Pages

 

Tuesday, April 24, 2012

BREAKING NEWS:VAN PERSIE ATWAA TUZO NYINGINE

0 comments
Robin van Persie
Straika wa Arsenal Robin van Persie asubuhi hii ametajwa kushinda tuzo ya  mwaka ya Mwanasoka Bora wa Waandishi,ikiwa ni siku tatu baada ya kutajwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa Chama cha Wanasoka wa Kulipwa Uingereza (PFA)

Tuzo hizo ni kwa kutambua mchango wake binafsi kwa timu yake msimu huu,ambayo ameifungia magoli 34 na kuisaidia kuingia kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Ulaya.Scott Parker ndiye alitwaa tuzo hiyo msimu uliopita,tuzo ambazo hutokana na kura za waandishi wa habari za michezo wapatao 400 na washiriki wengine katika mchakato wa kupiga kura
Minong`ono ilienea kuwa Van Persie angetwaa tuzo hiyo na katika upigaji kura mdachi huyo alikuwa mbele akiwaacha wapinzani wake Wayne Rooney,Paul Scholes na mmarekani Clint Dempsey ambaye amesimama nafasi ya nne.Van Persie anakuwa mchezaji wa kwanza wa Arsenal kuchukua tuzo hiyo tangu Thierry Henry alipoitwaa mwaka msimu wa 2005 - 2006 na anakuwa mdachi wa pili tangu mchezaji mwengine wa Arsenal Denis Bergkamp alipoitwaa msimu wa 1997 - 1998 baada ya kuisaidia Arsenal kutwaa mataji mawili,la ligi kuu na la F.A

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797