Afrika Kusini,Jacob Zuma usiharibiwe  kwenye jumba la maonesho ya picha jijini Johannesburg amekamatwa na kuwekwa mahabusu


Kanali Vishnu Naidoo msemaji wa polisi alieleza:
"Amekamatwa muda mfupi uliopita "
Picha za televisheni zilimuonesha mlinzi huyo akimpiga kichwa na kumbinua sakafuni mtuhumiwa Lowie Mabokela kijana mdogo aliekuwa akichafua mchoro kwa rangi nyeusi jana Jumanne


Naidoo amesema Mabokela alifungua kesi ya kushambuliwa jana usiku

Mabozela akivuruga rangi nyeusi kwenye mchoro wa Zuma
Barend la Grange akiweka alama ya X juu ya mchoro
Kijana Lowie Mabozela

Unyama aliofanyiwa Mabokelo umezua mjadala na hasira zingine nchini Afrika Kusini


Mtuhumiwa wa pilialieharibu mchoro,Barend la Grange ambae ni profesa hakuonekana kufanyiwa unyama wakati anakamatwa


Jumba la maonesho liliendelea kuwa limefungwa leo Jumatano.Mtuhumiwa mwengine wa tatu alikamatwa akichora ukutani nje ya jengo la maonesho maneno yasemayo`RESPECT`
Barend la Grange

Watuhumiwa wote watatu wamepewa dhamana baada ya kusomewa mashtaka na mahakama ya Hillbrow


Habari zingine zinasema wenye maonesho wameamua kufunga na kuondoa mchoro wa Zuma na kuupeleka sehemu salama baada ya vitisho kuzidi
Read more...

Tuesday, May 22, 2012

PICHA YA JACOB ZUMA AKIWA UCHI YACHORWA NA KUWEKWA KWENYE MAENESHO,YAZUA UTATA MKUBWA

0 comments
Picha hii inaonesha sehemu ya juu ya mchoro uliopewa jina la `The Spear `ukifananisha taswira ya rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma


Mchoro wa picha inayomkejeli rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ukionesha mfano wa sehemu za siri za rais huyo wa taifa lenye nguvu barani Afrika, umewekwa hadharani kwenye jumba la maonesho ya picha la Goodman huko Johannesburg,Afrika Kusini na kuanzisha mjadala mkali.
Mchoro huo uliopewa jina la `The Spear`ulichorwa na kuwekwa hadharani na msanii wa michoro wa Cape Town, Brett Murray ambae amejitetea kuwa hakuwa na lengo la kumuudhi mtu yeyote ila ni njia yake ya kujieleza kisiasa kwa staili ya ucheshi,kama msanii
Mchoro huo ni sehemu ya michoro iliyo kwenye maonesho ya Murray anayoyaita `Hail to the Thief II`


Katika kuonesha kukerwa na mchoro huo,watu wawili waliingia kwenye jumba hilo na kuuharibu kwa rangi.Mtu mmoja aliweka alama ya X kwa kutumia rangi nyekundu kwenye eneo la kichwa  na sehemu za siri za mchoro huo na mwengine ambae ni kijana mdogo alivurga mchoro kwa kupulizia rangi nyeusi.
Mwandishi wa BBC ambae alikuwa eneo hilo leo asubuhi aliandika kwenye Twitter:


"Mchoro wa Zuma umevurugwa kwa rangi nyeusi.Muhusika kaniambia kuwa mchoro huo ni wa kichokozi.Walinzi wamemvamia na kumkamata...mtu wa pili nae mbaroni"


Mchoro huo ulikuwa unalindwa na kampuni binafsi ya ulinzi wakati wa tukio


Baada ya kutiwa mbaroni watuhumiwa walifikishwa kwenye kituo cha polisi cha Rosebank


Mapema leo wawakilishi wa chama cha ANC walikimbilia mahakama kuu ya Gauteng mjini Johannesburg kufungua pingamizi la kuzuia jumba la Goodman lisitumie mchoro huo wenye urefu wa mita 1.85 kwenye maonesho.Na pia walikwenda kwenye ofisi za City Press kutaka picha za mchoro huo zisiwekwe mtandaoni


Polisi awali walitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuwa  mitaa kadhaa kuzunguka eneo la mahakama kuu itabidi ifungwe  kuruhusu wafuasi wa ANC ambao wangefika hapo kwa maandamano.Walisema mitaa hiyo itakuwa wazi ifikapo saa 9 alasiri ambapo mahakama itakuwa inafunga shughuli zake


Jumuia ya wanawake wa ANC walihimiza wanawake wenzao kuunga mkono uamuzi wa ANC kuandamana hadi mahakamani.Katika taarifa yao walisema:

"Hakuna Mwafrika Kusini yeyote,katika ofisi yoyote anaestaihili kuvunjiwa heshima namna hii na ni mtu aliekosa hekima kichwani mwake tu ndie anaeweza kudiriki kuchora mchoro kama huu.Tunatoa shutuma kali kwa kazi hii (ya Murray) na tutaendelea kuidharau kadri inavyostahili,tukitegemea Brett Murray atachukua fursa hii kujiangalia,heshima na tabia yake kama binadamu"


Chama cha ANC kiliwataka wanachama wake kukusanyika kwa wingi nje ya mahakama kuu leo kutetea utu, heshima na hadhi ya Zuma, rais wa ANC
Gazeti la Times nalo liliripoti leo asubuhim kuwa msemaji wa kanisa la Nazareth Baptist Church,Enoch Mthembu amependekeza Bret Murray apigwe mawe hadi kufa


"Huyu mtu amelitukana taifa zima na anstahili kupigwa mawe hadi afe.Alixchofanya kinaonesha ni jinsi gani alivyolelewa kibaguzi.Sanaa haiungi mkono kuwavunjia heshima binadamu wenzako"


Chama cha ANC kiliwasilisha karatasi za kimahakama kwenye jumba la maonesho na City Press ambazo zilizotolewa na mahakama siku ya Ijumaa
Karatasi hizi zinazuia pande zote mbili kuweka hadharani mchoro na picha za mchoro huo kwenye mitandao yao au mahali pengine popote


Habari kutoka kwenye jumba la maonesho la Goodman zinasema kuwa wamekataa kutii amri ya mahakama ya kuondoa mchoro huo na kusema kuwa mchoro huo watautumia hadi hapo maonesho yatakapokwisha na kuongeza kuwa kazi yao inalindwa na haki yao kikatiba ya uhuru wa kujieleza


Habari zilizopatikana mchana  zinasema kuwa  watuhumiwa waliokamatwa wakiharibu mchoro huo kwenye jumba la maonesho la Goodman asubuhi ya leo ,wametambuliwa kuwa ni profesa wa chuo kikuu na kijana mdogo mwenye umri wa miaka 15


Mwanasheria wajumba hilo Gregg Palmer amesema kuwa watu hao watafunguliwa kesi ya kuharibu mali.


