Pages

 
Showing posts with label kimataifa. Show all posts
Showing posts with label kimataifa. Show all posts

Wednesday, July 17, 2013

BAN KI MOON ALAANI MAUAJI YA WANAJESHI WA TANZANIA DARFUR

0 comments


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UNO), Ban K-Moon(pichani), amesema amesikitishwa na kuhuzunishwa na mauaji ya askari saba wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), lililofanywa na waasi wa Sudan Julai 13, mwaka huu.
Askari hao wa JWTZ waliokuwa Darfur, Sudan ya Kusini kulinda amani kwa mujibu wa UNO, walishambuliwa na waasi hao karibu na kambi ya Manawashi eneo la Khor Abeche, mji wa Darfur Jimbo la Nyala ambapo pia askari wengine 17 walijeruhiwa baadhi yao vibaya.
Katika salamu zake hizo kupitia kwa Msemaji wake, Katibu Mkuu huyo wa Uno, ameelezea masikitiko yake kuhusiana na vifo hivyo na kutoa pole kwa familia za marehemu waliokuwa wakilinda amani, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Vikosi vya Umoja wa Afrika kwa Umoja wa Mataifa vya Kulinda Amani (Unamid).

Ban K-Moon amelaani shambulio hilo dhidi ya Unamid na kuelezea matumaini yake kwamba Serikali ya Sudan itachukua hatua zinazofaa kuhakikisha kwamba wahusika wanafikishwa mbele ya sheria.
Wakati huo huo, Taarifa iliyotolewa na Unamid juzi jioni ilisema wajumbe wa Baraza la Usalama wanalaani kwa nguvu zote mashumbulizi hayo dhidi ya askari wa vikosi vya Unamid.
"Wajumbe wa Baraza la Usalama wameelezea masikitiko yao na kutuma salamu za pole kwa familia za marehemu hao pamoja na kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Aidha, wameitaka Sudan kufanya upelelezi wa kina kuhusiana na tukio hilo na kuwafikisha wahalifu hao mbele ya mkono wa sheria.
Taarifa hiyo ya Unimad iliongeza kuwa shambulio lolote dhidi ya vikosi vya Unimad halikubaliki na kuonya kuwa lisitokee tena shambulio lingine la aina hiyo huku ikisisitiza pande zinazovutana Darfur kushirikiana kwa lengo la kufikia malengo yaliyokusudiwa.


Read more...

Sunday, July 14, 2013

MUNGU KAINGILIA KATI?MALAIKA JIBRIL(GABRIEL)`AONEKANA KWENYE MAANDAMANO` MISRI

0 comments

Waandamanaji wanaomuunga mkono Rais Morsi,wamedai kuwa wameona mwanga wa aina yake..

Kwa mujibu wa gazeti la Al Arabia,taarifa hizi zimetolewa na muhubiri mmoja anayeegemea upande wa Morsi,wakati akiwahutubia wafuasi wa Morsi katika viwanja vya Rabia all-Adawiya jijini Kairo,

Katika hotuba hiyo iliyorushwa na vituo kadhaa vya televisheni vya Misri,muhubiri huyo amesema kuwa malaika Jibril ameonekana miongoni mwa wafuasi wa Morsi wanaoandamana

Muhubiri huyo Sheikh Ahmad Abdel Hadi kutoka kikundi cha Muslim Brotherhood amesisitiza kuwa watu wanaoheshimika kutoka Madina Al-Munawara, Saudi Arabia, wamemueleza kuhusu ndoto malaika Jibril alivyotokea na kuingia kwenye msikiti wa Rabia aL-Adawiya na kuwataka watu wanaoswali wakae kama walivyo.

