Pages

 
Showing posts with label burudani. Show all posts
Showing posts with label burudani. Show all posts

Friday, August 2, 2013

NANDO ALITAKA KUJIUA

0 comments
 
Siku  chache zilizopita mwakilishi wa Tanzania kwenye shindano la Big Brother Africa 8 (The Chase) Nando alitimuliwa kutoka kwenye jumba linalowahifadhi washiriki wa shindano hilo kwakile kilichoonekana kutishia usalama wa mshiriki mwenzake Elikem,mwakilishi wa Ghana.
Habari mpya hivi sasa ni juu ya `tweet` ya mshiriki huyo juu ya jaribio lake la kutaka kujiua mwaka 2011
Hii inaonesha kuwa Nando amepitia kwenye utoto wenye misukosuko na juzi kati alikiri kuwahi kutumia tiba maalum ya kupambana na matatizo aliyokuwanayo.Labda pengine njia hizi za maisha ndio zilizojenga tabia yake ya ukorofi
Tukio hilo la kujaribu kujiua lilipelekea mwaka mmoja baadae aanzishe ukurasa wa Facebook aliouita L.O.V.E ambao ameufanya maalum kwa watu waliopitia masukosuko ya kimaisha kujadiliana.

Read more...

Friday, July 26, 2013

HUU NI WARAKA MZITO KWA WATANZANIA KUTOKA KWA KALA JEREMIAH KUHUSU LOWASSA

0 comments
Msanii wa Hip hop Kala Jeremiah

TANGAZO KWA UMMA

MIMI KALA JEREMIAH NILIKUWA MSANII WA KWANZA TANZANIA KUMSEMA MHESHIMIWA EDWARD LOWASA KUPITIA WIMBO WANGU UITWAO WIMBO WA TAIFA BAADA YA MHESHIMIWA KUKUMBWA NA KASHFA YA UFISADI WA RICHMOND.KWA KIPINDI KILE KILA MMOJA WETU ALIHAMAKI SANA NA KUONA KWELI MZEE WA WATU NI FISADI.KWENYE WIMBO HUO KUNA MISTARI NILISEMA. mi siyo mwana siasa sisubiri tume ichunguze nistaafu ka Lowasa.

KWA KUWA MIMI NI MZURI SANA KWENYE KUFANYA UCHUNGUZI BINAFSI NILITUMIA MUDA MWINGI SANA KULICHUNGUZA SWALA HILI LA KASHFA HII NA BAADAE NILIGUNDUA KUWA NI SWALA LA KISIASA.NA YALIKUWA NI MAPITO AMBAYO MWANADAMU YOYOTE HUPEWA MUDA WA KUPITIA MAGUMU ILI KUPIMWA IMANI YAKE KWA MUNGU.

BAADA YA KUGUNDUA HAYO MWAKA JANA NILITENGENEZA WIMBO UNAOITWA AZIMIO LA ARUSHA AMBAO UPO KWENYE ALBUM YANGU YA PASAKA AMBAYO IKO SOKONI TOKEA MWAKA JANA. KATIKA WIMBO HUO WA AZIMIO LA ARUSHA NILIANDIKA MISTARI IFUATAYO. walipiga dili waka msakizia lowasa ili kuficha siri kali.NILIANDIKA MSTARI HUU BAADA YA KUFANYA UCHUNGUZI NA KUJIRIDHISHA KUWA MHESHIMIWA NI KIONGOZI BORA SANA NA HASA KWA UAMUZI WAKE WA KUJIUZULU BILA SHINIKIZO KUBWA NA WAKATI KWA NAFASI ALIYOKUWA NAYO YA UWAZIRI MKUU ALIKUWA NA UWEZO WA KUGOMA KUJIUZULU NA HASA KWA KUWA HAKUWA FISADI KAMA ILIVYOSEMWA.

MWEZI WA TATU MWISHONI MWAKA HUU NILITOA WIMBO UNAOKWENDA KWA JINA LA KARIBU DAR AMBAKO NILISEMA dar es salam ingekuwa nchi Rais angekuwa Lowasa huku watu washashtukia kuna mchezo kwenye siasa HAPA NILIKUWA NAMAANISHA KUWA WATU WENGI WANAOISHI DAR WANAWAHI KUJUA MAMBO YA WANASIASA KWA KUWA WANASIASA WANAISHI HUKU LAKINI PIA WATAFITI WENGI WA MAMBO YA KISIASA WANAISHI HUKU KWA HIYO NI RAHISI ZAIDI KUUJUA UKWELI MAPEMA.

NAAMINI KUONDOKA KWA LOWASA KWENYE UWAZIRI MKUU KUMEZOROTESHA MAENDELEO YA TAIFA KWA KIASI FLANI

NDUGU ZANGU WATANZANIA NI WAZI KUWA LOWASA NI JEMBE TENA JEMBE LA KAZI KUMBUKENI BILA LOWASA KUSINGEKUWA NA SHULE ZA KATA TANZANIA,NA ANGEENDELEA KUWEPO MADARAKANI ALIKUWA NA MPANGO WA KUANZA MCHAKATO WA ZAHANATI ZA KATA.IKUMBUKWE PIA LOWASA NDIYE ALIYESIMAMIA UJENZI WA CHUO CHA UDOM TENA KWA PESA ZA KITANZANIA BILA KUOMBAOMBA VIMIKOPO.

MRADI WA MAJI KUTOKA MWANZA KWENDA SHINYANGA NI KAZI YA LOWASA. ZIPO KAZI NYINGI AMBAZO NIKIZITAJA ZOTE NAWEZA KUJAZA UKURASA.NACHOJARIBU KUSEMA HAPA NI KWA KUWA MIMI NI MSANII NA NI KIOO CHA JAMII NINGEOMBA WEWE MWANAJAMII CHUKUA HATUA YA KUFANYA UCHUNGUZI BINAFSI KUHUSU LOWASA.BILA KUFUATA MKUMBO WA KISIASA NAAMINI UTAKUBALIANA NA MIMI KUWA LOWASA NI JEMBE.