Ripota wa kituo cha Tv cha eNews,Iman Rappetti,ambae alikuwepo leo asubuhi kwenye jumba hilo kuripoti juu ya mchoro huo uliopewa jina la `The Spear` (mkuki),alieleza jinsi alivyokabiliana na profesa aliekuwa akiharibu mchoro.
Amesema kuwa alikuwa karibu kabisa na mchoro huo wakati profesa huyo alipotoa kifaa cha kuhifadhia rangi na kuanza kuchora alama ya X kukatiza sehemu za siri za mchoro huo


Ameelezea jinsi alivyomvuta mkono kumzuia asiharibu mchoro huku akipiga kelele kuomba msaada kutoka kwa wafanyakazi wa jumba hilo


Rappetti alimuelezea mtu huyo kuwa alikuwa wa kawaida tu amevaa koti lililofumwa,lakini hakujua kuwa nyuma yake alisimama kijana mdogo kashika kasha lenye rangi nyeusi tayari kufuata nyayo za profesa.Alipiga kelele kumzuia kijana huyo alipoanza kupakaza rangi nyeusi juu ya mchoro huo


Wafanyakazi wa jumba waliwadhibiti profesa na kijana, kabla ya polisi kufika mara moja na kuwachukua.Wafanyakazi wa hapo walimwambia Rappetti kuwa, awali profesa alijitambulisha kuwa ni wa kabila la Afrikaans,lakini Rappetti ana wasiwasi kuhusu hilo

"Haonekani kama ni Mwaafrikaans"

Umati wa watu na waandishi wa habari walianza kujaa kuzunguka jengo ambalo tayari lilikuwa limeshafungwa.Ndani ya lango kuu la kuingilia walisimama walinzi watatu wa kampuni binafsi huku wameshika silaha za moto na wamevaa jaketi za kuzuia risasi.
Read more...

SIRI YA AJALI YA MAFISANGO HII HAPA

0 comments
Gari Toyota Cresta lenye namba T 387 BMZ, likiwa limepondeka baada ya ajali iliyosababisha kifo cha mchezaji soka nyota wa Kimataifa wa Timu ya Taifa ya Rwanda na Simba SC ya Tanzania, marehemu Patrick Mafisango, iliyotokea eneo la VETA, Barabara ya Chang'ombe.
Olly Elenga, ni mtoto wa dada yake Mafisango. Yeye alishuhudia ajali hiyo jijini Dar es Salaam na ndie aliyeikimbiza maiti ya mchezaji huyo Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam

"Kilichotokea ni kwamba baada ya Mafisango kurudi Sudan, Jumanne, siku iliyofuata alizima simu kabisa akasema hataki kwenda popote. Akanipa dola 100 nipeleke kwa dada mmoja waliyekutana naye kwenye ndege jana yake kwa ajili ya kukodi gari ile iliyopata ajali, tukapewa na dereva anayeitwa Bozi. Mafisango hakuwahi kumiliki gari jijini Dar es Salaam. Lakini asubuhi ya Jumatano iliyopita (Mei 16) alimpigia simu nyota wa Yanga, Haruna Niyonzima `Fabregas' na kumwita kwake ili wajadili kuhusu mambo ya timu ya taifa ya Rwanda. Fabregas alikuja nyumbani kuanzia asubuhi na wakanywa pombe na baadaye wakaongezeka akina Redondo (Ramadhani Chombo.) "

"Wakakubaliana waende Kinondoni kwa Queen Suzy yaani yule dansa wa bendi ya FM Academia `Wana Ngwasuma', ambaye ana baa yake karibu na Mango Garden, basi ndio wakanywa hapo na baadaye mke wa Redondo, aliyewaandalia chakula akawaita nyumbani kwao ili wakale, walipofika kule wakanywa bia sana, hapo Mafisango alikuwa hapatikani kwenye simu kwani zilikuwa zinatumika simu za Redondo na marafiki wengine aliokuwa nao."

"Tulikaa sana kwa mke wa Redondo mpaka saa tano usiku. Mafisango alishalewa sana, alikuwa hafai akajilaza kitandani hapo kwa mke wa Redondo akawa ananiambia tuwashe gari twende Keko kulala lakini mke wa Redondo akamwambia 'shemeji nina hamu ya kwenda Ngwasuma' waliokuwa kwenye Ukumbi wa Maisha Club, akatuambia twende wote. Mafisango akakubali akamwambia ataenda kumfurahisha kwa heshima yake".

"Tumefika kule ndani tukanywa sana pombe akatuza wanamuziki, tulivyoondoka akang'ang'ania kuendesha gari badala ya yule Bozi (dereva) aliyekuwa anaendesha tangu mchana, tulikuwa watano kwenye gari pamoja na yeye, kila mara Bozi alikuwa anazozana na Mafisango kwa kuwa alikuwa anamwambia mbona Mafisango mbona haendeshi vizuri gari halafu iko kasi na anayumbisha usukani hautulii, yaani ilifika sehemu mpaka tunataka kumshusha yule Bozi, lakini akasema hashuki mpaka ahakikishe tumefika Keko na kupaki gari la bosi wake."

"Tulipofika pale Keko, taa zilituzuia tukasimama, zilipowaka za kijani tukaondoka lakini spidi Mafisango aliyotoka nayo pale ilikuwa kali ghafla tukavuka geti la kwanza la Veta tukaona guta mbele yetu, kwa vile gari ilikuwa kasi ikabidi Mafisango airudishe kulia kwa nguvu kumkwepa yule jamaa halafu baada ya kumpita akairudisha kushoto ndio hapo ikaingia kwenye mtaro ikapanda ikapinduka na nikachanganyikiwa nilipoona kichwa cha Mafisango kimenasa ndani kwenye sehemu ya gia halafu gari imekwisha na yule dada (rafiki wa mke wa Redondo) aliyekuwa amekaa naye mbele naye akawa kabanwa ikabidi nimtoe. "

"Pia nikamtoa na Mafisango akiwa anavuja damu na wakati huo alishafariki. Nikasimamisha taxi nikamkimbiza Muhimbili kufika pale wakanihakikisha kwamba amekufa sikuamini."