Vile vile kuna taswira nyingine ilyotokea ya Mtume Muhammad(SAW)amejumuika na Bw Morsi na watu kadhaa.Katika taswira hiyo anasema muda wa swala ulipofika,watu walimuomba Muhammad(SAW)aongoze swala lakini Mtume alimteua Morsi aongoze swala

Muhubiri huyo amesema mtu mwingine wa kuaminika ametokewa na taswira inayoonesha ngamia wapatao 50,pamoja na vijana nawatoto kadhaa wakiwa jangwani.Baada ya muda wale ngamia,vijana na watoto wakaanza kusikia kiu kali.Walianzakuswali kumuomba Mungu awasaidie na papo hapo ardhi aligawanyika na che chem ya maji ikatokea.Baada ya kumaliza kiu yao,sauti ikasikika ikiwaambia vijana `watunzeni ngamia wa Rais Mohammed Morsi`


Wakati huo huo Sheikh Mosad Anwar wa Misri amemfananisha Morsi na Nabii Yusuf,kwa kuwa wote wametawala baada ya kupitia misukosuko kwa miaka mingi ikiwa pamoja na kuwekwa kizuizini mara kwa mara

Katika hatua nyingine Sheikh Shawki Abdel Latif mwakilishi wa Wizara ya Awqaf(Kusimamia Msaada ya Kijamii)ameibeza kauli ya muhubiri Abdel Hadi kwa kusema kuwa "..ndoto kama hizo zimelenga katika kuhalalisha vitu visivyofaa vionekane kuwa vinafaa,Wanaweka sumu kwenye asali kwa  kuongea uongo juu ya Mtume Muhammad,amani iwe juu yake"
Shekh huyo alipoulizwa zaidi na gazeti la Al Arabiya kuhusu uwezekano wa malaika Jibril kutokea katika msikiti wa Rabia al-Alawiya alijibu:"Huo ni uongo pia,Jibril ni Malaika na hutokea mbele ya Mtume wa Mungu tu"

"Maneno kama hayo ni njia ya kujaribu kutumia dini kwa manufaa ya kisiasa na kutaka kuhalalisha utawala wa Rais Morsi" Aliongeza Sheikh Abdel Latif
Sheikh Abdel Latif hakuishia hapo,alipendekeza kukamatwa kwa watu wanaoeneza habari kuhusu ndoto ya Mtume Muhammad akimwambia Morsi aongoze swala kwani kauli hiyo ni `tusi` kwa Uislam na Mtume mwenyewe

Makumi Elfu ya waandamanaji wanaomuunga mkono Rais Morsi walimiminika mitaani kwa wingi kuanzia juzi Ijumaa,wakiapa kupambana ili BwMorsi arejeshwe madarakani huku watu wanaounga mkono kupinduliwa kwa Rais Morsi wakiendelea na maandamano na kuweka pabaya mustakabali wa kisiasa wa Misri.

Chama cha Muslim Brotherhood,alikotokea Rais Morsi kinazidi kusambaratika kufuatia kukamatwa kwa viongozi waandamizi kadhaa na wengine kukimbilia kusikojulikana kufuatia mapinduzi ya Julai 3,ambayo chama hicho na wafuasi wake kimeyaita ni ya kijeshi.

Milio ya risasi katika eneo la jeshi jumatatu ya mwanzoni mwa wiki inayokwisha,imewaacha  makumi ya watu wakipoteza maisha yao na wengine makumi kujeruhiwa kulingana na takwimu za Wizara ya Afya ya nchi hiyo
 
Read more...

Saturday, July 13, 2013

BOMOA BOMOA:FAMILIA NZIMA YAJICHOMA MOTO MBELE YA OFISI ZA MANISPAA!

0 comments
Moshi ukiwa umezagaa angani mbele ya jengo la serikali muda mfupi baada ya tukio hilo
Watu watano wa familia moja wamejichoma moto mbele ya ofisi za serikali kwa kile walichodai kupinga mpango wa serikali kubomoa nyumba waliyokuwa wakiishi.

Tukio hilo la kutisha na kusikitisha limetokea magharibi mwa India katika mji wa Rajkot,ulioko katika jimbo la Gujarat na limehusisha mama,watoto wake wawili wa kiume na wake zao.

Hasumati Dalvani mama mwenye umri wa miaka 62,wanawe ,Bharat Masingh,40 na Girish Masingh,38 pamoja na wake zao Asha na Rekha,walijimiminia mafuta ya taa mwilini kabla ya kujilipua.

