Pages

 

Saturday, July 13, 2013

SIRI NJE:MTANZANIA AAMBUKIZWA GONJWA LA ZINAA BBA!!

0 comments
Kwa sauti ya kunong`ona,mshiriki wa kiume kutoka Tanzania katika shindano la Big Brother Africa mwaka huu,Nando,amelalamika kuwa ameambukizwa ugonjwa wa zinaa uitwao Clamydia na mshiriki mwenzie wa kike kutoka Ghana aitwae Selly.

Kwa siku kadhaa sasa,Nando na Selly wamekuwa mbalimbali,jambo ambalo washiriki wenzao pamoja na watu wanaofuatilia shindano hilo wameshindwa kujua kwanini.

Nando alifichua siri hiyo ya kuambukizwa clamydia,gonjwa linaloambukizwa kupitia zinaa,lakini  hakuna mtu mwenye uhakika iwapo Nando anasema ukweli,Hata hivyo angalau kauli ya Nando imeweza kutegua kitendawili cha kwanini washiriki hao hawapatani tena siku hizi,tofauti na ilivyokuwa awali.

Katika siku chache zilizopita Nando amekuwa hajisikii vizuri na muda mwingi amekuwa akiutumia kupumzika kitandani,na hakuna aliyekuwa anajua alikuwa akisumbuliwa na nini.

Iwapo ni kweli Nando ameambukizwa gonjwa hilo,hakuna anaeweza kusema moja kwa moja kuwa Selly ndie aliemwambukiza Nando au Nando alikuwa na gonjwa hilo tangu mwanzo na pia tusipuuze uwezekano wa Nando kuwa anasumbuliwa na tatizo jingine,lakini kwa jinsi mtiriko wa mambo ulivyo,Nando amekuwa hajisiki vizuri na amekuwa akionana na daktari mara kadhaa.Zaidi ya hayo Selly amemdokezea mshiriki mwingine kutoka Botswana, O`neal,kuwa Big Brother amemshauri kutumia kinga anapokuwa mzigoni.Jambo ambalo linaashiria madai ya Nando kuwa na ukweli kiasi fulani

Nando tangu hapo amekuwa akimbughudhi Selly na ilifikia pabaya pale Nando alipokuwa akimdhihaki Selly aliposhindwa kwenye moja ya mashindano ndani ya jumba hilo,hali iliyopelekea Selly kuondoka huku akilia,na kuwaomba washiriki wenzie wam`nominate` ili atoke arudi nyumbani.

Wakati wa mahusiano yao Nando na Selly walikuwa kwenye mahaba mazito na haikuchukua hata siku kabla hawajavunja moja kati ya amri kumi za mwenyezi mungu.Lakini Nando aliwahi kumueleza Selly kuwa yeye hayuko `serious` kwenye mahusiano yao ila anataka kujifurahisha tu.

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797