"Lakini Mafisango aliumia sana na kama si pombe aliyokunywa asingekufa."

Katika mazishi yake, watoto wake wote watatu walihudhuria ambao ni David, Patrina na Crespo aliyekuwa anaishi naye Dar es Salaam.
Crespo aliteka umati wa watu katika mazishi hayo kwani kila mmoja alitaka kumsogelea na kumtazama.
Read more...

`BOBAN` AANGUKA NA KUPOTEZA FAHAMU `AIRPORT`

0 comments
BOBAN akilia kwa uchungu siku aliyokufa Mafisango
KIUNGO wa Simba, Haruna Moshi Boban, ameanguka katika Uwanja wa Ndege wa N`Djili mjini Kinshasa kutokana na mapigo ya moyo kushuka ghafla.

Tukio hilo lilitokea jana Jumatatu wakati Boban akiwa anajiandaa kurudi Dar es Salaam baada ya kuhudhuria mazishi ya Patrick Mafisango aliyefariki Alhamisi iliyopita kwa ajali ya gari iliyotokea jijini Dar es Salaam.

Hali ya Boban ilibadilika ghafla akiwa uwanjani hapo na akashindwa kuona mbele kabla ya kulegea na kuanguka.

Madaktari wa uwanja huo walitumia zaidi ya saa 1:30 kumtibu Boban kabla hajarejea katika hali ya kawaida huku bado akiwa na simanzi kubwa kutokana na kifo cha Mafisango.
Boban alimwambia Mwandishi wa michezo wa gazeti la Mwanaspoti katika uwanja huo wa ndege wa Kinshasa,

"Nilimkumbuka sana Mafisango, wakati nikitafakari, nikaona ninalegea, nikashindwa kuona kitu chochote mbele na nikaanguka,"a

Daktari aliyemuhudumia Boban alisema 


 "Alikuwa na hali mbaya sana, mapigo ya moyo yalikuwa chini, yangeweza kuondoa maisha yake."

Licha ya kupata matibabu hayo, Boban pia alipewa kahawa kwa lengo la kuinua mapigo yake ya moyo.

Boban ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Mafisango ikiwa ni pamoja na kulala chumba kimoja wanapokuwa kambini Simba, aliwakilisha wachezaji wengine wa klabu hiyo katika msiba huo mjini Kinshasa.

Mwili wa Mafisango aliyekuwa akicheza nafasi ya kiungo enzi za uhai wake, ulizikwa katika makaburi ya Kinkole nje kidogo ya Kinshasa juzi Jumapili kuhitimisha safari yake ya miaka 32 ya uhai wake duniani.

Msimu huu akiwa na Simba alifunga mabao 12 akiwa ndiye kiungo pekee aliyefunga mabao mengi katika Ligi Kuu Bara alikofunga mabao 11. Jingine alifunga katika Kombe la Shirikisho.

Katika ajali yake iliyotokea eneo la Veta, Chang'ombe wakati akirejea kutoka klabu ya Maisha, alikuwa na rafiki zake ambao walipata majeraha madogo
Read more...

UJAUZITO WA LULU `WACHOROPOKA`

0 comments

 
Ujauzito wa mwigizaji nyota wa sinema Bongo ambaye yuko  Gereza la Segerea, Dar es Salaam kwa tuhuma ya kuhusika na kifo cha Steven Kanumba, Elizabeth Michael 'Lulu' umedaiwa kutoka.

Kwa mujibu wa taarifa za wachunguzi kupitia chanzo cha habari hizi sababu kubwa ya mimba hiyo kutoka ni kutunga nje ya mfuko wa uzazi hali ambayo ingemletea matatizo Lulu.
Chanzo kilisema bila kuainisha tukio hilo lilitokea lini:
“Nikwambie kitu, unajua wengi wanaamini Lulu ana mimba na hivi karibuini iliandikwa imefikisha miezi mitatu, ilikuwa sahihi, lakini ukweli ni kwamba kwa sasa imetoka.Sababu kubwa ni kwamba afya yake ilidorora, ukiachia ule ugonjwa wa U.T.I alioripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba anao, lakini kingine ni kuwa iligundulika ujazuito wake ulitunga nje ya mfuko wa uzazi ikawa haina jinsi, ikabidi kutolewa na kusafishwa.” 

Kikiendelea kuzungumza kwa umakini mkubwa, chanzo hicho kilidai kuwa  ujauzito huo ni wa tatu kuchoropoka kwa msanii huyo.
“Unajua huu unakuwa ujauzito wa tatu kwa Lulu kutoka. Kwa kweli kama si hivyo angekuwa na mtoto,” kilisema chanzo bila kuweka wazi nyingine mbili zilitoka kwa matatizo gani.
Chanzo hicho kilidai:
 “Kuna wakati Lulu alikwenda China, aliporudi alikuwa na ujauzito, lakini nao ulitoka, inaonekana ana matatizo kidogo kwenye upande wa kizazi,”  .
Kikaendelea:
 “Baada ya hapo, haukupita muda mrefu, akanasa nyingine ya mwanamuziki mmoja wa Bongo Fleva, pia hiyo nayo ikaja kutoka ya tatu ni hii ya Kanumba.”


Mchunguzi ambae alitumwa na chombo kimoja cha habari kwenda Gereza la Segerea ili kukutana na Lulu na kuzungumza naye ameelezea ugumu wa kumpata ‘laivu’ nyota huyo kutokana na ukweli kwamba kuna watu maalum watatu ambao ndio wenye ruhusa ya kumwona mtuhumiwa huyo,na si zaidi ya hao.
Hata hivyo, ‘shushushu’ huyo alifanikiwa kupata fursa ya kumjulia hali mahabusu mwingine aliyepo kwenye gereza hilo na ndipo akapata bahati ya kuonana na Lulu ambaye alionekana kuwa mnyonge.
Baada ya salamu, mchunguzi huyo alimtupia swali Lulu kuhusu afya yake na ya ujauzito alionao ambapo alijibu kwa mkato.
“Nani amekwambia mimi nina mimba?”


