Pages

 

Thursday, June 28, 2012

CHADEMA YATOA TAMKO KUHUSU MKASA WA DK.ULIMBOKA

0 comments
Benson Kigaila, Mkurugenzi wa mafunzo na organization Chama Cha Demokrasia na Maendeleo. akitoa tamko la chama hicho juu ya kutekwa na kuteswa mwenyekiti wa madaktari dk Ulimboka steven, katika makao makuu ya CHADEMA Mtaa wa Ufipa Kinondoni, leo mchana
Mkurugenzi wa Mafunzo na Oganaizesheni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo,CHADEMA,Bw.Benson Kigaila leo mchana ametoa tamko la chama hicho juu ya utekwaji nyara wa Kiongozi wa Jumuia ya Madaktari Tanzania,Dk.Ulimboka Steven,ambae usiku wa kuamkia jana alitekwa nyara na watu wasiojulikana,kujeruhiwa na kutelekezwa katika maeneo ya Pandemabwe nje kidogo ya jiji la Dar Es Salaam.
Mbele ya waandishi wa habari katika ofisi za makao makuu ya chama hicho Mtaa wa Ufipa,Kinondoni ,jijini Dar Es Salaam,Bw.Kigaila amesema: 
"Suala hili la kutekwa Dk ulimboka linatukumbusha miaka ya sabini wakati wagombea haki walivyokuwa wakipotea katika hali za kutatanisha. Matukio mengi ya kuuwawa wagombea haki nchini yanatuonyesha ni namna gani serikali yetu ni dhaifu na bunge lina meno ya plastic. 

Chadema tunadhani na ni ukweli ulio wazi kuwa tukio hili lina mkono wa serikali, IGP Mwema mtaalamu wa kuoteshwa kutokea vurugu katika maandamano ya chadema iwapi inteligensia yake katika hili?

Serikali haina nia thabiti ya kumaliza tatizo la madaktari maana imeamua kuongeza mishahara kwa baadhi ya watendaji wa serikali mpaka kufikia milioni kumi kwa mwezi, mfano ikulu inakarabatiwa kila mwaka kwa kutumia bilioni 6, hii ni hatari. Halafu wanatuambia serikali haina fedha za kumaliza tatizo la madaktari.. "
PICHA NA HABARI KWA HISANI YA HAFIDH KIDO (JEMBE)

Read more...

MKASA WA KIONGOZI WA JUMUIA YA MADAKTARI TANZANIA ALIYEKUWA AMETEKWA

0 comments


Mweneyikiti wa Jumuia ya Madaktari nchini Dk Stephen Ulimboka, ambae amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kutekwa nyara, kupigwapigwa na kujeruhiwa vibaya na watu wasiofahamika,ameongelea tukio zima lililomkuta.

Taarifa zinasema kwamba madaktari wanaomhudumia wamesema kuwa Dkt Ulimboka  amevunjwa mbavu, miguu yote miwili, kang’olewa meno yote ya mbele na kuumizwa vibaya katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

Tukio hilo la kikatili na kusikitisha limetokea usiku wa kuamkia jana jijini Dar es Salaam, na linadaiwa kufanywa na watu wasiojulikana ambapo kabla ya kufanya unyama huo walimteka nyara na baadae  kumtelekeza katika eneo la msitu wa Pande Mabwepande.

Akisumulia tukio hilo Dkt Ulimboka alisema kuwa  juzi usiku alipigiwa simu na mtu aliyejitambulusha kwake kuwa anaitwa Hemed, aliyemwambia kuwa anahitaji kuongea naye, na ndipo walipopanga kuonana katika eneo la Leaders Kinondoni.

Dk Ulimboka aliyekuwa akiongea kwa taabu, aliendelea kusimulia kuwa wakati akiongea na mtu huyo anayekiri kuwa alikuwa akifahamiana naye kabla, alikuwa na wasiwasi kwani kila mara alikuwa akipokea simu na kuwasiliana na watu wengine ambao hawakuwapo eneo hilo.

