Pages

 

Thursday, April 26, 2012

REAL MADRID VS BAYERN MUNICH,PICHA ZA MATUKIO

0 comments
Washabiki wa Bayern Munich wakipata vinywaji masaa machache kabla ya mechi jana
Read more...

Wednesday, April 25, 2012

UKATILI GANI HUU!BINTI WA MIAKA 8 ABAKWA NA KUNYOFOLEWA JICHO

0 comments
Kuna habari kuwa binti mmoja mwenye  umri wa miaka 8 amebakwa ,kung`atwa ng`atwa shingoni na hatimae kung`olewa jicho lake
Read more...

Tuesday, April 24, 2012

MOURINHO NA WACHEZAJI WA MADRID WAKISHANGILIA BARCELONA KUTOLEWA NA CHELSEA

0 comments
JOSE MOURINHO AKIONGOZA WACHEZAJI WAKE KUSEREBUKA WAKATI WAKISHANGILIA KUTOLEWA KWA BACELONA NA CHELSEA JANA USIKU

Read more...

SHUHUDIA MATUKIO YA MECHI YA BARCELONA VS CHELSEA KATIKA PICHA

1 comments
Read more...

ZOGO LAANZA KUGOMBEA KAMPUNI YA KANUMBA

0 comments
Hisani `TINO` Muya
MWIGIZAJI Nyota wa filamu na mtayarishaji wa filamu Swahiliwood, Hisani Muya` Tino`, amemshukia mchekeshaji na mwigizaji wa filamu Steven Mangere `Steve Nyerere` kwa kusema kuwa ni tatizo na mgombanishi wa wasanii wakubwa.
Read more...

BREAKING NEWS:VAN PERSIE ATWAA TUZO NYINGINE

0 comments
Robin van Persie
Straika wa Arsenal Robin van Persie asubuhi hii ametajwa kushinda tuzo ya  mwaka ya Mwanasoka Bora wa Waandishi,ikiwa ni siku tatu baada ya kutajwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa Chama cha Wanasoka wa Kulipwa Uingereza (PFA)
Read more...

ONA PICHA ZA WACHEZAJI WA CHELSEA WAKIJIFUA LEO

0 comments


Read more...

DIAMOND KUSHUKA NA HELKOPTA NDANI YA DAR LIVE JPILI HII.mpg

0 comments

Read more...

Monday, April 23, 2012

MASHUJAA MUSICA YAIKWANGUA `TWANGA`

0 comments




 
Lilian `INTERNET`
Read more...

ONA `LULU` ALIVYOFIKISHWA MAHAKAMANI LEO ASUBUHI

0 comments



Read more...

MAELFU HUENDA WAKAKOSA INTERNET IFIKAPO JULAI

0 comments

Kwa mujibu wa habari nilizozinyaka kitu ambacho watumiaji wengi wa kompyuta duniani hawakuwa wanakijua kuwa wezi wa kimataifa wanaotutumia mitandao ya kompyuta (international hackers)waliingiza tangazo feki kwenye mitandao duniani kwa lengo la kudhibiti mienendo ya kompyuta dunia nzima.Baada ya hujuma hiyo, kwa kasi ya kushangaza, Shirika la Upelelezi la Marekani, FBI, kwa kutumia kompyuta za serikali ya nchi hiyo, lilijanzisha mfumo salama wa mtandao wa dharura kuzinusuru kompyuta zilizoshambuliwa duniani kote zisijifunge…lakini
Read more...

Sunday, April 22, 2012

SARKORZY AANGUSHWA KATIKA UCHAGUZI

0 comments





Francois Hollande


Mgombea urais kwa tiketi ya chama cha kisoshalisti nchini Ufaransa Francois Hollande, ameshinda duru ya kwanza ya uchaguzi nchini humo.
Kura nyingi zikiwa zimehesabiwa Bw Hollande tayari amepata asilimia 28 ya kura.