Baadhi ya mastaa wa sinema Bongo ambao hawakuwa tayari majina yao kutajwa, walipishana ‘kiswahili’ kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa ujauzito wa Lulu .
Wapo waliodai ujauzito huo ulitoka akiwa gerezani, wengine walidai ulitoka wiki moja kabla ya kifo cha Kanumba lakini wapo waliodai bado anao.
Staa wa kiume: 

“Lulu hana ujauzito, ulitoka. Ninavyojua mimi, wiki moja kabla ya kifo cha marehemu (Kanumba) ndiyo ulitoka, kwa hiyo hana.”
Staa wa kike:
 “Lulu bado ana mimba ila ni siri sana. Lakini hata nyie wenyewe si mmeona tumbo lile? anao!”
Staa wa kike: 

"Lulu mpaka anaingia kwenye matatizo kwa kifo cha Kanumba alikuwa na kibendi, hawezi kukitoa kwa sasa, maana yuko gerezani.”

Lulu anatarajiwa kufikishwa Mahakama Kuu ya Tanzania Mei 28, mwaka huu ili kujibu tuhuma zinazomkabili juu ya kifo cha Kanumba.
Read more...

Monday, May 21, 2012

IKWIRIRI YAGEUKA UWANJA WA VITA,MMOJA AFARIKI DUNIA

0 comments
  HALI  siyo shwari Ikwiriri wilayani Rufiji, baada ya watu wasiojulikana kuvamia nyumba ya Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD), kuivunja na kuharibu mali huku wengine wakichoma moto magari na nyumba za wananchi

Taarifa zinasema kuwa, vurugu hizo ziliibuka usiku wa kuamkia juzi kutokana na mapigano kati ya wakulima na wafugaji eneo hilo.

.
Vurugu hizo zilizosababisha kuigeuza Ikwiriri uwanja mdogo wa vita zimetokana na wananchi wenye hasira kali ambao walikuwa wanapinga mauaji ya mkulima Shamte Tawangala (60) mkazi wa Ikwiriri aliyeuawa kwa kupigwa na fimbo na vijana jamii ya wafugaji waliokuwa wakichunga ng'ombe katika shamba lake.
Kamanda Mangu alisema kuwa chanzo cha mauaji hao kinaelezwa kuwa ni wachungaji hao kutaka kulishia mifugo yao kwenye shamba la mahindi la Tawangala, na alipojaribu kuwakataza walianza kumshambulia kwa fimbo maeneo mbalimbali ya mwili wake hadi kufariki dunia.

 Habari zinadai kuwa, mapambano kati ya polisi na wananchi  yalizuka baada ya watu kuamua kuingia barabarani kupinga kukamatwa kwa wenzao zaidi ya 20, na pia kukaidi kutimizwa kwa ombi lao la kutaka waachiwe huru.


Akizungumzia kukamatwa kwa wananchi hao, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ernest Mangu alisema watuhumiwa hao walitiwa mbaroni juzi wakati wa vurugu kati ya wakulima na wafugaji ambazo zilidumu kwa zaidi ya saa sita kupinga mauaji ya mkulima yaliyofanywa na wafugaji ambao walikimbia baada ya tukio hilo.
Kamanda Mangu alisema kuwa kabla ya watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani juzi asubuhi, zilizuka vurugu nyingine zilizofanywa na wananchi ambao walikuwa wakishinikiza kuachiwa wenzao waliokuwa wamekamatwa.
“Ni kweli leo (juzi) asubuhi muda wa saa tatu wananchi walianza tena vurugu kushinikiza wenzao waliokamatwa na polisi waachiwe, walianza kwa kuchoma matairi, lakini vurugu hizo hazikuchukua muda mrefu kwa kuwa askari wa kutuliza ghasia tunao, na waliweza kuzima vurugu hizo na zoezi la wenzao kufikishwa mahakamani likafanyika kama lilivyopangwa,”alisema Mangu.
Aidha, alisema kuwa katika vurugu hizo wapo ambao wamekamatwa, lakini idadi yao haijajulikana kwa kuwa wako kwenye mahojiano na polisi na watakapobainika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.


Mangu alisema  walikuwa wanashikilia watu 50 kwa tuhuma za kufanya vurugu, ikiwamo kufunga barabara na kuharibu mali kadhaa.
Alisema wanaoshikiliwa siyo wafugaji wala wakulima, hivyo kama kuna taarifa za kuwapo ulipizaji kisasi siyo sahihi kwani kati ya makundi hayo hakuna kundi lililochukuliwa zaidi ya vijana wa mjini waliokuwa wakifanya vurugu.

“Sisi hatujawakamata wafugaji au wakulima, katika operesheni ilikuwa ya kukamata watu waliokuwa wakifanya vurugu ndiyo tunaowashikilia, sasa ukisema kuna madai ya wafugaji kutaka kulipiza kisasi hapo nashangaa kwa maana mbili, kwanza siku ya fujo hakuna hata mfugaji mmoja aliyelipiza kisasi kwa mkulima,”alisema Mangu na kuongeza:

 “Kweli wafugaji walionyesha kutii walau sheria kwa sababu, licha ya baadhi ya watu kudai wakulima wanawashambulia, wao walikuwa hawajajibu mashambulizi ndiyo maana vurugu hizi tumeweza kufanikiwa kuzizima mapema, lakini kama wafugaji nao wangeenda kuwapiga wakulima hapo sasa kazi ingekuwa ngumu.”   
 MILIO ya mabomu ya machozi na vita ya mawe baina ya askari wa Jeshi la Polisi na wananchi, viliendelea kwa siku mbili, ambapo watu 50 wamekamatwa na kufikishwa mahakamani.
Chanzo cha habari hii kilishuhudia mapambano baina ya polisi waliokuwa wakiwatupia mabomu ya machozi wananchi walioonekana mbele yao, ambao nao katika kujibu mapigo waliwashambulia askari hao kwa mawe.
Polisi hao walilazimika kutumia mabomu hayo, na kufanikiwa kuwakamata watu wengi ambao walikuwa wakikimbia bila mpangilio baada ya kuzidiwa na moshi wa mabomu hayo, katika kutuliza ghasia na mapigano yaliyozuka baina ya wakulima na wafugaji yaliyozuka juzi baada ya kuuawa kwa mkulima mmoja na vijana wawili jamii ya wafugaji.


