Pages

 

Sunday, April 15, 2012

TUZO ZA KILI AWARDS NCHINI TANZANIA

0 comments
Vijana wa THT wakishambulia jukwaa jana wakati wa sherehe za kukabidhi tuzo za Kili Awards hapa jijini Dar Es Salaam
Msanii wa Bongoflava, Diamond akipokea tuzo yake
Mama Khadija Kopa akitoa mchango wake kuchangamsha sherehe
Khadija Kopa,mumewe na watoto wao katika  pozibaada ya kupokea tuzo
Mchekeshaji Steve Nyerere na msanii wa maigizo Sinta wakifuatili utoaji wa tuzo
Diamond Platinum janaaliwafunika wasanii wenzake wa muziki baada ya kujinyakulia tuzo tatu za Kilimanjaro Music Awards maarufu kama Kili Awards.Diamond alishinda tuzo kwa kuchaguliwa na washabiki wa muziki nchini kwa njia ya kura na alijizolea tuzo ya video bora ya mwaka kwa video ya wimbo `Moyo Wangu`,mtumbuizaji bora wa mwaka na mtunzi bora wa mwaka.Msanii kutoka Tanga Roma alipata tuzo mbili zikiwa ni Wimbo Bora Wa Hip hop(Mathematics) na Msanii Bora Wa Hip hop

Msanii anaechipukia ambaye alishiriki kuimba wimbo wa Nai Nai, Ommy Dimpozi ameweza kujinyakulia tuzo mbili,msanii bora chipukuzi na Wimbo Bora Wa Kushirikiana (Collabo) kwa wimbo wa `Nai Nai` ambayo amegawana na mshiriki mwenza kwenye wimbo huo  Ally Kiba ambae nae amepata tuzo nyingine ya Wimbo Bora wa Rhumba/Zouk kwa wimbo wake wa `Dushelele`
Tuzo zilikuwa hivi:
                  KILI TZ MUSIC AWARD (KTMA) 2012
1. Wimbo Bora Wa Reggae- Arusha Gold , Warriors from East

2. Wimbo Bora wa Dancehall- Maneno Maneno , Queen Darlin'
 
3. Wimbo Bora Zouk Rhumba- Dushelele By Ally Kiba
 
4. Wimbo bora wenye vionjo vya asili- Vifuu Tundu By A.T
 
5. Wimbo Bora wa Taarab- Nani kama Mama By Isha Mashauzi
 
6. Wimbo Bora wa Kiswahili(Bendi)- Dunia Daraja By Twanga Pepeta
 
7. wimbo Bora wa Afro Pop- Hakunaga By Suma Lee
 
8. Wimbo Bora wa R&B- My Number 1 Fan By Ben Pol
 
9. Wimbo Bora wa Hip Hop- Mathematics By Roma
 
10. Msanii Bora Anayechipukia- Ommy Dimpoz
 
11. Rapa Bora wa Bendi-Kitokololo
 
12. Msanii Bora wa Hip Hop- ROMA
 
13. Wimbo Bora wa Kushirikiana- Nai Nai By Ommy dimpoz ft Ally Kiba
 
14. Wimbo Bora Afrika Mashariki- Kigeugeu By Jaguar
 
15. Mtumbuizaji Bora wa kike- Khadija Koppa
 
16. Mtumbuizaji Bora wa Kiume- Diamond Platnumz
 
17. Mtunzi Bora wa kiume-Diamond Platnumz

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797