Nicolas Sarkozy anafuatia kwa asilimia 27 hii ikiwa ni idadi ndogo zaidi kwa rais yoyote wa taifa hilo ambaye amewahi kugombea tena kiti hicho.
Haijawahi kutokea kuwa rais aliye madarakani anashindwa kwenye duru ya kwanza ya uchaguzi.
Na matokeo haya yanampa mpinzani wa Rais Sarkorzy, Francois Hollande nafasi nzuri sana katika duru ya pili ya uchaguzi huo utakaofanyika baada ya wiki mbili.
Hata hivyo kilicho washangaza wengi baada ya matokeo hayo kutangazwa ni idadi ya kura chama kinacho egemea upande wa kulia kilipata.
Kwa makadirio tu, mtu mmoja kati ya wapiga kura watano nchini Ufaransa alikipigia kura chama hicho, hii ikiwa idadi kubwa zaidi ya kura chama hicho cha Front Nationale kilichowahi kupata kwenye uchaguzi wowote nchini humo.
Rais Sarkorzy anasema matokeo hayo yanaonyesha hali ya wasi wasi raia wa nchi hiyo waliyonayo ni kura za maoni dhidi ya utawala wake.
Hata hivyo ametoa changamoto kwa mpinzani wake ajitokeze kwenye mdahalo kati yao kabla duru ya pili ya uchaguzi huo.
Lakini bila shaka kutokana na uchache wa kura alizopata dhidi ya Rais Sarkorzy, kiongozi huyo wa chama cha kisoshalisti, Francoise Hollande atakuwa makini sana asipoteze kura muhimu.
Bw Hollande anasema wafaransa wanaimani na mradi wake kwa nchi hiyo ambao umelenga kurejesha haki, usimamizi bora wa uchumi wa nchi, ukuzaji wa nafasi za kazi, kulinda viwanda na kujiandaa vyema kwa siku za usoni.
Read more...

NIZAR KHALFAN AREJEA....KUJIUNGA NA SIMBA

0 comments

Kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Nizar Khalfan aliyekuwa anacheza soka la kulipwa katika timu ya soka ya Vancouver Whitecaps ya Canada inayoshiriki ligi ya  Marekani, amejiunga rasmi na Mabingwa Watarajiwa’ wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu huu, Simba, ambapo habari kutoka ndani ya klabu hiyo ambazo bongostaz.blogspot.com imezipata, zinasema kuwa usajili wa mchezaji huyo umefanikishwa na mmoja wa wafadhili wa zamani wa klabu hiyo, Azim Dewji.
Dewji mwenyewe alipotafutwa kuzungumzia hilo alikiri na kusema kuwa, aliombwa na uongozi wa Simba kufanikisha usajili wa mchezaji huyo na kwamba baada ya kufanikiwa, ameshamkabidhi Nizar kwa uongozi wa klabu abapo aliongeza  kuwa mchezaji huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar na Moro United atakuwa na nafasi ya kuanza kuichezea Simba katika michuano ya kimataifa mwaka huu endapo itaingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.Nizar baadae atakabidhiwa  rasmi jezi atakayoitumia akiwa Simba.
 
Baada ya kuzing’oa Kiyovu ya Rwanda na Setif ya Algeria, wiki hii Simba itaishukia Al Ahly Shandy ya Sudan na kama ikifanikiwa kuvuka kiunzi hicho, itaingia katika raundi nyingine itakayoamua timu za kucheza Nane Bora Afrika

Nizar alijiunga na Vancouver Agosti 22 2009 na kuichezea mechi 9 msimu huo wa 2209 na akasaini mkataba mwingine wa kuichezea timu hiyo msimu wa 2010.Juni 12 2010 aliifungia Vancouver goli lake la kwanza katika mechi dhidi ya Austin Aztex na tarehe 9 Februari 2011 alisaini mkataba mpya wa mwaka mmoja wa kuichezea timu hiyo katika ligi ya MLS

Tarehe 23 Novemba, 2011 Vancouver iliachana na Nizar na kudondokea katika daftari la Philadephia Union lenye orodha ya wachezaji wa Major League Soccer walioachwa ili kutoa nafasi kwa timu zitakazo muhitaji.Miezi mitatu baadae Muungano Wa Philadephia ulimwachia huru Nizar Khalfan kabla ya msimu wa 2012
Read more...