Familia hiyo imekuwa ikipambana kupinga mpango wa serikali kubomoa nyumba yao waliyoishi kwa miaka 35 sasa,baada ya wakazi wa eneo hilo kulalamika kuwa haikuwa salama.
Mmoja wa majeruhi waliojilipua akisaidiwa kupelekwa hospitali

Watu walioshuhusia tukio hilo walijaribu kuzima moto kwa kutumia vipande vya mapazia,lakini walikuwa wameshachelewa.Watoto  na wake zao walifariki baada ya kufikishwa kwenye Hospitali ya Umma ya Rajkot.

Msemaji wa Hospitali hiyo Dakta Sanjay Shah amesema kuwa majeruhi walifikishwa wakiwa wameungua asilimia 90 hadi 95 ya miili yao,walikuwa katika halimbaya sana.Madaktari walijaribu kuokoa maisha yao lakini ilishindikana.Mama mtu bado yuko hai lakini yuko katika hali mbaya sana

Katika hatua nyingine Meya wa jiji la Rajkot,wakati akitoa rambirambi kwa familia hiyo alisema Manispaa yake haikuwa na mpango wa kubomoa nyumba ya familia hiyo.

Polisi wa huko wamewadaka watu wengine wanne ambao wanadaiwa kuchochea tukio hilo la kujiua.Manispaa tayari imethibitisha kutoa  ya kiasi cha Rupia Milioni 2 na laki 5,sawa na wastani wa Shilingi milioni 66 za kitanzania kama fidia kwa familia hiyo
Read more...

Friday, July 12, 2013

MAMA KUTOKA KENYA ASABABISHA BINTI MFALME WA SAUDIA KUKAMATWA MAREKANI

0 comments
Picha kutoka kwenye jalada la kesi iliyotolewa na Idara ya Polisi,ikimuonesha Meshael Alayban
Mama mmoja aliyetajwa  kuwa mwana mfalme kutoka Saudi Arabia amekamatwa katika jimbo la Carlifonia nchini Marekani kwa tuhuma za kushiriki biashara ya kuuza watu.
Meshael Alayban, 42, anakabiliwa na mashtaka ya kumlazimisha mama mmoja kutoka Kenya kufanya kazi kwa zaidi ya masaa kumi na sita kila siku, na kumlipa kiasi kidogo cha pesa kuliko walivyokuwa wameafikiana.
Maafisa wa serikali wa wa eneo hilo, wamesema kuwa Bi Alayban alichukua paspoti  ya mama huyo, hatua iliyomfanya atoroke.
Mawakili wa binti mfalme huyo wamesema kuwa kesi hiyo imesababishwa namzozo kuhusu hali ya utendaaji kazi.
Novemba mwaka uliopita, wapiga kura katika jimbo la Carlifonia, waliidhinisha sheria kali dhidi ya watu watakaopatikana na hatia ya kuhusika na ulanguzi wa watu.


Saudi princess charged in Calif. with human trafficking
Binti Mfalme Meshael Alayban (Kulia) akimsikiliza mkalimani wakati alipofikishwa mahakamani jana huko Santa Ana California
Iwapo atapatikana na hatia, Bi Alayban, huenda akahukumiwa kifungo cha miaka kumi na miwili gerezani, adhabau ambayo ni asilimia mia moja zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali, kabla ya wapiga kura kuidhinisha mabadiliko ya sheria hiyo..Waendesha mashtaka wanasema Bi Alayban, ni mmoja wa wake sita wa Mwana Mfalme Abdulrahman bin Nasser bin Abdulaziz al-Saud, mmoja wa watoto wa kiume wa familia ya kifalme nchini Saudi Arabia.