MIMI HUWA NAPENDA KUSOMA VITABU VYA WANAHARAKATI NA KUNA KITABU KIMOJA NILIKIPITIA CHA MWANAHARAKATI KUTOKA ITALY AITWAE NICCOLO MACHIAVELLI AMBAYE ALIZALIWA MWAKA 1469 NA KUFARIKI 1527. KATIKA ENZI ZA UHAI WAKE ALIWAHI KUANDIKA VITABU KADHAA LAKINI KATI YA VITABU HIVYO KITABU KIITWACHO THE PRINCE NDICHO KILIMPA HESHIMA KUBWA SANA KWA KUWA ALIIKOSOA SERIKALI YA KIFALME YA KIPINDI HICHO KITU AMBACHO HAKIKUWA RAHISI KWA MTU KUFANYA HASA IKIKUMBUKWA KUWA ENZI ZA UFALME ZILIKUWA ENZI ZA UBABE. KATIKA MANENO KUTOKA KWENYE KITABU HICHO AMBAYO NINGE PENDA KUKUSHIRIKISHA WEWE NDUGU YANGU MTANZANIA NI MANENO YAFUATAYO MACHIAVELLI ALIANDIKA HIVI. kuna kipindi ambacho mataifa yanapita katika vipindi vigumu. na kwa kipindi hicho kigumu mataifa hayo yatahitaji sana kupata kiongozi mwenye kuweza kuchukua maamuzi magumu,na ambaye hatakuwa chini ya sauti ya mtu mwingine, na ambaye ataweza kuyatekeleza maamuzi magumu kwa haraka hata kama ni kwa kuwaumiza wachache ili wengi wawe huru.atakayekuwa tayari kutekeleza jambo baya ili likapita na kusahaulika na atakayetekeleza mambo mazuri kwa muda mrefu na yakaendlea kukumbukwa.kiongozi huyo atatakiwa kuchagua kuogopwa ama kupendwa lakini ni bora akachagua kuogopwa lakini akitenda haki kwa wananchi husika.HAYO NI BAADHI YA MANENO ALIYOANDIKA MACHIAVELLI KWENYE THE PRINCE KITABU AMBACHO KILIMPELEKEA KUITWA NA MFALME NA KUPEWA NAFASI YA JUU YA UONGOZI KATIKA SERIKALI HIYO YA KIFALME.

KWA MAONI YANGU NADHANI TAIFA LETU LIMEPITIA VIPINDI VIGUMU KADHAA NA KWA MANENO YA BWANA MACHIAVELLI NADHANI KIONGOZI ANAYEFAA AMBAYE ANAWEZA AKACHUKUA MAAMUZI MAGUMU NA AMBAYE HAWEZI KUWA CHINI YA SAUTI YA MTU MWINGINE NI MHESHIMIWA EDWARD NGOYAI LOWASA.

tafakari chukua hatua
Read more...

Sunday, July 21, 2013

SHILOLE AFANYA MAHOJIANO NA `TAKE ONE` NYUMBANI KWA DIAMOND

1 comments
Mtangazaji wa Clouds Tv, Zamaradi Mketema, alikuwa nyumbani kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongoflava)Nasib Abdul (Diamond Platinumz) ambako msanii huyo alikuwa akifuturisha.Bi Mketema alipata wasaa wa kumhoji msanii mwingine katika tasnia hiyo ya muziki Zuwena Mohamed`Shilole`.Mahhojiano hayo yalikuwa mahsusi kwa kipindi cha TAKE ONE cha Clouds Tv kinachoendeshwa na Bi Mketema.Watu hao wawili walikuwa ni sehemu ya watu kadhaa walioalikwa kwa ajili ya kufuturu nyumbani kwa Diamond.
 Katika mahojiano hayo ambayo yanatarajiwa kurushwa hewani na Clouds Tv siku ya Jumanne hii saa 3.30 usiku,Shilole amelezea faida alizopata kama msanii katika safari yake nchini Marekani,na pia matarajio yake baada ya safari hiyo,ikiwamo ya kufanya kazi na msanii mmoja mkubwa wa nchi hiyo.
 

Read more...

Wednesday, July 17, 2013

BREAKING NEWS:LUKUMAY WA KLABU MASAI AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI

0 comments
LUKUMAY  (kulia)enzi za uhai wake
Habari nilizozipata muda mchache uliopita ambazo zimethibitishwa na ndugu na jamaa wa karibu zinasema Benedict Charles Lukumay amefariki kwa ajali ya gari eneo la Mikumi mkoani Morogoro usiku huu.
 
Chanzo cha kifo chake kimeelezwa kuwa ni ajali ya gari iliyotokea eneo la Mikumi mkoani Morogoro majira ya saa mbili usiku. Meneja mkuu wa Meridian Hotel LTD Mzee Mponda amethibitisha juu ya kifo hicho, huku huku akisema kuwa ilitokana na ajali ya gari.

 "Wakiwa na mwenzake aliyefahamika kwa jina la Adrian na gari binafsi wakielekea mkoani Iringa gari aliyokuwamo marehemu iligonga nyuma ya roli lililokuwa limesimama njiani." alisema Mzee Mponda.

 Adrian ambaye ndiye aliyekuwa anaendesha gari alinusurika kwenye ajali hiyo.

 Benedict alikuwa ni mmoja kati ya Wakurugenzi watendaji wa kampuni ya Meridian Hotel LTD inayomiliki na kuendesha kumbi za burudani zikiwemo Masai Kinondoni, Masai Ilala na Masai Galapo Ilala.
Kifo chake kimeacha pengo kubwa si tu kwa familia bali hata wapenda burudani, akifahamika kimchango katika kusimamia na kuendeleza burudani na yakiwemo maonyesho mbalimbali ya wanamuziki wa bongo fleva na fani nyinginezo.

Mungu alaze Pema ROHO ya Marehemu Ben..
Read more...

PHOTOS:LADY JAY DEE`S MAKE-UP SESSION DURING THE VIDEO SHOOTING OF HER SINGLE HIT `YAHAYA`

0 comments

Read more...

Saturday, July 13, 2013

SIRI NJE:MTANZANIA AAMBUKIZWA GONJWA LA ZINAA BBA!!