Alisema baada ya muda alishangaa kuona wanaongezeka watu wengine watano wakiwa na silaha, kisha wakamwambia kuwa anahitajika kituo cha Polisi na kumvuta na kumuangusha barabarani kabla ya kumuingiza katika gari lenye rangi nyeusi na kuondoka naye.

Dkt Ulimboka alisema kuwa wakiwa njiani walimpiga, na kumfikisha katika msitu huo wa Pande na kuendelea kumpiga hadi akapoteza fahamu.

  Taarifa zaidi zinasema mmoja wa madaktari wenzie aliyefahamika kwa jina moja la Dkt Deo, ameongelea mksa huo na kusema  kuwa alipigiwa simu na mtu hasiyemfahamu na kumfahamisha tukio hilo.

Alisema alipofika katika kituo cha Polisi cha Bunju, alimkuta akiwa katika hali mbaya na ilikuwa ngumu kumtambua kwakuwa alikuwa na majeraha mengi eneo la usoni.

Aliongeza kuwa akiwa na wenzie waliamua kumchukua na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwaajili ya matibabu.

"Hali yake kwa kweli niliikuta mbaya sana, alipigwa mno na ameumizwa kwa kweli tumemleta hapa hili aweze kupata matibabu, lakini mimi nilivyomkuta mara ya kwanza nilishindwa hata kumtambua kwa jinsi alivyokuwa ameumizwa"alisema Dkt Deo

Alisema kuwa alisimuliwa na Dkt Ulimboka kwamba watu hao waliomteka na kumpiga walikuwa na silaha na kwamba alishindwa kuwatambua.

Aliongeza kuwa Dkt Ulimboka alidai kuwa wakati akiwa katika hali mbaya alikuwa akisikia mazungumzo yao, wakibishana juu ya kumuua wengine wakisisitiza achomwe sindano, na wengine wakitaka kumpiga risasi.

Alisema wakati mabishano yakiendelea kati yao, Dkt Ulimboka aliinuka akiwa na lengo la kukimbia lakini watu hao walipiga risasi
hewani iliyomshtua na kuangua chini.

Kwa upande wake Dkt Cathbeth Mcharo ambaye ndiye aliyempokea Dkt Ulimboka Hospitalini hapo, alisema kuwa hali yake ni mbaya na kwamba wanajitahidi kumpatia huduma za haraka.

Alisema kuwa kwa hatua za awali amefanyiwa vipimo mbalimbali, hili iweze kufahamika aina ya matibabu anayotakiwa kupatiwa.
Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova amezungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo la utekaji nyara na kujeruhi lililompata kiongozi mgomo wa Madaktari Steven Ulimboka anayedaiwa kutekwa na watu watano wakati akipata kinwaji katika klabu ya Leaders Kiondoni jijini Dar es salaam.

Kamanda Kova amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye hakutaka kumtaja jina lake kiusalama na kutoharibu upelelezi kuwa msamaria mwema huyo alimuokota Ulimboka katika msitu wa Mabwepande na kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo polisi aliyekuwa zamu alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Kamanda Kova amesema jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara, kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini, ameongeza kwamba wahusika wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo

Wakati hayo yakitokea inadaiwa kuwa Askari Kanzu mmoja alikumbana na kipigo kikali kutoka kwa madaktari hapo Muhimbili kwa kile kilochodaiwa kutambuliwa na Dkt Ulimboka kuwa mmoja wa watu walio mjeruhi.

Pia inadaiwa kuwa Askari huyo aliingia chooni na kufanya mawasiliano na wenzake huku Madaktari hao wakimsikiliza na kutokana na alichokua akiongea chooni humo ndipo alipotoka aliambulia kichapo kikali.

Pia baadhi ya madkatari na wauguzi walikuwa wakisukuma gari alilokuwa amepanda Dkt Ulimboka huku wakiimba nyimbo za Umoja na Mshikamano Daima miongoni mwao.