Mama aliezua sakata hilo  Mkenya ambaye jina lake halijatolewa, aliajiriwa na Bi Alayban miaka miwili iliyopita, baada ya kuandikiana makubaliano na shirika moja la kutoa ajira nchini Saudia.
Mama huyo alihaidiwa kulipwa dola elfu moja mia sita kila mwezi na kuwa atafanya kazi masaa manane kila siku kwa siku tano.
Lakini, Bi Alayban amekuwa akimlipa dola mia mbili ishirini kila mwezi na kulazimishwa kufanya kazi kwa zaidi ya masaa kumi na sita kila siku.
Mama huyo kutoka Kenya vile vile amedai, kunyang`anywa paspoti yake ya kusafiria na alirudishiwa muda mfupi tu kabla ya wao kusafiri kwenda Carlifonia na Bi Alayban.
Akiwa Carlifonia, alilazimishwa kufanya kazi nyingi za nyumbani kwa familia nane zilizoishi katika vyumba vinne tofauti, ambako amedai alishikwa kama mateka .
Wakati alipofanikiwa kutoroka, alisimamisha basi moja na kwenda moja kwa moja hadi kituo cha polisi.
Bi Alayban alikamatwa siku ya Jumatano ya juzi na kufikishwa mahakamani jana.
Aliachiliwa huru kwa dhamani ya dola milioni tano na kuamriwa kurejesha pasi ya kusafiria ya mama huyo kutoka Kenya.
Aidha Bi Alayban sasa atavalia chombo maalum ambacho kitatoa maelezo ya mahala aliko na hataruhusiwa kuondoka Marekani hadi kesi hiyo itakapokamilika.
 Waendesha Mashtaka walitaka jaji kumuachilia kwa dhamani ya dola milioni Ishirini au anyimwe dhamana kwa kuwa yeye ni tajiri mkubwa na angeweza kutoroka
Read more...

MALEMA AZINDUA RASMI CHAMA CHAKE

0 comments


Aliyekuwa kiongozi wa vugu vugu la vijana la chama tawala nchini Afrika Kusini cha ANC, Julius Malema amezindua kundi la kisiasa litakalojulikana kama Wapiganiaji wa Uhuru wa Kiuchumi au Economic Freedom Fighters, EFF.
Malema, ambaye alitimuliwa kutoka kwa chama cha ANC, mwaka wa 2012, amesema chama chake cha EFF kinataka zoezi la kugawanya mashamba kuanzisha upya na pia kutaifishwa kwa migodi yote ya madini.
''Tutagawana ardhi sisi zote ukiwa mweusi au mweupe. Lakini ukikataa kugawanya itamaanisha kuwa utalazimishwa kufanya hivyo'' Alisema Bwana Malema.
Ametaja dhamira kuu ya vugu vugu hilo kuwa kupamabana mfumo wa kipebari.
Akiwa amevalia kofia nyekundu iliyo na maandishi ''Amirijeshi Mkuu wa EFF'' Bwana Malema amewaambia waandishi wa habari kuwa chama chake kimebuniwa ili kutetea maslahi ya raia wanaoteseka katika maeneo ya mashinani.

Malema ambaye alikuwa mmoja wa washirika wa karibu wa rais Zuma, kwa sasa ni mmoja wa wakosoaji wakubwa na aliongoza mikakati ya kumuondoa kama kiongozi wa chama cha ANC wakati wa mkutano wa baraza kuu la chama hicho mwaka wa 2012.
Malema ameshutumu rais Zuma kwa kutoimarisha juhudi za kuwasaidia raia weusi wa nchi hiyo ambao ni masikini na waliompigia kura.
Hata hivyo haijabainika ikiwa atawania kiti chochote katika uchaguzi mkuu utakaoandaliwa mwaka ujao, akisema kuwa uamuzi huo utatolewa baada ya mkutano wa baraza kuu la chama hicho cha EFF utakaofanyika mwisho wa mwezi huu.
Wachanganuzi wa kisiasa wanasema idadi kubwa ya raia wa Afrika Kusini, wamepoteza imani na chama cha ANC, ambacho kimekuwa madarakani tangu mwaka wa 1994.
Rais wanasema maafisa wengi wa chama hicho ni wafisadi na hawana nia ya kuimarisha hali ya maisha
Read more...