0 comments
Kwa sauti ya kunong`ona,mshiriki wa kiume kutoka Tanzania katika shindano la Big Brother Africa mwaka huu,Nando,amelalamika kuwa ameambukizwa ugonjwa wa zinaa uitwao Clamydia na mshiriki mwenzie wa kike kutoka Ghana aitwae Selly.

Kwa siku kadhaa sasa,Nando na Selly wamekuwa mbalimbali,jambo ambalo washiriki wenzao pamoja na watu wanaofuatilia shindano hilo wameshindwa kujua kwanini.

Nando alifichua siri hiyo ya kuambukizwa clamydia,gonjwa linaloambukizwa kupitia zinaa,lakini  hakuna mtu mwenye uhakika iwapo Nando anasema ukweli,Hata hivyo angalau kauli ya Nando imeweza kutegua kitendawili cha kwanini washiriki hao hawapatani tena siku hizi,tofauti na ilivyokuwa awali.

Katika siku chache zilizopita Nando amekuwa hajisikii vizuri na muda mwingi amekuwa akiutumia kupumzika kitandani,na hakuna aliyekuwa anajua alikuwa akisumbuliwa na nini.

Iwapo ni kweli Nando ameambukizwa gonjwa hilo,hakuna anaeweza kusema moja kwa moja kuwa Selly ndie aliemwambukiza Nando au Nando alikuwa na gonjwa hilo tangu mwanzo na pia tusipuuze uwezekano wa Nando kuwa anasumbuliwa na tatizo jingine,lakini kwa jinsi mtiriko wa mambo ulivyo,Nando amekuwa hajisiki vizuri na amekuwa akionana na daktari mara kadhaa.Zaidi ya hayo Selly amemdokezea mshiriki mwingine kutoka Botswana, O`neal,kuwa Big Brother amemshauri kutumia kinga anapokuwa mzigoni.Jambo ambalo linaashiria madai ya Nando kuwa na ukweli kiasi fulani

Nando tangu hapo amekuwa akimbughudhi Selly na ilifikia pabaya pale Nando alipokuwa akimdhihaki Selly aliposhindwa kwenye moja ya mashindano ndani ya jumba hilo,hali iliyopelekea Selly kuondoka huku akilia,na kuwaomba washiriki wenzie wam`nominate` ili atoke arudi nyumbani.

Wakati wa mahusiano yao Nando na Selly walikuwa kwenye mahaba mazito na haikuchukua hata siku kabla hawajavunja moja kati ya amri kumi za mwenyezi mungu.Lakini Nando aliwahi kumueleza Selly kuwa yeye hayuko `serious` kwenye mahusiano yao ila anataka kujifurahisha tu.

Read more...

Thursday, July 11, 2013

BAADA YA DIAMOND KUTOA SIRI, UWOYA ALIA NA DUNIA

0 comments


Kufuatia jana kuripotiwa habari iliyopewa kichwa cha habari  "DIAMOND AFICHUA KISA CHA KULALA NA UWOYA!"  inayomhusu mwanadada Irene uwoya na Msanii wa kizazi kipya Diamond platnumz  na gazeti la Global publishers, hatimaye Irene Uwoya alichukua dakika kadhaa kuandika hichi alichokiandika hapa chini:
“Kuna saa najiuliza kwanin ukimwamin mtu ndio anageuka...kwanin ukiwa muwaz watu wanakuchukulia vbaya? Leo nimeumia sanaaa kuliko skuzote...sijaamini mtu niliye mwamini kumuona kama rafiki yangu anaweza kuongea shit kuhusu mim...au najiuliza siruhusiwi kuwa na rafik wa kiume? Lakin sa nyingine nakaa chin nasema God ...u know me better”
Read more...

MAMA WA PROFESA J AFARIKI KWA AJALI,MWENYEWE AELEZEA.

0 comments
Profesa J akiwa aktika picha ya pamoja na wazazi wake siku  za nyuma
Mama mzazi wa mwanahip-hop nguli nchini Joseph Haule anaekwenda na jina la kisanii la Profesa J amefariki dunia baada ya kugongwa na gari huko Mbezi Juu nje kidogo ya jiji la Dar Es Salaam alikokuwa akiishi na mwanae


Taarifa zinasema kuwa Marehemu Bi Rosemary Majanjara Haule alipatwa na ajali hiyo alipokuwa akikatiza barabara kuelekea dukani majira ya saa mbili usiku na kuwa baada ya  kugongwa wasamaria wema walimsaidia kwa kumkimbiza Hospitali ya Tumbi Kibaha kwa kutumia usafiri wa Bajaj,ambako muda mfupi baadae alifariki dunia.Bado haijajulikana aina ya gari iliyomgonga.

 Vyanzo mbalimabli vya habari vimesema Profesa J mwenyewe amethibitisha kutokea kwa msiba huo na kuwa bado inamuwia vigumu kuamini kilichomtokea mama yake kwa kuwa muda mfupi baada ya kupatwa na ajali aliwasiliana nae kwa njia ya simu kumjulisha kuwa amepata ajali na yuko kituo cha Polisi (ilikupatiwa PF3 ambayo ingemuwezesha kutibiwa Hospitali) 
"Mama aliniambia mwanangu nimegongwa na gari njoo niko Polisi naandikisha...mwanangu nakufa..aliniambia mama na mara simu ikakatika.Kila nilipojaribu kupiga ikawa haipatikani."Alisema Profesa J kwa uchungu.
Profesa J alisema kuwa wakati anapigiwa simu na mamayake alikuwa katika mkahawa wa Nyumbani Lounge,maeneo ya Namanga,jijini Dar Es Salaam,amabko alikuwa na kikao na msanii mwenzie Lady Jay Dee na mumewe Gadna Habash ambao baada ya kuwafahamisha kilichotokea walimsindikiza hadi Hospitali ya Tumbi Kibaha.
"Tulipofika Hospitalini Tumbi sikuamini nilichokikuta,nilijua mama amelazwa,badala ya kupelekwa wodini nilipilekwa kwenye chumba cha maiti na kumkuta mama ameshafariki" Alisema Profesa J kwa majonzi
Said Nuhu Blog inatoa pole sana kwa Profesa J kwa kufikwa na mtihani huu.Mola Amlaze Pema Mama Rosemary Haule.Msiba upo nyumbani kwa Profesa J Mbezi Mwisho






Nyumbani kwa Profesa J








Read more...