Mmoja wa wakazi wa eneo hilo alisema kuwa, shughuli zote tangu mtaa wa Kaunda hadi eneo la Mwembemhuro kuelekea bonde la Mto Rufiji, zilifungwa na magari yote yalizuiwa kuingia katikati ya mji wa Ikwiriri.

Taarifa kutoka Jeshi la Polisi zimeeleza kuwa, zaidi ya nyumba saba, duka moja na magari kadhaa yaliharibiwa katika tukio hilo.
Mangu alisema kuwa hadi sasa maofsa wa polisi Mkoa wa Pwani wakiwa na helkopta, wameweka kambi katika eneo hilo ili

.

Wakati hayo yakiendelea, watu 49 kutoka jamii ya wafugaji wamehamia na kuishi na familia zao Kituo cha Polisi Ikwiriri, kuepuka vurugu zinazoendelea mitaani ambazo juzi ziliripotiwa kupoteza maisha ya mkulima mmoja.
Ingawa polisi wanasema hali ni shwari, taarifa zilizothibitishwa na watendaji wa chini zinaeleza siyo shwari na wakati wowote vurugu zinaweza kurudi tena.

Katika eneo la Ikwiriri inakopita barabara kuu ya Dar es Salaam- Mtwara,  tangu juzi  biashara ya maziwa iliyokuwa ikifanywa na wake wa wafugaji haikuwapo, inadaiwa wamehofia usalama wao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ernest Mangu,  alisema wanaendelea kufanya doria  ili kujiridhisha.
Pia, Mangu alisema lengo la doria hizo pia ni kuhakikisha kinachosemwa na baadhi ya watu kuwa, kuna dalili za kurejea vurugu iwapo ni kweli au la.

Kuhusu madai ya ofisa mmoja wa jeshi hilo kuhamishwa kituo cha kazi siku hiyo ya tukio, Mangu alisema hana taarifa hizo.

*PICHA YA SATELLITE KWA MSAADA WA GOOGLE GEOEYE
Read more...

Sunday, May 20, 2012

`DOGO` BOSI WA FACEBOOK,MARK ZUCKERBERG, AFUNGA NDOA KWA STAILI SIKU YA JUMAMOSI

0 comments
Mwanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Facebook, Mark Zuckerberg, amefunga ndoa siku ya Jumamosi na rafiki yake wa kike  wa siku nyingi msichana mwenye asili ya China, Priscilla Chan.
Zuckerberg kijana bilionea mwenye umri wa miaka 28 alitangaza rasmi tukio hilo kwa washabiki wake wa Facebook kupitia Timeline yake


Wawili hao walianza mahusiano wakiwa Chuo Kikuu cha Harvard na wamekuwan imara kwa takriban miaka 9 sasa.Walilishana kiapo katika sherehe isiyokuwa kubwa upande wa nyuma wa nyumba yao huko Palo Alto,California.Kitendo hicho kilileta hali ya mshangao kwa wageni waalikwa wasiopungua 100,kwa mujibu wa  jarida la People,kwa kuwa wengi wao walidhani ni sherehe za kuhitimu kwa Priscilla,ambae tarehe 14 mwezi huu alipata shahada ya chuo kikuu ya elimu ya afya ya watoto kutoka Chuo Kikuu cha California cha San Fransisco(UCSF)

Hii ni Historia yake

Inasemekana Zuckerberg ndie aliebuni pete ya Priscilla ambayo ni ya kawaida tu iliyonakshiwa kidogo na chembe chembe za madini ya ruby,hata mavazi aliyovaa yalionekana kuwa `simple`
Add caption
Zuckerberg kijana ambaye anasifika kwa kufanya mambo yake `simple` alitoa taarifa za tukio hilo katika hali ya kawaida sana kwa kubadilisha status ya kwenye Timeline yake kutoka `in relationship` na kuwa `married`,status ambayo watu zaidi ya laki 8 wame `like` kwa masaa 24 iliyokaa mtandaoni.Muda mfupi baadae dada wa Mark aitwae Arielle aliandika katika facebook yake "Balls.Now I`m the only unmarried Zuckerberg." Na bibi harusi Priscilla nae alimuweka Arielle kama `family member` wake mpya

Kijana Mark Zuckerberg ana hisa zenye thamani isiyopungua dola za kimarekani bilioni 20.Kampuni yake ya Facebook ambayo kwa mara ya kwanza kabisa imeingia katika biashara ya hisa,imeanza  katika mnada wao wa kwanza uliofanyika Ijumaa kwenye eneo lao la Facebook Silicon Valley.Mnada wao wa awali haukwenda vyema kama matarajio ya kampuni yalivyokuwa huku kila hisa zikipnda bei kidogo tu kutoka bei ya mnada ya dola 38 kwa hisa na kuuza asilimia 25 tu ya hisa zao zote.Zaidi ya hisa milioni 576 ziliuzwa na kubadili rekodi ya soko la awali la hisa nchini Marekani.Mwaka jana Facebook iliingiza mapato ya dola za kimarekani bilioni 3.7 na kuvuna faida ya dola za kimarekani bilioni 1.Facebook ina watumiaji wamtandao huo wapatao milioni 900 duniani kote


Kuibuka kwa Facebook na kuleta maajabu ya kiutamaduni duniani kulipelekea kutengenezwa kwa filam iitwayo `Social Network` mwaka juzi.Zuckerberg alianzisha mtandao wa Facebook akiwa bwenini katika chuo alichokuwa akisoma cha Havard miaka minane iliyopita.
\
Si Zuckerberg wala Chan ambao wameongezea chochote kwenye facebook zao kuhusu ndoa yao na watu wa habari wamekuwa wakituma e-mail kwa wahusika katika kampuni ya Facebook ili kupata ufafanuzi zaidi,lakini hazijajibiwa.

Read more...