Wednesday, July 10, 2013

ASIKUDANGANYE MTU,RUSHWA BADO IPO JUU DUNIANI,KENYA YAONGOZA AFRIKA MASHARIKI

0 comments
Watu wengi duniani wanaamini kuwa ufisadi umezidi huku mmoja kati ya watu wanne akikiri kutoa rushwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Shirika la kupambana na ufisadi duniani Transparency International limetoa ripoti ya utafiti wake jana, inayoonyesha kuwa viwango vya ufisadi duniani bado viko juu lakini watu wana uwezo wa kuukomesha.
Kati ya nchi kumi zilizotajwa,nane zinatokea barani Afrika.
ambapo katika kanda ya Afrika mashariki Kenya bado iko nyuma kukabiliana na rushwa .
Read more...

"MANDELA SASA ANAFUNGUA MACHO NA KUTABASAM"-WAJUKUU

0 comments
Swati Dlamini (kushoto) na Zaziwe Dlamini-Manaway (kulia)
Wajukuu wawili wa Rais Mweusi wa Kwanza wa Afrika Kusini Nelson Mandela,waliuvamia mtandao wa Twitter na kudumu humo kwa masaa tisa wakijibu maswali juu ya maendeleo ya afya ya kiongozi huyo wa zamani. na mzozo wa kiukoo unaofukuta juu  ya eneo la maziko

Zaziwe Dlamini-Manaway na Swati Dlamini wamesema babu yao sasa anweza kutabasam na kuwa ukoo bado umefungamana

Wajukuu hao walikuwa wakishiriki katika kipindi cha Tv kinachohusu maisha halisi (Reality Tv)kiitwacho `Being Mandela` ambacho kimeanza kuoneshwa nchini Marekani.

Bw.Mandela amelazwa hospitali akiwa mahututi katika mji mkuu wa Afrika Kusni, Pretoria.

Alikimbizwa hospitalini zaidi ya mwezi mmoja uliopita kutokana na kusumbuliwa na maradhi yaliyoshambulia mapafu yake

Taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Rais wa nchi hiyo ilisema Bw. Mandela bado hali yake si shwari ila imeimarika.

Mandela aliwekwa kizuizini kwa miaka 27 kutokana na harakati zake za kupinga utawala wa kikandamizaji wa wazungu wachache,kabla hajachiwa mwaka1990, na miaka minne baadae alichaguliwa kuwa Rais wa Afrika Kusini.Aliachia ngazi baada ya kutawala kwa miaka mitano.

Wiki mbili zilizopita mzozo uliibuka katika ukoo wa Bw.Mandela juu ya eneo la kuzikia na masalia ya watoto wake watatu ambao walifariki katika miaka ya 1947,1969 na 2005.

Mahakama iliamuru masalia ya watoto hao wa Mandela yahamishwe kutoka Mvezo,mji aliozaliwa Bw.Mandela ,na yapelekwe yakazikwe Qunu,katika Jimbo la Eastern Cape, anapoishi baada ya kustaafu.

Kesi ilifunguliwa na jamaa 16 wa ukoo huo ambao walipinga kitendo cha mjukuu wa kiume wa Bw.Mandela, Mandla. kufukua masalia ya watoto hao wa Bw. Mandela na kuyahamisha na kuyapeleka Mvelo bila kufuata taratibu, akitegemea Bw.Mandela azikwe huko pia.

Katika kujibu maswali waliyoulizwa wajukuu hao wawili wa Mandela walisema hawajivunii kuona jinsi mambo yalivyogeukia kuwa hivyo.

"Yameshatokea,ila mwisho wa siku bado tuko kama watu wa ukoo mmoja" waliandika kwenye mtiririko wa ujumbe katika ukurasa wa Twitter wa kipindi hicho cha  `Being Mandela`


Walipotakiwa kuelezea mipango ya ukoo katika kurudisha umoja wao,walijibu,"Tunawaruhusu wazee wa ukoo watuongoze.Umoja wetu haujapotea moja kwa moja,ni mwenzetu tu aliamua kufanya mabo tofauti,ila siku zote tutaendelea kumpenda binamu yetu (Mandla)"

Walipotakiwa kuzungumzia maendeleo ya afya ya Bw .Mandela walisema anafungua macho na kutabasam.