Wednesday, July 10, 2013

BI HARUSI HUYU KAFARIKI DUNIA MUDA MFUPI KABLA YA KUFUNGA NDOA

0 comments
Hapa alikuwa akilishwa chakula na Bwana Harusi Mtarajiwa aliyetajwa kuwa ni Kasisi Masawe wakati wa tafrija ya kuagana na familia maarufu kama SEND-OFF
 Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Bibi Harusi ambaye ni mkazi wa Chanika mjini Handeni, Levina Mmasi (23) amefariki dunia saa moja kabla ya ndoa yake kufungwa katika Kanisa la Katoliki la Roma Wilaya Handeni Jumamosi na hivyo kuilazimu kamati ya maandalizi ya harusi kujigeuza na kuwa ya msiba.
Kifo hicho kilichotokea Jumamosi mwishoni mwa wiki iliyopita, kimekuwa gumzo mjini Handeni hukufamilia ya marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Firmin Mrimasha, alisema kuwa chanzo cha kifo cha Levinwananchi wakisema kuwa ni tukio ambalo halijawahi kutokea katika wilaya hiyo. Msemaji wa a ambaye alijifungua mwanzoni mwa wiki iliyopita,ilikuwa ni homa aliyoipata ghafla siku ya Alhamisi na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni na kukutwa na malaria na kisha kulazwa kwa matibu.

 “Huyu bibi harusi alikuwa ametoka kujifungua, alikuwa na mtoto wa kiume kutokana na ujauzito wa miezi saba, ndipo ghafla Alhamisi akapata homa tukampeleka hospitali alikolazwa na baada ya kupata nafuu, aliruhusiwa Ijumaa.

“Baada ya kuruhusiwa akaanza maandalizi ya harusi na Jumamosi ambayo ndiyo siku ya ndoa yake, alijiandaa lakini ilipofika saa 8.05 akafariki dunia akiwa nyumbani akisubiriwa kwenda kanisani kufunga ndoa ambayo ilikuwa ifungwe saa 9.00,” alisema Mrimasha.

Alisema, “Inasikitisha sana ila imeshatokea yaani marehemu amefariki saa moja kabla ya ndoa yake na baada ya kifo hicho, mtoto wake naye alifariki muda mfupi baada ya mama yake kufariki dunia,” alisema Mrimasha.

Akizungumzia mkasa huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Harusi hiyo iliyogharimu Sh7.7 milioni, Abdi Kipacha alisema kuwa kwake ni tukio la kwanza kutokea tangu kuzaliwa kwake na kamwe hawezi kulisahau.

“Nilishazipangia kazi kamati za maandalizi, lakini ghafla tukapewa taarifa kuwa bibi harusi amefariki...Hatukuamini, ikabidi niwatangazie wanakamati wenzangu kuwa hakuna tena shughuli, bibi harusi amefariki,” alisema mwenyekiti huyo wa kamati na kuongeza:

“Kitu tulichokuwa tukisubiri ni kuambiwa bibi harusi angefika saa ngapi, lakini ghafla tukapewa taarifa za kifo, ilikuwa ni vigumu kuamini lakini ni kweli imetokea na inasikitisha kwani si jambo la kawaida,” alisema Kipacha.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na wanandugu ni kuwa marehemu alikuwa Mwalimu wa Shule ya Msingi Nndawa mkoani Lindi na kwamba alikuwa katika kundi la walimu wa ajira mpya ambayo hadi mauti yanamkuta alikuwa hajapokea hata mshahara wake wa awali.

Akizungumzia hali hiyo, Padri aliyekuwa afungishe ndoa hiyo, Max Sabuni wa kanisa hilo Katoliki Handeni alisema:       “Nimesikitishwa na tukio hili kwa kuwa halikuwahi kunitokea...Kilichobaki ni wanandugu kuwa watulivu kwa kuwa Mungu amechukua kiumbe wake kwa muda alioupanga.”

Aliwataka ndugu, jamaa na marafiki kuwa na subira katika kipindi hiki cha majonzi
Read more...

TUHUMA ZA KUAIBISHA ZAMUANDAMA ODAMA

0 comments
Mtandao wa bongo movies umetumiwa madai, kumhusu mwanadada muigizaji wa Filamu aliyepata tuzo hivi karibuni, Jennifer Kyaka anakwenda na jina la kisanii la Odama kuhusu safari zake za kwenda nje ya nchi.
Habari au tuhuma hizi , zinasema kuwa mwanadada huyo huwa haendi nje ya nchi kama anavyowaambia washabiki wake kupitia blog yake ya odama1.blogspot.com kuwa anasafiri kwenda nje kikazi zaidi, na badala yake imesemwa kuwa huwa anabaki hapa hapa nchini akijifanya yupo nje ya nchi,akiwa na lengo la kulazimisha umaarufu

Mdau aliyepeleka tuhuma hizo amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha wa picha mbalimbali toka kwenye mtandao mmoja wa kijamii ambao staa huyo  anautumia kudanganya ,zikimuonesha akiwa maeneo mbalimbali ya “duniani huko” ambayo kwa kuangalia picha hizo anasema kuwa ni feki na zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia tu ya kuhariri picha maarufu kama PHOTOSHOPMtandao wa Bongo Movies umewaomba wadau wenye majibu na utaalamu wa picha wasaidie kwa kutazama picha hizi ili kuthibitisha kama tuhuma hii ina ukweli wowote.

Read more...

Tuesday, July 9, 2013

PICHA ZILIZONIFIKIA ZA MSANII WAKAZI AKIREKODI VIDEO YA SINGO YAKE `TOUCH` HUKO `SAUZI`

0 comments
Wakazi akirekodi video ya singo yake inayokwenda kwa jina la `Touch` huko Afrika ya Kusini

Read more...