WASTARA AZUNGUMZIA HALI YA MUMEWE NAYE PIA AKIWA AMELAZWA

0 comments

Mke wa Sajuki (Wastara) ambae yuko India kwa sasa akiwa anamuuguza mumewe (Sajuki) amezungumza kwa mara ya kwanza na mtandao wa millardayo.com kuhusu hali ya sasa ya Sajuki.
Amesema “kwa kweli hali imebadilika na ninategemea kuona hali nzuri zaidi leo (jana) ni siku ya tano toka tumekuja huku India, Sajuki amebadilika sana kwa sababu siku tulipoondoka Tanzania hali yake ilikua mbaya hata rangi alibadilika lakini kwa sasa amerudi kwenye hali ya kawaida”
Kwenye sentensi nyingine, Wastara amesema Sajuki alikua hawezi hata kuongea ukamuelewa, sasa hivi anaongea hata kwa mda wa saa moja kitu ambacho alikua hawezi kabisa na sasa hivi ameweza kukaa kabisa”
 
Wastara amesema “changamoto tuliyonayo ni kwamba tunahudumiwa na watu mbalimbali ukiachana na dokta, hawajui kiingereza sasa unaweza kukuta unahitaji kitu lakini hamuelewani, kitu kingine ni swala la chakula, chakula ni kipya kwetu wote wawili huku ni Asia wana vyakula vyao”
Kuhusu Ugonjwa wa Sajuki, Wastara amesema walivyoondoka Tanzania walijua wanakwenda India na Sajuki atatibiwa ugonjwa unaomsumbua moja kwa moja lakini kabla ya kufanyiwa chochote ikagundulika kwamba alikua na tatizo la pumzi hivyo haikuwezekana kutibiwa ugonjwa wake kwa sababu inatakiwa kabla ya kufanyiwa opareshen anatakiwa kuwa kwenye hali ya kawaida, kwa hiyo ametibiwa kwanza tatizo la pumzi ili aweze kuhema vizuri ndio aanze kutibiwa ugonjwa wake”
Kwa kumalizia Wastara amesema “mimi pia nilipofika tu India nilikua mdhaifu, nilipoteza Network zote ikabidi nilazwe kwa sababu nilikua hoi, hapa yenyewe nimelazwa lakini naendelea vizuri
SOURCE:millardiayo.com 
Read more...

Thursday, May 17, 2012

MAREKANI YARUHUSU DAWA MPYA YA KUZUIA UKIMWI IANZE KUTUMIKA

0 comments
MAMLAKA ya Chakula na Dawa ya Marekani (FDA), imeidhinisha dawa ya Truvada kuwa tiba ya kuzuia kuenea kwa Virusi Vya Ukimwi (VVU).Dawa hiyo ambayo awali ilikuwa katika kundi la zile zinazotumiwa kwa ajili ya Kupunguza Makali ya VVU (ARV), imepandishwa chati wakati ambapo tayari ipo sokoni ikiuzwa kama moja ya ARV za kawaida.

Kwa mujibu wa maelezo ya FDA, mwathirika anayetumia dawa hiyo anaweza kujamiiana na mwenza wake ambaye hana VVU bila kutumia kondomu na hatomuambikiza.

Matokeo ya utafiti huo yaliwahi kuchapishwa kwenye gazeti hili toleo la Februari 12, mwaka huu na sasa kilichofanyika ni FDA kuidhinisha Truvada ambayo ilionyesha kufanya kazi vizuri ikilinganishwa na ARV nyingine.

Uidhinishaji wa dawa
Jopo la wanasayansi 22 wa FDA waliokutana Jijini Washington wiki iliyopita, walipitisha Truvada baada ya kupitia ripoti ya utafiti kuhusiana na ufanyaji kazi wa dawa za ARV.

Wanasayansi hao waliisifu dawa hiyo baada ya kuonekana kufanya kazi vizuri kwa watu waliopo kwenye hatari ya kuambukizana VVU kwa kasi zaidi.

Kwa namna dawa hiyo inavyofanya kazi, mwathirika akiitumia hawezi tena kumwambukiza mtu mwingine ambaye atashiriki naye tendo la ndoa bila kutumia kondomu.

Lakini, dawa hiyo masharti yake hayatofautiani na yale ya ARV kwani mtumiaji atapaswa kuitumia maisha yake yote ili kumwekea kinga asiwaambukize wengine na yeye aishi muda mrefu.

Kulingana na ripoti ya utafiti uliofanyika Marekani, dawa hiyo ina uwezo wa kuzuia maambukizi ya VVU hadi asilimia 90.Hata hivyo, kwa watu ambao wamekuwa wakitumia dawa holela hasa za ARV, hali imekuwa tofauti kwani Truvada imeonekana ikifanya kazi kwa kiwango cha asilimia 44 tu.

"Hii ni ishara kwamba kuna kundi la watu ambao dawa hiyo haitafanya kazi kikamilifu kutokana na mazingira ya matumizi ya dawa holela,"ilisema sehemu ya ripoti.

Hata hivyo, wanasayansi wanasema  tatizo hilo linafanyiwa uchunguzi ili kupata njia bora ya kukabiliana na tatizo hilo.

Faida ya Truvada
Wataalamu wameeleza kwamba itasaidia watu ambao wana VVU lakini, hawapendi kufanya tendo la ndoa kwa kutumia kondomu."Leo ni siku ya tukio la kuwasisimua wengi katika kuzuia maambukizi ya HIV,” alisema mmoja wa wataalamu kutoka Taasisi ya kujitolea kusaidia jamii ya Fenway, Dk Kenneth Mayer ambaye alikuwa miongoni mwa wajumbe wa FDA walioipitisha dawa hiyo.

"Ingawa (Truvada) haikuweza kuonyesha uwezo wa asilimia 100 kuzuia maambukizi ya VVU, namna inavyofanya kazi itakuwa na matokeo mazuri ya kupambana na Ukimwi duniani,” alisema Dk Mayer.

Tahadhari
Hata hivyo, wataalamu hao walihimiza kuwepo kwa uchunguzi zaidi wa kitafiti ili kujua kama Truvada itafanya kazi vizuri duniani kote.Mtaalamu wa Dawa kutoka Taasisi ya Taifa ya Saratani nchini Marekani (NCI),  Dk Lauren Wood alilalamika akisema kuwa utafiti huo haukuzingatia matatizo ya figo.

Alisema matatizo ya figo yamekuwa yakijitokeza kwa waathirika wengi wa Ukimwi hasa barani Afrika."Mimi sikufurahishwa sana kwa sababu utafiti huu haukuzingatia maeneo ambayo watu wengi wako kwenye hatari ya maambukizi,” alisema Dk Wood.

Lakini, alisema utafiti uliofanyika nchini Marekani umeonyesha wazi kwamba ni dawa inayoweza kupunguza kwa kiwango kikubwa kasi ya kusambaa kwa VVU.

Wataalamu kadha nao walisema pamoja na Truvada kupitishwa na FDA, ni lazima maelezo ya kitaalamu yatolewe kwa madaktari ili wawe na uelewa wa kutosha kuhusu matumizi yake.