Mabinti hawa ni watot wa binti waNelson Mandela,Zenani kutoka katika ndoa yake na mkewe wa zamani Winnie Madikizela-Mandela.

Bw.Mandela alioa na kuacha mara mbili na sasa amemuoa aliekuwa mke wa Rais wa zamani wa Msumbiji Samora Machel,Graca.


Read more...

Monday, July 8, 2013

MOS DEF ATOA VIDEO MAALUM YA MWEZI WA RAMADHAN JUU YA WAFUNGWA GUANTANAMO BAY

0 comments

Wakati mwezi mtukufu wa Ramadhan unazidi kusogea,zaidi ya wafungwa 100 wanaoshikiliwa katika gereza la Guantanamo Bay wamekuwa wanaendelea na mgomo wao wa kula.Katika  taarifa za siri iliyovuja kutoka gerezani hapo,zaidi ya wafungwa 40 wamekuwa wakilishwa kwa kutumia mabavu,kwa maagizo ya jeshi la nchi hiyo

Katika video hii ya dakika 4 iliyoandaliwa na taasisi ya haki za binadamu,muongozaji wa filam Asif Kapadia na Yasin Bey ambae anajulikana zaidi kama Mos Def muigizaji na mwanamuziki  kutoka Marekani inaonesha jinsi wafungwa hao wanavyolazimishwa kula kwa kutumia nguvu.

Viongozi wa Jumuia ya Kiislam wameitaka serikali ya Rais Barack Obama kufikiria upya juu ya uamuzi huo wa kuwalisha wafungwa kwa kutumia mabavu,hasa wakati huu wa mfungo wa Ramadhan.

Serikali ya Marekani ilisema kuwa ili kuzuia dharura inayoweza kutokea hapo baadae au matatizo katika wajibu wao, itaheshimu funga ya mchana  kwa kuwalisha kwa nguvu wafungwa 45 wakati wa usiku.Lakini vikundi mbalimbali vya kiislam vimesema kuwa kuendelea kutumia mtindo huo wa kulazimisha kula wakati wa mwezi wa Ramadhan ni sawa na kutia chumvi kwenye kidonda.

"Katika imani yetu ni kosa kumlazimisha mtu kula wakati wowote ule,lakini inaumiza kuona mambo haya yanafanywa hata mwezi wa Ramadhan"Amenukuliwa akisema Ibrahim Hooper msemaji mkuu wa kikundi kinachosimamia haki za Waislam nchini Marekani.The Council On American-Islamic Relations(CAIR).

"(Ni kosa) sio tu kwa mujibu wa imani za kiislam bali pia kitendo hiki kinakiuka misingi ya haki za binadamu kimataifa na hata kanuni za kitabibu"

Dakta Azzam Tamimi kiongozi wa jamii ya Waislam nchini Uingereza amesema "Tunatarajia serikali ya Marekani italifikiria upya suala hili.Mwezi wa Ramadhan unavyoanza suala hili litazidi kuleta fedheha kwa watawala wa Marekani.Ni wakati muafaka Rais Obama afanye maamuzi ya kijasiri kulishughulikia katika njia ambayo itaeleweka na jumuia za kiislam duniani kote.

Wafungwa wanne kati ya 106 waliogoma kupinga kitendo cha serikali ya Marekani kuwaweka kizuizini muda mrefu bila ya kuwafungulia mashtaka, wamefungua kesi katika mahakama za huko Marekani, kupinga kulishwa kwa nguvu.

Kesi iliyofunguliwa katika mahakama ya Washington wiki iliyopita inapinga kulishwa kwa nguvu usiku kwani mgomaji anaweza asinywe maji na kuhatarisha maisha ya alielishwa kwa nguvu.

Katika kuadhimisha mwanzo wa mwezi mtukufu,kikundi cha Haki za Binadamu kimetuma video maalum kwa gazeti la The Guardian la Uingereza.

Ndani ya video hiyo Repa na Muigizaji maarufu wa Marekani Mos Def ambae alisilimu na sasa anaitwa Yasin Bey anaonekana kama mfungwa akiingia kwenye chumba maalum cha Guantanamo Bay kwa ajili ya kwenda kulishwa na madaktari ambao wanatumia mirija ya kulishia wagonjwa mahututi.