Hali ya ulinzi ilikuwa kali Hospitalini hapo kwani Picha zilikuwa haziruhusiwi kupigwa.

ZINAZOHUSIANA NA HII: 
  
Read more...

Wednesday, June 27, 2012

KIONGOZI WA MGOMO WA MADAKTARI AOKOTWA AKIWA HAJITAMBUI

0 comments
Mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari  nchini, Dk Stephen Ulimboka amelazwa katika hospital ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuokotwa katika pori la Pande nje kidogo ya jiji akiwa taaban.Inasemekana Dk Ulimboka alitekwa jana na watu wasiojulikana.
  
Helen Kijo-Bisimba wa LHRC amenukuliwa katika East Africa Redio,ambaye amekariri maelezo ya Dkt. Ulimboka ambayo pia yamesikika yakitamkwa na mwenyewe (Dkt. Ulimboka Steven), kupitia kituo cha redio cha CloudsFM, kwamba walikuja watu watatu waliovalia kiraia na kujitambulisha kuwa wao ni askari. Watu hao walimchukua na kumuingiza katika gari lisilokuwa na namba na kuanza kuelekea barabara ya Bagamoyo. Huko walimfunga kitambaa usoni, kamba mikononi na miguuni kisha wakampiga huku wakimwambia amekuwa akiwasumbua kwa muda mrefu na kama wangekuwa na sindano ya sumu wangemmaliza kabisa.

Dkt. Ulimboka alifikishwa katika hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa huduma. Hali yake ni mbaya ila "stable".

 Baadhi ya watu wa shirika la Tanzania Legal Human Rights Center (LHRC) walifanya juhudi za kumtafuta kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dkt. Ulimboka Steven aliyekuwa ametoweka jana usiku.

 Taarifa iliyotoka kwa mmoja wa wanaharakati hao inasema, walifanikiwa kumpata Dkt. Ulimboka katika eneo la Mwabepande, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam,  akiwa amefungwa kamba miguuni na mikononi, hajitambui  na asiyeweza kuzungumza.



Taarifa hiyo inaongeza kuwa, Dkt. Ulimboka alikuwa amepigwa vibaya sana katika sehemu mbalimbali za mwili wake na anahitaji matibabu ya haraka
  
Juhudi zinafanywa kumpatia msaada unaohitajika Dkt. Ulimboka.

 HABARI INAYOHUSIANA:

 
Read more...

Monday, June 25, 2012

BOMB ATTACK AS PEOPLE WATCHING ENGLAND VS ITALY IN MOMBASA

0 comments
An attack victim being helped at the Coast General Hospital in Mombasa

One person was killed and several others injured in a grenade attack in a bar and restaurant in Mishomoroni estate in Mombasa, Kenya on Sunday night.
The attack occurred at around 10p.m. at the so called Jericho Beer Garden in the sprawling Mombasa estate.The dead man and the injured were at the outer section of the bar dancing to the music when the explosion occurred in three successive rounds.

The inner section of the pub was full of customers who had gathered to watch the European championships football match between England and Italy.
Police in Kenya said one person died, but St John Ambulance personnel who helped with rescue efforts put the number of fatalities at three. 

Security Officers helping an attack victim
This happened one day after US Embassy issued warning of an imminent terror attack on Mombasa.

Witnesses said they heard three loud explosions followed by screams.The scene was littered with debris of broken bottles and crates of beer.Police immediately cordoned off the area marking it as a crime scene and picked the body of the young man who was killed in the explosion.

A witness Mr Emmanuel Omondi said he was in the pub and had escorted a friend who was leaving and had just walked a few steps away when he heard the explosions.
“At first I thought it was the transformer which had blown up because it has been having problems. But immediately thereafter I heard a second blast and then a third one,” he narrated.

He said the man who died in the explosions was one of those who were on the dance floor.
He and other customers who escaped unhurt helped carry some of the injured to `matatus`(local passenger buses) that rushed them to hospital before the St John Ambulance team arrived.