Z ANTO AKANUSHA HABARI ZA KIFO CHA SAJUKI

0 comments
Z ANTO
JUMA `Sajuki` KILOWOKO

 Kupitia wall yake ya facebook,msanii wa muziki wa Bongoflava Ally Mohamed Ahmad maarufu kama Z Anto amekanusha taarifa zilizoenea kuwa msanii wa filam Tanzania Juma Kilowoko maarufu kama Sajuki amefariki dunia.Katika status yake aliyoipost saa sita usiku wa kuamkia leo msanii huyo aliandika:

"Kuugua sio kufa ukitaka kujua hli ona kifo cha Kanumba amekufa hali ya kuwa hakuwa na maradh yeyote yaliyokuwa yanamsumbua akabak Sajuki anayeumwa. Kuna uvumi usemao Sajuki Kafa hii inshu siyo kweli coz me hata nyumbani cjafika nimetoka hom kwake kumsalimia. Jua yupo hai huu ndiyo ukweli uliopo"
Hawa ni baadhi ya marafiki waliochangia kwenye wall yake

Read more...

Saturday, April 21, 2012

MGAWANYO WA MALI WAANZA KUITIKISA FAMILIA YA KANUMBA!

0 comments
WIKI mbili baada ya kifo cha aliyekuwa msanii nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba, wazazi wake; Charles Musekwa Kanumba na Mama yake, Flora Mutegoa ambao hawaishi pamoja, wametofautiana kuhusu suala la mali na mirathi.
Juzi, Mzee Kanumba aliibuka na kudai kuwa kuna kundi la watu linalomdanganya mama huyo wa marehemu kwamba linajua zilipo mali za Steven jambo ambalo alisema ni uongo na kumtaka awe na subira na asidanganyike.
Hata hivyo,kauli hiyo imepingwa na Mutegoa ambaye amehoji sababu za mumewe huyo kuzungumzia mali za mwanaye wakati huu. Alidai kuwa Mzee Kanumba hajawahi kuwa na mawasiliano na marehemu tangu mwaka 1999 alipoondoka kwao, Shinyanga.
Akizungumza katika mahojiano maalumu  juzi, Mzee Kanumba alimsihi mkewe kutodanganyika kwa kuwa yeye akiwa baba mzazi wa Kanumba anajua mali zote za mtoto wake na ndiye pekee anayeweza kumtendea haki katika kuzigawa.

“Mali za marehemu mwanangu nazifahamu zote, kwa hiyo hakuna shaka tutazigawa kwa sababu hakuna baba mwingine na haki yangu ipo palepale hakuna atakayeinyang’anya,” alisema na kuongeza:
“Nisingependa tuwape watu faida ya kuanza kuvutana mahakamani, tunatakiwa suala hili tulimalize sisi wenyewe kama tulivyompata mtoto wetu. Ninasisitiza mali zote zisifanyiwe vurugu ziachwe kama zilivyo.”
Katika kuthibitisha kwamba anazijua mali hizo, mzee huyo alisema Steven ameacha magari matatu, Sh40 milioni, viwanja viwili na akaunti mbili za benki na Kampuni ya Filamu.

Akerwa na tambiko
Mzee Kanumba alisema anasikitishwa na tambiko la Kihaya lililofanyika katika kaburi la mtoto wake, jambo ambalo alisema halikutakiwa kwa kuwa marehemu alikuwa Mkristo na alizikwa kwa imani hiyo.
“Mimi ni Mkristo, mtu aliyezikwa Kikristo huwezi tena kuanza kumfanyia mambo ya kipagani na kuanza kumtambikia, hiyo kwetu hairuhusiwi,” alisema Mzee Kanumba na kuongeza:
“Hata hivyo, marehemu alikuwa Msukuma, si Mhaya, itakuwaje wamtambikie Kihaya na kumwaga pombe aina ya rubisi huku marehemu alikuwa hatumii pombe na mimi pia situmii pombe?”
Kuhusu tambiko, Flora alisema hakuna kitu kama hicho kilichofanyika kwenye kaburi la mwanaye isipokuwa Wahaya wana mila zao kwa mwenzao aliyepatwa na msiba.

“Kilichofanyika siyo tambiko bali, ni mila zetu za Kihaya. Unapofiwa wenzako wanakuletea vitu kama kreti ya soda, bia na mkungu wa ndizi. Lile siyo tambiko ni mila tu, mimi pia ni Mkristo, siwezi kushiriki matambiko,” alisema.

Alisema suala hilo la kugawa mali au msimamizi wa mirathi walitakiwa kukutana pande mbili, yaani yeye na mkewe baada ya kupita siku 20 tangu alipozikwa waangalie namna ya kugawa huku akisisitiza kuwa hakuna mtu mwingine anayeruhusiwa kuingilia masuala hayo.