LAURYN HILL AFUNGWA JELA

0 comments
Aliekuwa mwanamuziki mashuhuri wa nchini Marekani na duniani ambae pia aliwahi kubeba tuzo ya Grammy,Lauryn Hill, ameanza kutumikia adhabu yake ya kukaa jela miezi mitatu kwa kosa la kukwepa kulipa kodi
Hill anaanza kutumikia adhabu hiyo kwenye gereza la Danbury katika jimbo la Connecticutt huko kwao nchini Marekani


Wafungwa kwenye gereza hilo ambalo ulinzi wake si mkali,wanaishi katika vyumba vilivyokuwa  katika mabweni na wajibu wao ni kufanya kazi mbalimbali

Hill ambae alianza fani yake na kundi la Fugees akiwa bado msichana mdogo katika miaka ya 1990 kabla ya kutoa albam yake ya Miseducation of Lauryn Hill  mwaka 1998,alikubali kosa lake mwaka jana,la kutokulipa kodi katika kiasi cha dola milioni 1.7 alizoingiza kuanzia 2005 hadi 2007

Pia imejumuishwa kodi aliyoikwepa mwaka 2008-2009.Mwanasheria wake aliiomba mahakama isimfunge,ila awekwe chini ya uangalizi kwa vile Hill amekuwa kitoa sana misaada kwa jamii,hali ya familia yake ambayo imekuwa kubwa na pia kutokana na ukweli kuwa deni alilodaiwa ameshalilipa

Wakati akisomewa hukumu mwezi Mei Hill aliezea jinsi alivyoshindwa kulipa kodi alipoamua kuachana na mambo ya muziki ili kujiweka mbali na matatizo ambayo yangeweza kumtokea,yeye na watoto wake.Ana watoto sita sasa.

Alielezea kuwa mabo aliyokuwa akitendewa alipokuwa katika fani ya muziki ndio yaliyomsukuma kuachana na biashara hiyo

Naibu mwanasheria mkuu wa Marekani Bi Sandra Moser aliutambua na kkuelezea kipaji cha ubunifu alichokuwa nacho Hill na moyo wake wa kuwakumbuka watoto masikini ,lakini akasema sababu alizotoa Lauryn Hill ni visingizio tu vilivyojengwa na na hisia zake na wala haviwezi kumfanya akwepe kuwajibika

Akitoka kifungoni  atatakiwa awe chini ya uangalizi kwa muda wa mwaka mzima na  atakuwa kwenye kifungo cha nyumbani katika miezi mitatu ya kwanza
Read more...

AGNES MASOGANGE ANASWA NA MADAWA YA KULEVYA `SAUZI`

0 comments
HATIMAYE  wale Wanawake wawili walionaswa  na  madawa ya  kulevya  Afrika  kusini wametambuliwa kuwa  ni  mabinti  wa  KITANZANIA ..


Mabinti  hao  wanaodaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevya zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania.

Akizungumza na mwandishi wetu  jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.

Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Jerald (MASOGANGE)  ambaye alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24. Wawili hao bado wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.

Alisema Jeshi la Polisi Nchini kwa upande wake linaendelea kufanya uchunguzi kubaini kama dawa hizo walitoka nazo wapi na pia linawasaka watu ambao watakuwa ndiyo wamiliki wa dawa hizo.

Jumapili iliyopita mtandao huu  ulipata taarifa za kukamatwa kwa dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani hiyo nchini Afrika Kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania.

Taarifa hizo zilionyesha kuwa wanawake wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oriver Tambo uliopo eneo la Kempton Park siku ya Ijumaa wiki iliyopita wakitokea Tanzania.

Wanawake hao walikamatwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini wakiwa na masanduku sita ambayo yalipokaguliwa yalikutwa na takribani kilo 150 za dawa hizo ambazo pia zinajulikana kama ‘Tik’ zikiwa na thamani ya bei ya mtaani ya Randi milioni 42 sawa na Sh. bilioni 6.8.

Baada ya kukamatwa na dawa hizo wanawake hao walikabidhiwa polisi. Tukio hilo linatoka takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Juni 28, mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulenya hivi sasa ni janga la kitaifa nchini.

Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.

Pia alisema katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.

Pinda alisema mwaka huu pekee kumekuwa na ukamataji mkubwa wa dawa za kulevya katika eneo la kimataifa la Bahari ya Hindi karibu na Tanzania.
 


Alisema hivi sasa mikate, maandazi na askrimu zinazouzwa kwenye shule za msingi, zinawekwa dawa za kulevya.

Alisema vitendo hivyo vinafanya vijana wengi wa shule za msingi na hata sekondari kuwa na tabia za ajabu, ikiwamo kuingia darasani wakiwa na kiatu kimoja mguuni, mkufu wenye nyembe na kidani chenye nyembe kifuani.


CHANZO: LEWIS MBONDE
Read more...

Sunday, July 7, 2013

BEYONCE APATA MAMA WA KAMBO

0 comments
Wanamuziki Beyonce na Solange ambao ni mtu na dada wamepata mama wa kambo baada ya baba yao kufunga ndoa na mwanamke mwingine,kufuatia kuachana na mama yao mzazi akina Beyonce
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AP, Mathew Knowles,baba wa akina Beyonce,ambae pia alikuwa meneja wa Beyonce alifunga ndoa na rafiki yake wa kike,mwanamitindo Gena Charmaine Avery huko Houston Texas,mwishoni mwa wiki iliyopita.Mathew Knowles mwenye umri wa miaka 61 na Gena Avery mwenye umri wa miaka 48,walikuwa wameshachumbiana mwaka mmoja na nusu uliopita.Beyonce na Solange hawakuhudhuria harusi.
Mathew Knowles alitalakiana rasmi na mama mzazi wa akina Beyonce,Tina Knowles,mwaka 2011 baada ya mama huyo kufungua kesi ya kudai talaka mwaka 2009.Ndoa yao ilidumu kwa miaka 29.
Read more...

AIBU!!DIAMOND PLATINUMZ AMUUMBUA DIAMOND FEKI WA KWENYE FACEBOOK !

0 comments
Katika hali ya kuchoshwa na tabia za watu wanaotumia majina ya wasanii na watu maarufu kujipatia wafuasi kwenye akaunti zao za Facebook  au Twitter msanii Naseeb Abdul ambae kisanii anatumia jina la Diamond Platinumz ameibuka na shutuma nzito dhidi ya watu wenye tabia hio na kufikia hatua kumuibua DIAMOND PLATINUMZ feki ambaye kwenye akaunti yake ya Facebook anatumia jina la Diamond Platinumz Swaqq

Muda mfupi baada ya ujumbe wa Diamond Platinumz kuwa hewani Diamond feki aliweka hadharani mambo kwa `washabiki` wake kwa kuweka picha ambayo nayo inatia wasiwasi iwapo haendelei kuwadanganya



Na matusi hayakuishia hapo,Diamond feki bado anaendelea kupokea Comment za kumlaani
Read more...