MosDef katika video hii anaonesha taabu wanayoipata wafungwa wanaopitia zoezi hili la kulishwa kwa nguvu.

Nyota huyo wa filam za kimarekani,anasema alijitolea kukubali kuingizwa mirija hiyo, kama inavyoonekana, kwa kushirikiana na madaktari wawili ambao nao walijitolea kukamilisha igizo hilo.

Video hiyo inayodumu kwa dakika nne inajaribu kutoa taswira halisi ya kinachotokea ndani ya gereza hilo lililopo kisiwani, katika bahari ya Atlantiki jirani na nchi ya Cuba,kufuatia taarifa za siri ya kufanyika kwa zoezi hilo kuvuja kwa televisheni ya al-Jazeera.

Katika nyaraka za kijeshi zilizovuja kutoka gerezani hapo na kutumwa kwa al-Jazeera ambayo ina kichwa cha habari`Medical management Standard Operating Procedure `inafafanua kuwa ili mfungwa aitwe mgomaji,anatakiwa awe hajala angalau milo tisa na awe amepungua uzito kwa asilimia 85 ya uzito wake wa kawaida.

Iwapo mfungwa analazimika kulishwa kwa nguvu,madaktari wanajeshi walio ndani ya gereza hilo watamfunga minyororo na mdomoni atawekewa kifaa maalum katakachomdhibiti mfungwa huyo asing`ate au kutema mate.Na baada ya hapo,mirija ya chakula huzamishwa tumboni kwa kupitia matundu ya pua.

Zoezi hili huchukua takriban dakika 20 hadi 30,lakini mfungwa analazimika kubaki kwenye kiti huku kafungwa,kwa masaa hadi mawili hadi atakapopigwa X-Ray kifuani ili kufahamu iwapo chakula kimetua tumboni mwa mfungwa.

Baada ya hapo mfungwa huku akiwa na minyororo anapelekwa kwenye chumba kidogo `kikavu`ambako ataendelea kuchungwa na mlinzi kwa saa nzima ili asitapike au kujaribu kujitapisha.Endapo atatapika,anarudishwa tena kwenye kiti kuanza tena zoezi la kumlisha.

Na endapo mfungwa atang`ata mrija wa chakula,madaktari watakibana kicwa chake bila kuachia hadi pale mfungwa atakapo legeza mdomo wake

Makundi ya waumini wa dini zingine pia wamelaani zoezi hilo.Mwezi uliopita mchungaji Richard Pates mwenyekiti wa Kamati ya Sheria za Kimataifa na Amani katika Muungano wa Wachungaji wa Kikatoliki nchini Marekani,alimuandikia barua Waziri wa Ulinzi wa Marekani Chuck Hagel kumkumbushia malalamiko ya  Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu dhidi ya kitendo cha kuwalisha wafungwa kwa kutumia mabavu

Sehemu ya barua hiyo inasema;"Badala ya kutumia mbinu hizo,kwanza taifa letu lifanye kila liwezalo kushughulikia adha inayopelekea mgomo huo kufanyika" 

Read more...

Monday, June 25, 2012

BOMB ATTACK AS PEOPLE WATCHING ENGLAND VS ITALY IN MOMBASA

0 comments
An attack victim being helped at the Coast General Hospital in Mombasa

One person was killed and several others injured in a grenade attack in a bar and restaurant in Mishomoroni estate in Mombasa, Kenya on Sunday night.
The attack occurred at around 10p.m. at the so called Jericho Beer Garden in the sprawling Mombasa estate.The dead man and the injured were at the outer section of the bar dancing to the music when the explosion occurred in three successive rounds.

The inner section of the pub was full of customers who had gathered to watch the European championships football match between England and Italy.
Police in Kenya said one person died, but St John Ambulance personnel who helped with rescue efforts put the number of fatalities at three. 

Security Officers helping an attack victim
This happened one day after US Embassy issued warning of an imminent terror attack on Mombasa.