Mama amkana
Kwa upande wake, Mutegoa ambaye sasa bado yupo nyumbani kwa Kanumba, Sinza Vatican, Dar es Salaam alisisitiza kwamba marehemu hajawahi kuwasiliana na baba yake huyo tangu mwaka 1999.

Alieleza kushangazwa na taarifa hizo kutoka kwa mzazi mwenzake huyo na kusisitiza kuwa ni mapema mno kuanza kujadili mali za mtoto.

“Nasikitika kulisema hili kwani bado niko kwenye msiba wa mwanangu. Hata hivyo, sidhani kama mwenzangu anajua chochote kuhusu Steven, achilia mbali mali zake, hawajawahi kuwa na ukaribu mpaka kuweza kujua mali zake,” alisema na kuongeza:

“Hata hivyo, mbona anazungumzia mali tu, hivi anafahamu kama Steven alikuwa na madeni? Ninamsihi aachane na hizo habari kwa wakati huu kwani hazina uzito wowote ukilinganisha na thamani ya mtoto niliyempoteza,” alisema.
CHANZO CHA HABARI-THE CHOICE
Read more...

KAOMBA MAJI KALETEWA MAZIWA,KUMBE......DAH!

0 comments
Jamaa aktika mizunguko yake kafika mahali akajiskia ana kiu akaenda nyumba iliyokuwa jirani na hapo akaomba maji
ya kunywa.. Akaja mtoto na kikombe cha maziwa akampa.
Jamaa alipomaliza akaomba aongezwe dogo akamletea tena maziwa.. Jamaa ikabidi aulize, '
" vipi mbona mnagawa maziwa kwa wingi namna hiyo?'' 
dogo akamwambia kuwa panya alindumbukia kwenye maziwa ndio maana wote hapa nyumbani wameyakataa.. duh jamaa kusikia vile kwa mshangao akaachia kikombe chini kikavunjika.. yule dogo akapiga kelele eti ...
''Yalaaaaaaaaa kile kikombe Bibi anachotemea mate kimevunjikaaaaaaa....!!!!!!"
Read more...

Friday, April 20, 2012

WOLPER ABADILI DINI

0 comments
Katika picha ni Jacqueline Wolper na aina ya usafiri anaotembelea sasa
Staa wa kike anaekamata kwenye kiwanda cha muvi za kibongo Jacqueline Wolper ametajwa kuwa amebadili dini kutoka kwenye ukristo na kuhamia kwenye uislam.Staa huyo amenukuliwa na gazeti moja akikiri kuwa amefanya zoezi hilo wiki mbili zilizopita katika Masjid Kichangani pale Magomeni Mapipa na kuwa hivi sasa anakwenda kwa jina la Ilham.
Inadaiwa kuwa Wolper amechukuwa hatua hiyo baada ya kupata mchumba wa kiislam ambae kwa mujibu wa habari inadaiwa kuwa anatarajiwa kufunga nae ndoa karibu.Mchumba wake huyo ambaye ametajwa kuwa anakwenda kwa jina la Dulla au Dallas inadaiwa ameshajitambulisha kwa wazazi wa Wolper na kuwa Wolper mwenyewe alishaonana na wazazi wa Dallas
"Nimekuwa nikimchunguza Dallas kwa muda sasa na nimeridhika na nia yake ya kuishi na mimi kama mke na mume"
 Msanii huyo amesema kuwa sasa anajulikana kwa majina ya Ilham Wolper Dallas.Habari zinaendelea kusema kuwa baada ya Wolper kukubali kufunga ndoa na kuslim,mchumba wake huyo alitoa zawadi kwa mkewe mtarajiwa ambayo ni gari ya bei mbaya aina ya BMW X6 kama inayoonekana pichani
Read more...

THIBITISHO KUWA HABARI ZA MIONZI HATARI NI UZUSHI!!!!