Friday, June 22, 2012

KWAMBA LULU NI MKUBWA MAWAKILI WA SERIKALI WAWASILISHA VIELELEZO MAHAKAMA KUU

0 comments
Lulu alipofikishwa mahakama kuu Juni 11 mwaka huu
MAWAKILI wa Serikali jana waliwasilisha vielelezo Mahakama kuu kupinga maelezo ya upande wa utetezi kuwa umri wa msanii wa kike wa filamu  Tanzania Elizabeth Michael ni mdogo

Habari zinasema kuwa vielelezo hivyo vya Jamhuri ni Mkanda wa video aina ya CD, yenye mahohjiano kati ya mshtakiwa huyo na mtangazaji mmoja nchini. Vingine ni maelezo ya mshtakiwa huyo aliyoyatoa polisi wakati alipohojiwa kuhusu tuhuma zinazomkabili, maombi ya hati ya kusafiria (Passport) na maombi ya leseni ya udereva.

 Awali vielelezo hivyo walitakiwa kuviwasilishwa juzi, lakini ilishindikana na badala yake vikawasilishwa jana na kesi itaendelea kusikilizwa Jumatatu ijayo, Juni 25.

Msanii Elizabeth Michael ambae hujulikana zaidi kwa jina la Lulu anakabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akituhumiwa kumuua msanii mwenzake, Marehemu Steven Kanumba aliyefariki dunia nyumbani kwake Sinza, April 7, 2012.

Hata hivyo katika hatua za awali za kesi hiyo, umri wake ulizua utata baada ya mawakili wanaomtetea Lulu kudai kuwa bado ni mtoto kwa kuwa ana umri wa miaka 17 na si 18 kama hati ya mashtaka inavyoonesha.

Hivyo mawakili hao walilazimika kuwasilisha maombi mahakamani kuiomba mahakama iruhusu ufanyike uchunguzi wa umri sahihi wa mshtakiwa huyo na ikiridhika kuwa ni mtoto basi kesi yake iendeshwe kwa misingi ya kesi za watoto kisheria ili kulinda maslahi yake.

 Juni 11, 2012 Mahakama Kuu ilikubali  kufanya uchunguzi huo yenyewe kwa lengo la kubaini usahihi wa umri wa mshtakiwa huyo na ikaziagiza na kuzipangia tarehe pande zote katika kesi hiyo kuwasilisha mahakamani hapo vielelezo watakavyovitumia katika hoja zao.

 Jopo la mawakili wanaomtetea Lulu likiongozwa na Kennedy Fungamtama Juni 13 waliwasilisha mahakamani hati za viapo vya wazazi wake na vielelezo vingine kikiwemo cheti cha kuzaliwa na cha ubatizo vinavyoonesha kuwa bado ni mtoto.

 Lakini taarifa zilizopatikana mahakamani hapo zinaeleza kuwa vielelezo vilivyowasilishwa na Jamhuri vinaonesha kuwa mshtakiwa huyo ni mtu mzima kwa kuwa kwa mujibu wa vielezo hivyo ana umri zaidi ya miaka 18.

Viapo vya wazazi wa mshtakiwa huyo vilivyowasilishwa mahakamani hapo na Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Peter Kibatala ambaye ni mmoja wa mawakili wanaomtetea Lulu vinaeleza kuwa mshtakiwa huyo ana umri wa miaka 17.

Viapo hivyo ni kiapo cha mama yake Lulu Lucresia Augustin Kalugila, mkazi wa  Dar eS Salaam na kiapo cha baba mzazi Michael Kimemeta, mkazi wa Moshi.

Viapo  vyote vinaeleza kuwa mshtakiwa huyo alizaliwa April 16, 1995  katika kituo cha Afya Muhimbili na kupewa cheti cha kuzaliwa namba B.0318479 cha Julai 23, 2004.
 
Pia viapo hivyo vinaeleza kuwa baada ya kuzaliwa mshtakiwa,  mama yake alimpa jina la Diana Michael Kimemeta, lakini alimpeleka mtoto huyo Moshi mkoani Kilimanjaro kwa ndugu zake, walimpa jina la Elizabeth, jina la bibi yake Elizabeth Shikana.

Viapo hivyo vinaendelea kueleza kuwa baada ya majadiliano wote, yeye mama, baba na ndugu wengine walikubaliana kuwa wamuite Diana Elizabeth Michael Kimemeta .

“ Elizabeth Michael Kimemeta alibatizwa katika Kanisa la Katoliki  Chang’ombe Septemba 28, 1997 na alichukua majina ya ubatizo Diana Elizabeth Michael Kimemeta;” inasomeka sehemu nyingine ya kiapo hicho cha mama wa mshtakiwa.

Utata wa umri wa mshtakiwa huyo uliibuka Mei 7, 2012 katika  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya wakili wake Fungamtama kudai kuwa ana miaka 17 na hivyo kuomba kesi yake isikilizwe katika mahakama ya watoto.

Hata hivyo Mahakama ya Kisutu iliyakataa maombi hayo ikisema kuwa haina mamlaka ya kuyashughulikia na kushauri maombi hayo yawasilishwe Mahamaka Kuu.

Ndipo Mei 15 wakili Kibatala aliwasilisha maombi hayo mahakama kuu wakiomba mahakama hiyo iamuru kwamba Mahakama ya Kisutu ina uwezo wa kisheria kushughulikia maombi hayo.
Katika maombi hayo namba 46 ya mwaka 2012,  pia mawakili hao waliomba Mahakama Kuu kama itaridhika kuwa mahakama ya Kisutu haina uwezo wa kufanya wala kuagiza uchunguzi huo ufanyike, basi Mahakama Kuu yenyewe ama iagize au ifanye uchunguzi huo.

