Pages

 

Friday, August 2, 2013

NANDO ALITAKA KUJIUA

0 comments
 
Siku  chache zilizopita mwakilishi wa Tanzania kwenye shindano la Big Brother Africa 8 (The Chase) Nando alitimuliwa kutoka kwenye jumba linalowahifadhi washiriki wa shindano hilo kwakile kilichoonekana kutishia usalama wa mshiriki mwenzake Elikem,mwakilishi wa Ghana.
Habari mpya hivi sasa ni juu ya `tweet` ya mshiriki huyo juu ya jaribio lake la kutaka kujiua mwaka 2011
Hii inaonesha kuwa Nando amepitia kwenye utoto wenye misukosuko na juzi kati alikiri kuwahi kutumia tiba maalum ya kupambana na matatizo aliyokuwanayo.Labda pengine njia hizi za maisha ndio zilizojenga tabia yake ya ukorofi
Tukio hilo la kujaribu kujiua lilipelekea mwaka mmoja baadae aanzishe ukurasa wa Facebook aliouita L.O.V.E ambao ameufanya maalum kwa watu waliopitia masukosuko ya kimaisha kujadiliana.

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797