Security Officers arrive at the scene
Provincial Police boss Aggrey Adoli arrived at the scene with a team from the Anti-Terrorism, Police and Criminal Investigations Department officers and helped seal off the area.

A nine year old boy was among the people injured. , some with serious injuries.
Mr Adoli could not confirm whether it was a terrorist attack and said police could not link it to the American alert since it targeted locals and not American citizens.
He told Coast province residents not to panic saying the security situation was not alarming and was still in control.
 According to reports this morning, Anti -Terror Police officers have one suspect in custody connected to last night attack.  Coast PPO Aggrey Adoli said preliminary investigations indicate that they were three explosions at the scene and heavy gun shots.
Some of attack victims at Coast General Hospital in Mombasa
  

 At least 28 victims of the attack were taken to the Coast Provincial General Hospital with one person admitted in the ICU. Nurse incharge, Stella Ndivo says five were treated and discharged while others still admitted sustained bullet and soft tissue injuries, among them a 9 year old boy.
 Last week,Kenyan police arrested two Iranians after they seized chemicals they suspected were going to be used to make explosives in Mombasa.
 Police arrested the Iranians on Wednesday of last week in Nairobi. On the same day, police impounded a container in Mombasa originating from Iraq and suspected to be carrying explosives.


On the following day, police flew one of the suspects to Mombasa, where he led police to recover 15 kg of powder, which security experts took to their laboratory for testing.

YOU MAY RELATE TO THIS:
Read more...

Sunday, June 24, 2012

NAIBU WAZIRI AIBUKA NA KUKANUSHA KUFUMANIWA

0 comments
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mh. George Simbachawene(Mb)
Jana ziliibuka na kuenea habari za Naibu Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene kuwa alifumaniwa na mke wa askri huko Singida katika hoteli maarufu mjini humo ya Aqua.

NAIBU Waziri  ameibuka na kukanusha vikali uvumi mbele ya waandishi wa habari mjini Karatu jana jioni, Simbachawene ambaye pia ni Mbunge Kibakwe (CCM) mkoani Dodoma, alisema habari hizo ni uongo na kudai kuwa zimeenezwa na baadhi ya wabunge wa Chadema aliokutana nao mjini Singida jana wakati akiwa njiani kwenda msibani Karatu.

Alisema kuwa katika hoteli aliyofikia, kuna mtu alifumaniwa akiwa na mke wa askari na kufafanua kuwa watu walizua jambo hilo kwa kuwa naye alilala katika hoteli hiyo.

“ ...ukweli ni kwamba jambo hilo halijanitokea. Mimi nilifika hapa jana (juzi) nikitokea Dodoma kuelekea Karatu kuhudhuria msiba wa shemeji yangu,” alisema Simbachawene.

Aliwataja watu wanaodaiwa kueneza uvumi huo hizo kuwa ni wanachama wanane wa Chadema akiwemo Mbunge wa Viti Maalumu kupitia chama hicho, Christina Lissu.

“Baada ya kufika Singida nilikwenda katika baa moja na kuwakuta wabunge wa Chadema na baadhi ya wanachama, nilipata kinywaji na kurudi hotelini kulala,” alisema Simbachawene.

Huku akivua shati kuwaonesha waandishi wa habari kwamba hakukatwa mapanga mikononi kama ilivyodaiwa, alisema kuwa alipoamka asubuhi ndipo alianza kusikia habari kuwa amefumaniwa na mke wa mtu.

Awali taarifa kutoka Singida zilizowekwa pia kwenye mitandao ya kijamii zilidai kuwa Naibu Waziri huyo alikumbwa na mkasa huo jana alfajiri.

Tukio hilo ambalo inaelezwa kuwa lilitoka majira ya saa kumi, baada ya taarifa hizo kumfikia mwenye mke, ilimlazimu mmiliki wa hoteli hiyo kutoa taarifa Polisi ili kuzuia maafa zaidi

Katika uvumi wa jana ilidaiwa kuwa baada ya taarifa hizo, iliwalazimu askari Polisi kwenda katika hoteli hiyo ili kumuokoa Simbachawene, ambaye tayari alikuwa amejeruhiwa mkono kwa sime na askari huyo mwenye mke.