Sambamba na hayo pia waliomba Mahakama Kuu iamuru mwenendo wa kesi ya msingi katika Mahakama ya Kisutu usimamishwe hadi suala la umri litakapopatiwa ufumbuzi.

Katika uamuzi wake Jaji Dk. Fauz Twaib alisema kuwa Mahakama ya Kisutu ina mamlaka ya kushughulikia maombi hayo na kwamba ilikosea kukataa kuyashughulikia.

Pia Jaji Dk. Twaib  alikubaliana na hoja za pingamizi la awali la wajibu Maombi(Jamhuri) kupitia kwa Wakili wa Serikali Shadrack Kimaro akisaidiana na Wakili Elizabeth Kaganda, walizozitoa wakati wa usikilizwaji wa maombi hayo, Mei 28,2012.

 Wakili Kimaro alidai kuwa maombi hayo yamewasilishwa mahakamani hapo kinyume cha sheria na kwamba hata vifungu vilivyotumika katika madai hayo haviipi Mahakama Kuu uwezo wa kuyashughulikia.
 
 Hata hivyo licha ya kukubali kuwa maombi hayo yaliwasilishwa mahamakani isivyo sahihi, lakini Jaji Dk. Twaib alisema bado Mahakama hiyo ina mamlaka ya kuyashughulikia.

 Chini ya kifungu cha 44 cha Sheria ya Mahakama za Hakimu Mkazi, Jaji Dk. Twaib aliuagiza upande wa mwombaji(mawakili wanaomtetea mshtakiwa), kuwasilisha mahakamani hati hizo za viapo na vielelezo vya umri wa mshtakiwa huyo juzi Jumatano.



Read more...

Thursday, June 21, 2012

WOLPER AANGUSHA KILIO AKIJITETEA KUHUSU GARI `ALILONYANG`ANYWA`

0 comments
Hivi karibuni kulikuwa na uvumi kuwa nyota wa filamu za  Bongo, Jacqueline Wolper Masawe amenyang’anywa lile gari alilokuwa akitanua nalo hivi karibuni aina ya BMW X6, lenye namba za usajili T 574 BXF na kwamba, sasa nyota huyo anatembelea gari lake la zamani Toyota Noah.Taarifa zinazsema
chanzo cha kuenea kwa tetesi hizo kilianzia kwenye mitandao ya kijamii na blog  ambapo wadau mbalimbali waliandika kuwa Wolper alinyang’anywa gari hilo na mwanaume aliyemnunulia.Wengine  wakitaja hata jina la Frank ambaye ni mtoto wa mfanyabiashara maarufu jijini Dar kuwa ndiye mmiliki wa gari hilo kwa sasa.Kwa mujibu wa mwandishi wa tabloids za Global Publishers ambae alikutana na Wolper Jumatatu ya wiki hii ,Wolper mwenyewe alikiri kusikia taarifa hizo huku akikanusha kuwa si za kweli.


“Na mimi nimesikia lakini si kweli jamani. Hivi mtu anaweza kunyang’anywa nguo yake ya ndani au shati lake? Si itakuwa kichekesho, gari ni mali yangu na hakuna mwenye uwezo wa kuja kuninyang’anya kwani nalimiliki kihalali,” alinukuliwa Wolper akisema.
Wolper alisema amelifungia gari hilo nyumbani kwake, Mbezi Beach, Dar  Es Salaam kwa sababu "lina matatizo kidogo".
Ili kujiridhishana hatimaye kuifahamisha dunia ukweli Wolper aliombwa kuongozana na waandishi  kwenda Mbezi kuliona gari hilo kama lipo kweli auikbidi alifuate na kulifikisha ofisi za Global Publishers.
: “Nisikuongopee kuwa naweza kuja nalo hapo ofisini wakati tatizo lake nalifahamu mimi, nakuja kuwachukua twendeni nyumbani mkalione.” Ndio jibu alilolitoa Wolper baada ya kutakiwa kulileta gari kwa uthibitisho


Saa 2:16 usiku, Wolper aliongozana na waandishi hadi nyumbani kwake na walilikuta gari hilo likiwa ndani ya geti.
Anaonesha kadi ya umiliki

Huku akilionesha  gari hilo Wolper aliangusha kilio na kusema:
“Watu wananionea sana, wananichafua. Sijui lengo lao ni nini hasa? Kila kukicha nasingiziwa jambo, mara Jack kafanya hivi, mara vile.Mbaya zaidi, hata waigizaji wenzangu wapo wanaonichukia, au kwa kuwa nimepata maendeleo kidogo? Walitaka niporomoke kimaisha?”


Kuhakikisha kuwa Wolper hajanyang’anywa gari hilo, pia alionesha kadi yake ya umiliki.
SOURCE:GLOBAL PUBLISHERS

  ZINAZO HUSIANA NA HII:
 

Read more...

Friday, June 15, 2012

SABABU ZA ULINZI MKALI KWA LULU ZATAJWA

0 comments

Lulu akiingia Mahakama Kuu siku ya Jumatatu
Siri ya kumwekea ulinzi mkali Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye anakabiliwa na mashitaka ya kifo cha Steven Kanumba imebainika.

 Siri hiyo,kwa mujibu wa gazeti la IJUMAA, ilitolewa Jumatatu iliyopita na askari polisi mmoja ambaye hakuwa tayari kutajwa. Askari huyo siku hiyo ndie alikuwa na kazi ya kukagua watu wanaoingia kwenye Jengo la Mahakama ya Kuu kwa ajili kusikiliza kesi ya msanii huyo iliyokuwa ikitoa maamuzi ya kujadili umri wa Lulu.

Tangu kesi yake ilipoanza kutajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,msafara wa Lulu kwenda na kutoka mahaklamani umekuwa na ulinzi mkali wa askari wenye silaha nzito na Jumatatu wakati anafikushwa Mahakama Kuu hali ilikuwa hivyo hivyo,na pia kila aliyeingia Mahakamani alikuwa akipekuliwa vilivyo na askari wenye uzoefu wa kazi hiyo.Waandishi wa habari na wapigapicha walipekuliwa hata baada ya kuwa wameonesha vitambulisho vya kazi zao

Askari huyo alitoa mlolongo wa maelezo baada ya mwandishi mmoja kutaka kujua ni kwanini ulinzi umekuwa mkali kiasi hicho wakati anaelindwa ni msichana mdogo ambae haonekani kuwa anaweza kuwazidi nguvu na kutoroka.