Witnesses said they heard three loud explosions followed by screams.The scene was littered with debris of broken bottles and crates of beer.Police immediately cordoned off the area marking it as a crime scene and picked the body of the young man who was killed in the explosion.

A witness Mr Emmanuel Omondi said he was in the pub and had escorted a friend who was leaving and had just walked a few steps away when he heard the explosions.
“At first I thought it was the transformer which had blown up because it has been having problems. But immediately thereafter I heard a second blast and then a third one,” he narrated.

He said the man who died in the explosions was one of those who were on the dance floor.
He and other customers who escaped unhurt helped carry some of the injured to `matatus`(local passenger buses) that rushed them to hospital before the St John Ambulance team arrived.

Security Officers arrive at the scene
Provincial Police boss Aggrey Adoli arrived at the scene with a team from the Anti-Terrorism, Police and Criminal Investigations Department officers and helped seal off the area.

A nine year old boy was among the people injured. , some with serious injuries.
Mr Adoli could not confirm whether it was a terrorist attack and said police could not link it to the American alert since it targeted locals and not American citizens.
He told Coast province residents not to panic saying the security situation was not alarming and was still in control.
 According to reports this morning, Anti -Terror Police officers have one suspect in custody connected to last night attack.  Coast PPO Aggrey Adoli said preliminary investigations indicate that they were three explosions at the scene and heavy gun shots.
Some of attack victims at Coast General Hospital in Mombasa
  

 At least 28 victims of the attack were taken to the Coast Provincial General Hospital with one person admitted in the ICU. Nurse incharge, Stella Ndivo says five were treated and discharged while others still admitted sustained bullet and soft tissue injuries, among them a 9 year old boy.
 Last week,Kenyan police arrested two Iranians after they seized chemicals they suspected were going to be used to make explosives in Mombasa.
 Police arrested the Iranians on Wednesday of last week in Nairobi. On the same day, police impounded a container in Mombasa originating from Iraq and suspected to be carrying explosives.


On the following day, police flew one of the suspects to Mombasa, where he led police to recover 15 kg of powder, which security experts took to their laboratory for testing.

YOU MAY RELATE TO THIS:
Read more...

Friday, June 22, 2012

KENYAN POLICE SEIZE INBOUND EXPLOSIVE SHIPMENTS IN MOMBASA

0 comments

Port of Mombasa in Kenya
According to Reuters, Kenyan police had arrested two Iranians after they seized chemicals they suspected were going to be used to make explosives in Mombasa, which has been hit by a series of attacks.

The port city, the capital Nairobi and other parts of Kenya have suffered a series of grenade attacks since Kenya sent troops into Somalia last year to try to crush al Shabaab insurgents it blames for a surge in violence and kidnappings threatening tourism in east Africa's biggest economy.

Police arrested the Iranians on Wednesday in Nairobi. On the same day, police impounded a container in Mombasa originating from Iraq and suspected to be carrying explosives.

On Thursday, police flew one of the suspects to Mombasa, where he led police to recover 15 kg of powder, which security experts took to their laboratory for testing.

"They are cooperating well. They are giving us key information that might help us reduce terrorist attacks in the country," Ambrose Munyasia, a senior police officer at the Coast region told Reuters.
"We want to find out whether these substances are linked to any terror groups, including al Shabaab, al Qaeda and any other group," Aggrey Adoli, Coast provincial police officer, added.

Francis Kimemia, Kenya's acting head of civil service who was in Mombasa, said the government had sought the help of international agencies such the FBI and Interpol in helping deal with security threats.
"We have been working with them in terms of identifying criminals. We cannot fight terrorism alone. You have to work with other partners and other state organs," he said.

In the most recent attack, a bomb exploded in a trading center in the heart of Nairobi in late May, wounding more than 30 people. One person later died from their injuries.
Gunmen also detonated grenades outside a nightclub in Mombasa in May, killing one person and wounding several others.

Al Shabaab seeks to impose a strict version of sharia, Islamic law. The group emerged as a force in 2006 as part of a movement that pushed U.S.-backed warlords out of Somalia's capital, Mogadishu.
At present it also has hundreds of foreign fighters in its ranks.
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797