Mabingwa hao walipendekeza kwamba, wanaotumia kabla ya kuruhusiwa kutembea na wenzi wao bila kondomu lazima wachunguzwe kitaalamu ili wajulikane kama dawa iyo imewakubali au la.

Mwanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Afya cha Cincinnati, Dk Judith Feinberg alikosoa ripoti ya uchunguzi akisema ilipaswa kwenda mbali zaidi katika kuchunguza madhara yanayoweza kujitokeza kwenye matumizi ya dawa hiyo.“Tusipokuwa makini katika hilo, tunaweza tukawa tumepitisha jambo ambalo litasababisha madhara zaidi kuliko faida,” alionya Dk Feinberg.


Utafiti wa ARV
Wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Johns Hopkins ni miongoni mwa wale ambao walifanya uchunguzi juu ya ARV, kuwa moja ya dawa zinazopunguza maambukizi ya VVU.

Watafiti hao walibainisha kuwa wale wanaotumia ARV baada ya muda fulani, huweza kushiriki tendo la ndoa bila ya kutumia kondomu na mtu ambaye hana VVU na asimwambukize kwa asilimia 95.

Mkuu wa Mtandao wa Maabara za Kuchunguza VVU katika chuo hicho, Profesa Susan Eshleman alisema kwenye ripoti ya ugunduzi huo, wamebaini dawa za kurefusha maisha kwa waathirika wa HIV, sasa zinaweza kutumika kama sehemu ya kuzuia maambukizi.

Profesa Eshleman alisema kwamba, mwathirika wa VVU anayetumia ARV kikamilifu, anaweza kujamiiana na mtu ambaye hana virusi bila kondomu na asimwambukize.

“Huu ni ugunduzi wa kustajabisha,” alisema Profesa Eshleman akifafanua: “Matokeo haya yameleta mapambazuko mapya katika sayansi ya kuzuia maambukizi na inawaweka watafiti kwenye mazingira mazuri zaidi ya kupata suluhisho la kukabiliana na maradhi haya.”

Walivyogundua
Profesa Eshleman anasema utafiti huo walioupa jina la HPTN 052, walifanya kupitia maeneo mbalimbali ya dunia.

Kwenye ripoti hiyo ambayo pia ilichapishwa kwenye jarida maarufu la kisayansi linaloitwa Science, watafiti hao walisema mtu anapotumia ARV, hufikia wakati fulani wingi wa virusi mwilini hupotea kiasi kwamba anakuwa karibu sawa na yule ambaye hajaambukizwa.

“Jambo la msingi katika utafiti huu ni kwamba dawa hizi za kurefusha maisha zinapotumiwa kikamilifu, hupunguza mzigo wa virusi mwilini kwa zaidi ya mara 200. Ni sawa na kusema inapunguza hadi kufikia karibu na sifuri,” inaeleza ripoti hiyo.

Ni katika mazingira hayo, ripoti hiyo inasema kuwa damu ya mwathirika inakuwa haina virusi na hivyo uwezekano wa kumuambukiza mpenzi wake unakuwa haupo.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa ARV inafanya kazi mbili, kwanza kurefusha maisha ya mwathirika kwa kupunguza virusi mwilini na pili ni kumkinga asiambukize wengine.Sifa nyingine ya ARV, alisema ni kupunguza uwezekano wa waathirika kupata ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) kutokana na kiwango cha kinga za mwili kuongezeka.
SOURCE: mwananchi.co.tz
Read more...

BOY FINDS HUMAN FINGER IN HIS SANDWICH!

0 comments
Ryan Hart, a 14-year-old boy from Jackson, Michigan, had a rude surprise when he bit into his Arby's roast beef sandwich. "I was like, 'that's got to be a finger,'" he told reporters. "It was just nasty."
Reportedly, a restaurant employee cut off her finger with a meat slicer while preparing the meal. She left her station to deal with the emergency, and other employees, who were unaware of the injury, continued to complete the order.
"Somebody loses a finger and you keep sending food out the window," said the teen's mom, Jamie Vail. "I can't believe that." She added that following the gruesome discovery, her son was "traumatized," couldn't eat or sleep, and had been prescribed medication.
Ryan Hart
John Gray, Arby's vice president of corporate communications, gave the official Arby's statement:

"Arby’s wants to reassure customers, we are committed to providing quality food in a safe and healthy environment
We are deeply concerned and apologetic to the guest involved in this unfortunate incident. This is an isolated and unfortunate accident occurred in a franchisee’s Jackson, Michigan restaurant in which an employee was injured.
After learning of the incident, the franchisee’s restaurant team shut down food production and thoroughly cleaned and sanitized the restaurant. The franchisee fully cooperated with the Health Department during the investigation, and the restaurant was given the approval to remain open."

This is not the first time human remains have been found in a fast food meal but this case might be the most extreme.
•    A Dayton Ohio man sued Arby's in 2005 for serving his chicken sandwich with human skin on top.
•    An Albany-area man found a bandage with blood on it in his pizza crust at Pizza Hut last year
•    Also in 2011, Texan woman found blood on her French fries at a Houston area Crackle Barrel.
Read more...

LULU ANAUMWA

0 comments
Elizabeth ` LULU` Michael

Habari  zinaeleza kuwa staa wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amekwaa gonjwa baya akiwa mahabusu katika Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam.

Akizungumza  baada ya kuonekana kwenye duka moja  linalouza madawa ya binadamu,  Kinondoni, hivi karibuni, rafiki wa karibu wa Lulu alisema kuwa alikuja kununua dawa za kumpelekea Lulu gerezani kwa kuwa amepatwa na ugonjwa unaomshambulia sehemu nyeti wa Urinary Tract Infections (U.T.I).

“Namchukulia Lizzy (Lulu) dawa, amepata U.T.I, si unajua mazingira ya usafi kwenye vyoo vya gerezani? Ni rahisi sana mtu kupata au kuambukizwa U.T.I kwa sababu ni vyoo vya public (vinavyotumiwa na watu wengi),” alisema rafiki huyo ambaye huwa  gerezani hapo mara kwa mara.

  Lulu  anaendelea vizuri huku hofu kubwa ikiwa kwenye ujauzito wake kuhofiwa usije   kutoka.

Lulu yupo ndani ya mahabusu ya Segerea kwa tuhuma za kuhusika na kifo cha msanii mwenzake Steven Kanumba na atafikishwa tena mahakamani  Jumatatu hii.