Mara baada ya purukushani hizo katika eneo hilo, Naibu Waziri huyo alidaiwa kwenda kutoa taarifa katika kituo cha Polisi mkoani Singida, ambapo ilidaiwa kuwa katika maelezo yake aliandika jina la Josephat Joseph badala ya kutumia jina lake halisi.

Hata hivyo, Mbunge Christina Lissu, alisema anashangazwa na taarifa za yeye kuhusishwa kueneza uvumi huo.

Alisema walikutana na Naibu Waziri huyo, katika hoteli hiyo, wakiwa wanatoka mkoani Tabora katika kesi na wabunge wa Chadema, Conchesta Rwamlaza, Philipa Muturano na John Mrema ambaye ni Mkurugenze wa Bunge na Halmashauri ya chama hicho.

“ Tulipofika Singida nilimwona Simbachawene nilimwita jina, alitufuata na kutununulia vinywaji hapo hotelini,” alisema Lissu na kuongeza;

“Hata tulipofika hoteli, baada ya muda tukasikia kutoka kwa mmiliki wa hoteli akisema kuna watu wanataka kumharibia biashara. Tulipomuuliza kulikoni? Akasema kwani hamna habari si mmewaona Polisi wakati mnaingia hapa, huku akisema kuna kigogo wa Serikali amefumaniwa na mke wa askari.”

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Linus Sinzumw alipoulizw alisema, hakuna tukio kama hilo lililotokea mjini Singida wala mahali popote katika mkoa huo.
“Huo ni uzushi tu, hakuna tukio hilo mjini Singida na wala sijasikia taarifa zozote za aina hiyo kutoka maeneo mengine mkoani hapa, alisema Sinzumwa.

UNAWEZA KUCHUNGULIA NA HII 
Read more...

Saturday, June 23, 2012

BREAKING NEWS:NAIBU WAZIRI AFUMANIWA NA MKE WA MTU LEO

0 comments
Kuna habari kutoka Singida zinasema NAIBU WAZIRI.. (JINA LIMEHIFADHIWA) amefumaniwa akiwa na mke wa mtu (mke wa askari mmoja) pale Singida katika Hotel ya Aqua. 
 
.Kwa mujibu wa Blog ya The Choice  amefumaniwa  saa 10 alfajiri. Baada ya kupata tip hiyo, maaskari walikwenda wakazingira hotel hiyo, wakati WAZIRI HUYO akitoka yule askari mwenye mke kumbe alikuwa ameficha sime/panga akamkata Mheshimiwa Naibu Waziri.


Habari zinasema alikuwa yuko njiani kwenda msibani ukweni kwake, Karatu. Hata wakati wa kupiga kura jana jioni hakuwepo bungeni, akiaga kuwa anawahi msibani.
Habari zaidi zitawajia kadri nitakavyozinasa
Read more...

Friday, June 22, 2012

MNYIKA AELEZA SABABU YA KUOMBA MUONGOZO SAKATA LA MADAKTARI BUNGENI LEO

0 comments

Lengo la Kuomba Mwongozo - Sakata la Madaktari

Kwanini niliomba muongozo-Sakata la Mgomo wa Madaktari

Leo nilitaka kuomba muongozo wa Spika kwa mujibu wa Kanuni 49 (2) baada ya Waziri wa Afya kutoa kauli juu ya utekelezaji wa madai ya madaktari. Kanuni hiyo inataka kauli isiwe ya kuzua mjadala lakini aliyoyaeleza waziri juu ya uboreshaji wa maslahi ya madaktari yanazua mjadala kwa kuwa yanatofautiana na majibu ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyoyatoa bungeni jana, (Juni 21, 2012) na pia hayana uhalisi. Mathalani, wakati serikali ikidai imeongeza posho ya kuitwa kazini (on call allowance) toka Februari, 2012 na kutumia bilioni 7.9 kwa miezi michache, imetenga kwa watumishi wa Afya bilioni 18.9 tu kwa mwaka mzima wa 2012/2013 kiwango ambacho hakitoshi.