Alisema kesi ya Lulu ni tofauti kidogo na zingine, na kwamba ulinzi huo si kwamaba Lulu anaweza kututoroka, isipokuwa kuna taarifa kuwa kuna kundi la watu linataka kumdhuru na hata kumuua

Alipouliza iwapo kuna taarifa ambazo zinafafanua kundi hilo ni la watu gani alisema taarifa hizo ni za kipolisi na si sahihi kuziweka hadharani.

“Hiyo ni siri ya ndani, lakini sisi tunasema ole wake mtu yeyote atakayenaswa akiwa katika mpango wa kutaka kutekeleza mpango huo au atakayethubutu, yaani naapa atakiona kilichomtoa kanga manyoya.”

 Lulu amekuwa kwenye ulinzi mkali mahakamani hata anapokwenda msalani. Na kuhusu hilo askari huyo alifafanua kuwa wamepewa amri ya kuimarisha ulinzi na kwa maana hiyo popote mshitakiwa anapokwenda ulinzi haulegezwi.Na hali hiyo ipo hata Segerea anapohifadhiwa mshitakiwa kwa sasa.

,",,,,,lengo ni kuimarisha ulinzi, hatuwezi kulegeza ulinzi mahali popote na hivi ninavyokwambia hata ulinzi wa Gereza la Segerea umeongezwa kwa ajili yake, kuna askari wametolewa magereza mbalimbali wameongezwa"

Inasemekana ulinzi wa Lulu mahakamani,pamoja na askari wa kawaida, pia kuna askari zaidi ya 20 waliovalia kofia za chuma na nguo maalum za kuzuia risasi bunduki aina ya SMG  20 zenye risasi 60 ndani , kila moja pembeni ikiwa na mkanda wa risasi 60 za ziada.

Alipoulizwa iwapo hilo kundi alilolitaja lina nguvu inayostaili kudhibitiwa kwa ulinzi uliopo,alisema kuwa kwa kawaida unapojiandaa kupambana na adui lengo ni kumshinda,kwa hiyo ni vyema kujkamilisha kwa kila kitu,na si vyema kukadiria nguvu ya adui yako

 
"...... ni lazima ujikamilishe, huwezi kujua mwenzio amejiandaa vipi, cha msingi sisi tumejiandaa vya kutosha, si unaona huu msafara wa magari matatu na askari zaidi ya 30, tena wenye silaha unazoziona na nyingine huzioni tumetoka Segerea kuja hapa kwa ajili ya mtu mmoja.Ni gharama kubwa kwa serikali maana kuna askari walitakiwa kwenda likizo lakini wamelipwa kwa ajili ya kusitishiwa likizo zao kwa sababu ya huyu Lulu,” alisema askari huyo.

Taarifa zilizopo zinadai kuwa hali ya wasiwasi wa usalama wa Lulu ilianza tangu yuko kituoni Oysterbay.Vyombo kadhaa vya habari viliripoti kuwa kundi la watu waliotoka kwenye mazishi ya Steven Kanumba lilielekea kituoni hapo katika staili ya mchakamchaka na nyimbo, wakidai wakabidhiwe Lulu.  


UNAWEZA KUCHUNGULIA NA HIZI:








Read more...

50 CENT ATAKA `KOLABO` NA WAYNE ROONEY

0 comments
Mwanamuziki mkali katika miondoko ya Hip hop 50 Cent ameelezea nia yake ya kushirikiana na mwanandinga mahili wa Uingereza anaekipiga katika timu ya Manchester United,Wayne Rooney.

Akiongea na gazeti la kila siku la Uingereza THE DAILY STAR 50 Cent amesema,anaamini kabisa kuwa akifanya collaboration ya kibiashara na Wazza wanaweza kuingiza kipato kikubwa hadi kufikia paundi bilioni 1,hasa ikiwa watawekeza pamoja kwenye biashara za migahawa na mavazi

"Mimi ni shabiki mkubwa wa Wayne,ana jina kubwa,ningependa siku moja tuwe washirika wa kibiashara
Soka la Ulaya kwa sasa ni biashara kubwa.Unaweza kuingiza pesa nyingi kwenye biashara ikwa utatumia majina ya wachezaji wenye majina makubwa"

"Nilishawahi kukutana na Wayne,ni mtu mzuri,ni mmoja wa wachezaji mahiri wa soka duniani,pia ana miaka mingi mbele katika kazi yake."

"Mimi wakati wote ni mtu wa mipango ya pesa na ninajua kuwa hata mtu wangu Wayne yuko hivyo.Nafasi za kutengeneza pesa hazina mipaka.Unawekeza kwenye migahawa Ulaya,maduka ya nguo,klabu za usiku.Kuingiza mamilioni ni poa, lakini kuingiza mabilioni ni jambo zuri zaidi na Wayne anafahamu hilo"

"Nimeshamualika Wayne, mashindano ya EURO 2012 yakiisha ningependa aje kunitembelea home Miami,yeye na familia yake.Hakuna atakaewasumbua wala kuwapiga picha,watu wangu wata hakikisha hilo halitokei"




Read more...

NIGERIA`S DONTOM NEW ALBUM OUT TODAY:IT CONTAINS NEW SONG FEATURING AKON

0 comments

Album cover
Nigeria musician Dontom is launching his new album `REVOLUTION` today according to media in Nigeria
The fair-skinned Nigerian music act will officially release the 16-tracker album in an album party at Monty Suites, Uyo, Akwa Ibom State. Dontom has featured Konvict Music boss, Akon in a new song entitled “Flexing Dollar”. The smash hit is one of the tracks in his new album
Dontom said the red carpet which will be handled by Flamz Magazine will start today evening around 7pm Nigerian time Other tracks in the album include Pump it and Iban Iban Iban.


Dontom became the first Nigerian artiste to perform at the African Cup of Nations, where he performed alongside Akon in the 2012 AFCON final held in Equatorial Guinea/Gabon.
   
Dantom (up left)with Akon

Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797