Pages

 

Sunday, April 22, 2012

NIZAR KHALFAN AREJEA....KUJIUNGA NA SIMBA

0 comments

Kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Nizar Khalfan aliyekuwa anacheza soka la kulipwa katika timu ya soka ya Vancouver Whitecaps ya Canada inayoshiriki ligi ya  Marekani, amejiunga rasmi na Mabingwa Watarajiwa’ wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu huu, Simba, ambapo habari kutoka ndani ya klabu hiyo ambazo bongostaz.blogspot.com imezipata, zinasema kuwa usajili wa mchezaji huyo umefanikishwa na mmoja wa wafadhili wa zamani wa klabu hiyo, Azim Dewji.
Dewji mwenyewe alipotafutwa kuzungumzia hilo alikiri na kusema kuwa, aliombwa na uongozi wa Simba kufanikisha usajili wa mchezaji huyo na kwamba baada ya kufanikiwa, ameshamkabidhi Nizar kwa uongozi wa klabu abapo aliongeza  kuwa mchezaji huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar na Moro United atakuwa na nafasi ya kuanza kuichezea Simba katika michuano ya kimataifa mwaka huu endapo itaingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.Nizar baadae atakabidhiwa  rasmi jezi atakayoitumia akiwa Simba.
 
Baada ya kuzing’oa Kiyovu ya Rwanda na Setif ya Algeria, wiki hii Simba itaishukia Al Ahly Shandy ya Sudan na kama ikifanikiwa kuvuka kiunzi hicho, itaingia katika raundi nyingine itakayoamua timu za kucheza Nane Bora Afrika

Nizar alijiunga na Vancouver Agosti 22 2009 na kuichezea mechi 9 msimu huo wa 2209 na akasaini mkataba mwingine wa kuichezea timu hiyo msimu wa 2010.Juni 12 2010 aliifungia Vancouver goli lake la kwanza katika mechi dhidi ya Austin Aztex na tarehe 9 Februari 2011 alisaini mkataba mpya wa mwaka mmoja wa kuichezea timu hiyo katika ligi ya MLS

Tarehe 23 Novemba, 2011 Vancouver iliachana na Nizar na kudondokea katika daftari la Philadephia Union lenye orodha ya wachezaji wa Major League Soccer walioachwa ili kutoa nafasi kwa timu zitakazo muhitaji.Miezi mitatu baadae Muungano Wa Philadephia ulimwachia huru Nizar Khalfan kabla ya msimu wa 2012

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797