Hivyo nilitaka kuomba muongozo Spika awezeshe kauli hiyo ijadiliwe kama ilivyokuwa kwa kauli juu ya fedha za rada. Nakusudia kumuandikia barua Spika kushauri aelekeze kamati ya bunge ya huduma za jamii kauli hiyo ya waziri.


Pia bunge halipaswi kunyimwa fursa ya kutumia mamlaka yake kwa mujibu wa ibara ya 63 ya kuishauri na kuisimamia serikali kusuluhisha mgogoro na madaktari ili kuepusha mgomo wenye athari kwa nchi na wananchi kwa kisingizio cha kusudio la serikali kupeleka mgogoro mahakama kuu kwa kuwa mpaka leo taarifa iliyotolewa bungeni bado hakuna shauri katika kitengo cha kazi. Hivyo, Spika anapaswa kutoa jukumu kwa kamati husika ya bunge kuendelea na usuluhishi kabla ya serikali kukimbilia mahakamani.


Wabunge tupewe nakala ya taarifa ya majadiliano ya pande mbili yaliyochukua zaidi ya siku 90 badala ya kupewa hotuba ya nusu saa ya upande mmoja wa serikali pekee.


Hata serikali ikizuia mgomo wa wazi kwa zuio la kimahakama ieleweke kuwa mgomo wa chinichini kwa watumishi wa afya ambao una athari ya muda mrefu kwa maisha ya wananchi nchini.


Mwisho, serikali ipunguze matumizi yasiyo ya lazima na ipanue wigo wa mapato.


John John Mnyika.

Mbunge Jimbo la Ubungo (CHADEMA)
22 Juni, 2012
Read more...

KENYAN POLICE SEIZE INBOUND EXPLOSIVE SHIPMENTS IN MOMBASA

0 comments

Port of Mombasa in Kenya
According to Reuters, Kenyan police had arrested two Iranians after they seized chemicals they suspected were going to be used to make explosives in Mombasa, which has been hit by a series of attacks.

The port city, the capital Nairobi and other parts of Kenya have suffered a series of grenade attacks since Kenya sent troops into Somalia last year to try to crush al Shabaab insurgents it blames for a surge in violence and kidnappings threatening tourism in east Africa's biggest economy.

Police arrested the Iranians on Wednesday in Nairobi. On the same day, police impounded a container in Mombasa originating from Iraq and suspected to be carrying explosives.

On Thursday, police flew one of the suspects to Mombasa, where he led police to recover 15 kg of powder, which security experts took to their laboratory for testing.

"They are cooperating well. They are giving us key information that might help us reduce terrorist attacks in the country," Ambrose Munyasia, a senior police officer at the Coast region told Reuters.
"We want to find out whether these substances are linked to any terror groups, including al Shabaab, al Qaeda and any other group," Aggrey Adoli, Coast provincial police officer, added.

Francis Kimemia, Kenya's acting head of civil service who was in Mombasa, said the government had sought the help of international agencies such the FBI and Interpol in helping deal with security threats.
"We have been working with them in terms of identifying criminals. We cannot fight terrorism alone. You have to work with other partners and other state organs," he said.

In the most recent attack, a bomb exploded in a trading center in the heart of Nairobi in late May, wounding more than 30 people. One person later died from their injuries.
Gunmen also detonated grenades outside a nightclub in Mombasa in May, killing one person and wounding several others.

Al Shabaab seeks to impose a strict version of sharia, Islamic law. The group emerged as a force in 2006 as part of a movement that pushed U.S.-backed warlords out of Somalia's capital, Mogadishu.
At present it also has hundreds of foreign fighters in its ranks.
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797