0 comments
Picha hii inaonekana kama ya tukio la kutisha juu ya anga la jiji la Moscow, ilipigwa usiku wa tarehe 28 mwezi uliopita na jopo la wanasayansi wanaoishi kwenye kituo cha kimataifa cha angani wakati chombo chao cha kusafiri kikipita umbali wa maili 240 kutoka uso wa dunia.Kipande cha kunasa nishati ya jua(solar array panel)inayotumiwa kuendesha kituo hicho kinaonekana kushoto mwa picha hii....Hapa  upinde wa mwanga,taa za jiji na mwanga wa jua la afajiri vimepamba anga

Jana kulikuwa na mshikemshike dunia nzima wakati binadamu walipopata taarifa za kushtua za kushuka kwa mionzi hatari kutoka anga za mbali(COSMO RAYS).Watu walioathirika na taarifa hizo za uongo ni watumiaji wa mawasiliano ya kompyuta (INTERNET) na simu

Watu walitembeza ujumbe kupitia Internet na simu kutarifu kuwa kuanzi usiku wa manane hadi saa 9.30 usiku watu wote wanashauriwa kuzima simu zao za mkononi na kuzuwe ka mbali nao   kwa kuwa mionzi hatari inayotokea sayari ya Mars itatua kwenye uso wa dunia,,,kwa maana kwamba watakaokaidi ushauri huo watakumbwa na mtatizo yatakayosababishwa na mionzi hiyo 

Uongo huu ni kama marejeo ya ule uliowahi kusambazwa miaka michachae iliyopita na kuzusha tafrani duniani.Ujumbe  kwenye mtandao mmoja wa kijamii ulikuwa:


"2nite 1230 a.m to 330a.m Cosmo rays entering earth frm Mars, So switch off ur mobile at nite,don't keep ur cell with u & put it away while ur slping bcos thy are quite dangerous rays.NASA BBC NEWS."
Lakini taarifa za uhakika zinakanusha kuwa si NASA wala BBC waliowahi kutoa tahadhari kama hiyo.Uchunguzi wangu unaonesha kuwa habari hizi zilianza kidogo kidogo wiki tatu zilizopita katika nchi nyingi za Asia.Mtu mmoja aliandika katika internet kukanusha habari hizo:

 

"I searched ON NASA web page and on latest space and science news, the Cosmo rays is indeed a rumor. Someone received this message from a friend on a blackberry messenger and he or she wanted to know if its true,so they posted the news on the internet.I am replying from Windhoek ,Namibia and this rumor seems to be everywhere.I also received the message. I have a theory to present.Here is my hypothesis:Someone send the Cosmo rays message on the 1st of April to a friend,they didn’t want to make it obvious since 1st April is a fools Day,to make this believable, they make a joke three day after April Fools Day(1st of April 2012). My dad just calls me and orders i switch off my phone this night (April 3). No reason given. I then stumble on this cosmic rays thing on a friend’s FB page and deside to google, not out of doubt but for more information. Now i know better….. Information is key!"
Mtu mwingine kutoka Japan aliandika:
" WHY THE HELL ARE THEY SPREADING THIS STUPID RUMOR????
Mars doesn’t produce cosmic rays.
  THIS IS JUST A RUMOR"


Na mwingine kutoka hapa nchini aliyejitambulisha kwa jina la Hija aliandika:

 
.."I JUST RECEIVED SMS HERE IN TANZANIA WITH THE SAME CONTENT, BUT I WENT ALL OVER THE WEB – NOTHING SEEMS TO SUPPORT THIS STUPID RUMOR.
P/S STOP IT !"

Na huyu nae alichangia kwa kusema:


"AHAHAHA…BELATED APRIL FOOL’S DAY!!!!!!!!!!!!!!! LOL!!!"









 
Read more...

Thursday, April 19, 2012

MTOTO WA AJABU AZALIWA PAKISTAN!

0 comments
Mtoto mwenye miguu sita amezaliwa mjini Sukkur nchini Pakistan wiki iliyopita na amelazwa kwa uangalizi kwenye Taasisi ya Taifa Inayoshughulika na Afya ya  Watoto ya nchi hiyo,NICH,jijini Karachi.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo Dr. Jamal Raza,amefafanua kuwa katika hali isiyokuwa ya kawaida  ya mtoto huyo kuwa na miguu sita,mtoto huyo si mmoja kama anavyoonekana,bali ni watoto wawili katika mwili mmoja na kati yao mmoja bado hajakomaa.Amesema kuwa hali hii husababishwa na matatizo ya vinasaba(genetic desease) na kuwa matatizo hayo huwapata binadamu kwa uwiano wa kihesabu wa mtoto 1 kati ya watoto milioni 0.1.Amesema jopo la wataalam wa upasuaji watamfanyia uchunguzi wa kina mtoto huyo ili kuangalia namna ya kumsaidia na kwamba madaktari  bingwa kutoka nchi mbalimbali ikibidi wataitwa ili kusaidia
Read more...

