Pages

 

Thursday, April 19, 2012

MTOTO WA AJABU AZALIWA PAKISTAN!

0 comments
Mtoto mwenye miguu sita amezaliwa mjini Sukkur nchini Pakistan wiki iliyopita na amelazwa kwa uangalizi kwenye Taasisi ya Taifa Inayoshughulika na Afya ya  Watoto ya nchi hiyo,NICH,jijini Karachi.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo Dr. Jamal Raza,amefafanua kuwa katika hali isiyokuwa ya kawaida  ya mtoto huyo kuwa na miguu sita,mtoto huyo si mmoja kama anavyoonekana,bali ni watoto wawili katika mwili mmoja na kati yao mmoja bado hajakomaa.Amesema kuwa hali hii husababishwa na matatizo ya vinasaba(genetic desease) na kuwa matatizo hayo huwapata binadamu kwa uwiano wa kihesabu wa mtoto 1 kati ya watoto milioni 0.1.Amesema jopo la wataalam wa upasuaji watamfanyia uchunguzi wa kina mtoto huyo ili kuangalia namna ya kumsaidia na kwamba madaktari  bingwa kutoka nchi mbalimbali ikibidi wataitwa ili kusaidia

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797