Read more...

SAUDI MILLIONAIRE BUYS A BOTTLE OF WINE FOR $136,000

0 comments
A Saudi millionaire splurged $136,000 on a bottle of champagneat Dubai’s glitzy Cavalli club over the weekend, a UAE newspaper reported on Tuesday.
“The Saudi Arabian and his friends guzzled” a bottle of Louis Roederer Cristal in the early hours of Saturday morning, the 7DAYS newspaper said.
The vintage bottle was “one of just three believed to be available worldwide,” the paper added. The other two were for sale at nightclubs in New York and London.
According to 7DAYS, the Cristal bottle was from a “batch made in 1990 in Champagne, France,” originally intended for the Millenium celebrations.
Club’s manager David Lescarret would not divulge the Saudi’s total bill for the night, saying only that it was “very high” and included a “luxurious dinner.”
The manager said the Cavalli club bought the champagne at a Christie’s auction house in London at a cost of around $93,000.
Read more...

MAFISANGO KUAGWA LEO,RAGE AELEZA KILICHOTOKEA

0 comments
Hili ndio gari alilopata nalo ajali marehemu Mafisango

Leo Ijumaa watu watapata fursa ya kuuaga mwili wa marehemu Patrick Mafisango kwenye  viwanja vya TCC Club Chang'ombe jijini Dar es Salaam. kuanzia saa nne asubuhi (awali ilikuwa imepangwa mwili uagwe katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni) . Taarifa zilizotolewa baadaye na msemaji wa familia zimetaarifu kuwa mwili wa marehemu Patrick utasafirishwa na ndege ya saa kumi tayari kwa kuzikwa katika mji aliozaliwa wa Kinshasa huko nchini Congo DRC (awali taarifa zilizotolewa na meneja wa Simba Nico Nyagawa zilizema mwili wa Mafisango baada ya kuagwa utaondoka na kusafirishwa na ndege ya shirika la KQ kuelekea kwao Rwanda kwa ajili ya kuzikwa).

Anaelia ni mmoja wamarafiki wa marehemu Mafisango ambao alikuwa nao ndani ya gari



Haruna Moshi `BOBAN` akilia kwa uchungu jana msibani
 Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, marehemu Patrick alipata ajali alfajiri ya kuamkia jana Alhamisi katika maeneno ya TAZARA alipokuwa akiendesha gari na kutaka kuziwahi taa za kuongozea barabara na ndipo alipokutana na mwendesha pikipiki (taarifa nyingine zinasema ni mwendesha baiskeli ya matairi matatu - guta) na katika harakati za kujaribu kumkwepa kwa bahati mbaya gari lake lilikosa uelekeo na kugonga mti kisha kuingia mtaroni na kusababisha ajali iliyomwacha na majeraha makubwa.
BOBAN na wenzake wakiwa msibani

Ndani ya gari hilo inasemekana alikuwa ameambatana na mdogo wake pamoja na rafiki zake wakirejea kutoka kwenye klabu ya starehe. Patrick aliaga dunia muda mfupi baadaye alipokuwa akiwahishwa hospitalini. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam na maombolezo ya msiba yapo kwenye nyumba iliyopo maeneo ya Keko Toroli jirani na kituo cha Chang’ombe Maduka Mawili (Njia Panda ya Sigara).

Patrick alijiunga kuichezea Simba SC mwaka jana, akitokea timu ya Azam FC aliyojiunga nayo alipohamia nchini Tanzania miaka mitatu iliyopita. Awali alkuwa akiichezea APR ya Rwanda. Video za baadhi ya magoli aliyowahi kufunga zipo youtube.

Akina mama ambao ni washabiki wa marehemu Mafisango wakilia kwa huzuni msibani jana
 Patrick alizaliwa tarehe 9 Machi 1980 mjini Kinshasa, Kongo D.R.C lakini alikuwa na uraia wa Rwanda

Amefariki siku chache tu baada ya kocha wa timu ta taifa ya Rwanda, Milutin Sredojovik (Micho) kumuita kujumuika katika timu ya Taifa ya nchi hiyo kwa ajili ya maandalizi ya mechi za kuwania kufuzu kucheza kombe la dunia 2014.
Read more...

Wednesday, May 16, 2012

PATRICK MAFISANGO WA SIMBA SC AFARIKI DUNIA KWA AJALI ALFAJIRI YA KUAMKIA LEO

0 comments
MCHEZAJI Patrick Mafisango wa timu ya Simba ya Dar es Salaam amefariki dunia leo kwa ajali ya gari katika eneo la Tazara jijini Dar es Salaam. Taarifa ambazo zimetolewa kutoka Klabu ya Simba zimesema Mafisango amefariki dunia leo asubuhi kwa ajali ya gari maeneo ya Tazara. Mtandao huu utawaletea taarifa zaidi za tukio hilo muda mfupi baadaye. Mtandao huu pia unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na klabu nzima ya Simba kwa pigo hilo.
Read more...

Tuesday, May 15, 2012

MARA BAADA YA KUFIKA INDIA WASTARA AONGELEA TATIZO LILILOJITOKEZA

0 comments
Wastara wakati akichangisha hela ya matibabu ya Sajuki katika kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm

Wastara,Mke wa msanii wa filam za kibongo,Juma `Sajuki`Kilowoko aliongea katika kipindi cha `Leo Tena` na Dina Marios kwa njia ya simu moja kwa moja kutoka India ambako Sajuki ameenda kwa ajili ya matibabu.Dina ameyaweka maongezi hayo kwenye blog yake ya dinamarios.blogspot.com.Haya ndio maongezi yao:
SOURCE:www.dinamarios.blogspot.com
Read more...

Katherine Jackson Discuss Conrad Murray, Says He’s Not Serving Enough Jail Time

0 comments
Katherine has said that she’s never met Dr Murray nor, to her knowledge, has he ever reached out to meet her.  And she’s also expressed her feelings on his sentence, noting that she doesn’t think four years is long enough.  You can tell this will be a really emotional interview; she appears sad and teary eyed throughout the entire clip.
Read more...

PICHANI LIVE! KIJANA ALIVYOBAMBWA UBUNGO AKICHUNA MBWA KWA AJILI YA BIASHARA YA MISHIKAKI

0 comments
PICHA KUTOKA THE CHOICE TZ
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797