Monday, April 16, 2012

MUAMBA ARUHUSIWA RASMI KUTOKA HOSPITALINI

0 comments
Fabrice Muamba akipeana mkono wa kuagana na madaktari Andrew Deaner na Sam Mohsin kutoka Kituo Cha Afya Cha Bart






                        
Read more...

EL HADJI DIOUF AKAMATWA NA POLISI

0 comments
Mwanasoka raia wa Senegal anaecheza mpira wa kulipwa nchini Uingereza katika klabu ya Blackburn Rovers El Hadji Diouf amekamatwa na polisi wa jiji la Manchester jana kwa tuhuma za kuhusika na fujo zilizotokea kwenye klabu moja ya usiku jijini humo
Katika fujo hizo ambazo zilitokea alfajiri ya kuamkia jana jumapili mtu mmoja anaetajwa kuwa na umri wamiaka 33 alijeruhiwa kichwani na shingoni
Diouf na watu wengine watano walikamatwa kwa tuhuma za kuhusika na fujo hizo na waliachiwa baadae kwa dhamana hadi kesi yao itakaposomwa hapo Mei 23 mwaka huu wakati uchunguzi juu ya tukio hilo unaendelea
Miaka 14 ya maisha ya soka la kulipwa ya Diouf imegubikwa na na matukioo ya utata kutokana natabia yake ya ukorofi.Hivi sasa mchezaji huyo amefungiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Senegal kucheza soka kwa muda wa miaka 5 baada ya kubwatuka mbele ya waandishi wa habari kuwa maafisa washirikisho hilo wanaendesha shughuli za shirikisho kama nyani
Read more...

MWENYEKITI WA VIJANA CCM ARUSHA AJITOA CCM

0 comments
         
Mwenyekiti waUmoja Wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa Wa Arusha Bw.James Ole Millya ametangaza kujiondoa kwenye chama hicho leo mchana .Habari zaidi ungana nami baadae
Read more...

Sunday, April 15, 2012

REAL MADRID YAFANYA MABADILIKO KWA KUHESHIMU UISLAM

0 comments
Timu ya soka ya Hispania Real Madrid wamefanya mabadiliko kwenye nembo(logo) yao ya sasa kwa kuheshimu matakwa ya kiimani ya mashabiki wao wa kiislam.Miamba hiyo ya Hispania inatarajiwa kuondoa alama ya msalaba ambayo ipo kwenye nembo hiyo kwa karibu karne moja sasa
Timu nyingine ya Hispania ambayo ilifanya zoezi hilo ni miamba wengine wa Hispania Barcelona ambao waliamua kuondoa alama ya msalaba kwenye nembo yao
Read more...

MUVI ZA KANUMBA ZAANZA KURUSHWA NA DSTV MWEZI MZIMA KUANZIA JANA

0 comments

 Kuanzia jana Jumamosi kampuni ya televisheni ya kulipia kwa njia ya satellite, DSTV,kupitia chaneli yao ya Africa Magic Swahili, imeanza kurusha filam zilizochezwa na msanii maarufu wa tasnia ya filam nchini Tanzania, Marehemu Steven Kanumba aliyefariki ghafla nyumbani kwake Sinza usiku wa  kuamkia Jumamosi ya tarehe 7 Aprili
 Ikiwa ni sehemu ya kumuenzi Kanumba chaneli hiyo jana ilirusha filam ya UNCLE JJ kuanzia saa 1.30  usiku na leo jumapili kuanzia saa 2.00 usiku chaneli hiyo itarusha filam ya iitwayo THIS IS IT (Part1 na 2)

Jumamosi ijayo tarehe 21 April watarusha filam  MORE THAN PAIN kuanzia saa1.30 usiku ikifuatiwa na YOUNG BILLIONAIRE  (Part 1 na 2)itakayorushwa Jumapili kuanzia saa 2.00 usiku nautratibu huo utakamilishwa Jumamosi ya terehe 28 kwa filam BLACK SUNDAY ambayo itakuwa kwenye skrini saa 3.20 usiku wa siku hiyo

Mkurugenzi mwendeshaji wa M-Net Africa Bi Biola Abi alimwelezea msanii huyo kuwa alikuwa ni mwenye kipaji, uwezo na malengo.
"Ni lazima tumfurahie kijana huyu mwenye mambo makubwa, ambaye alizichangamsha skrini zetu na kukonga nyoyo za wengi.Kifo chake ni pigo kubwa kwenye tasnia ya burudani Afrika,tunapenda kuwapa pole nyingi familia marafiki na wote waliompenda"

Marehemu Steven Kanumba akitaka kujua wasanii wa Afrika Mashariki watanufaika vipi na mpango wa DSTV wa kurusha filam zao.Hii ilikuwa siku ya uzinduzi wa chaneli ya Africa Magic Swahili

Read more...

TUZO ZA KILI AWARDS NCHINI TANZANIA

0 comments
Vijana wa THT wakishambulia jukwaa jana wakati wa sherehe za kukabidhi tuzo za Kili Awards hapa jijini Dar Es Salaam
Msanii wa Bongoflava, Diamond akipokea tuzo yake
Mama Khadija Kopa akitoa mchango wake kuchangamsha sherehe
Khadija Kopa,mumewe na watoto wao katika  pozibaada ya kupokea tuzo
Mchekeshaji Steve Nyerere na msanii wa maigizo Sinta wakifuatili utoaji wa tuzo
Diamond Platinum janaaliwafunika wasanii wenzake wa muziki baada ya kujinyakulia tuzo tatu za Kilimanjaro Music Awards maarufu kama Kili Awards.Diamond alishinda tuzo kwa kuchaguliwa na washabiki wa muziki nchini kwa njia ya kura na alijizolea tuzo ya video bora ya mwaka kwa video ya wimbo `Moyo Wangu`,mtumbuizaji bora wa mwaka na mtunzi bora wa mwaka.Msanii kutoka Tanga Roma alipata tuzo mbili zikiwa ni Wimbo Bora Wa Hip hop(Mathematics) na Msanii Bora Wa Hip hop

Msanii anaechipukia ambaye alishiriki kuimba wimbo wa Nai Nai, Ommy Dimpozi ameweza kujinyakulia tuzo mbili,msanii bora chipukuzi na Wimbo Bora Wa Kushirikiana (Collabo) kwa wimbo wa `Nai Nai` ambayo amegawana na mshiriki mwenza kwenye wimbo huo  Ally Kiba ambae nae amepata tuzo nyingine ya Wimbo Bora wa Rhumba/Zouk kwa wimbo wake wa `Dushelele`
Tuzo zilikuwa hivi:
                  KILI TZ MUSIC AWARD (KTMA) 2012
1. Wimbo Bora Wa Reggae- Arusha Gold , Warriors from East

2. Wimbo Bora wa Dancehall- Maneno Maneno , Queen Darlin'
 
3. Wimbo Bora Zouk Rhumba- Dushelele By Ally Kiba
 
4. Wimbo bora wenye vionjo vya asili- Vifuu Tundu By A.T
 
5. Wimbo Bora wa Taarab- Nani kama Mama By Isha Mashauzi
 
6. Wimbo Bora wa Kiswahili(Bendi)- Dunia Daraja By Twanga Pepeta
 
7. wimbo Bora wa Afro Pop- Hakunaga By Suma Lee
 
8. Wimbo Bora wa R&B- My Number 1 Fan By Ben Pol
 
9. Wimbo Bora wa Hip Hop- Mathematics By Roma
 
10. Msanii Bora Anayechipukia- Ommy Dimpoz
 
11. Rapa Bora wa Bendi-Kitokololo
 
12. Msanii Bora wa Hip Hop- ROMA
 
13. Wimbo Bora wa Kushirikiana- Nai Nai By Ommy dimpoz ft Ally Kiba
 
14. Wimbo Bora Afrika Mashariki- Kigeugeu By Jaguar
 
15. Mtumbuizaji Bora wa kike- Khadija Koppa
 
16. Mtumbuizaji Bora wa Kiume- Diamond Platnumz
 
17. Mtunzi Bora wa kiume-Diamond Platnumz
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797