Pages

 

Friday, July 12, 2013

MAMA KUTOKA KENYA ASABABISHA BINTI MFALME WA SAUDIA KUKAMATWA MAREKANI

0 comments
Picha kutoka kwenye jalada la kesi iliyotolewa na Idara ya Polisi,ikimuonesha Meshael Alayban
Mama mmoja aliyetajwa  kuwa mwana mfalme kutoka Saudi Arabia amekamatwa katika jimbo la Carlifonia nchini Marekani kwa tuhuma za kushiriki biashara ya kuuza watu.
Meshael Alayban, 42, anakabiliwa na mashtaka ya kumlazimisha mama mmoja kutoka Kenya kufanya kazi kwa zaidi ya masaa kumi na sita kila siku, na kumlipa kiasi kidogo cha pesa kuliko walivyokuwa wameafikiana.
Maafisa wa serikali wa wa eneo hilo, wamesema kuwa Bi Alayban alichukua paspoti  ya mama huyo, hatua iliyomfanya atoroke.
Mawakili wa binti mfalme huyo wamesema kuwa kesi hiyo imesababishwa namzozo kuhusu hali ya utendaaji kazi.
Novemba mwaka uliopita, wapiga kura katika jimbo la Carlifonia, waliidhinisha sheria kali dhidi ya watu watakaopatikana na hatia ya kuhusika na ulanguzi wa watu.


Saudi princess charged in Calif. with human trafficking
Binti Mfalme Meshael Alayban (Kulia) akimsikiliza mkalimani wakati alipofikishwa mahakamani jana huko Santa Ana California
Iwapo atapatikana na hatia, Bi Alayban, huenda akahukumiwa kifungo cha miaka kumi na miwili gerezani, adhabau ambayo ni asilimia mia moja zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali, kabla ya wapiga kura kuidhinisha mabadiliko ya sheria hiyo..Waendesha mashtaka wanasema Bi Alayban, ni mmoja wa wake sita wa Mwana Mfalme Abdulrahman bin Nasser bin Abdulaziz al-Saud, mmoja wa watoto wa kiume wa familia ya kifalme nchini Saudi Arabia.

Mama aliezua sakata hilo  Mkenya ambaye jina lake halijatolewa, aliajiriwa na Bi Alayban miaka miwili iliyopita, baada ya kuandikiana makubaliano na shirika moja la kutoa ajira nchini Saudia.
Mama huyo alihaidiwa kulipwa dola elfu moja mia sita kila mwezi na kuwa atafanya kazi masaa manane kila siku kwa siku tano.
Lakini, Bi Alayban amekuwa akimlipa dola mia mbili ishirini kila mwezi na kulazimishwa kufanya kazi kwa zaidi ya masaa kumi na sita kila siku.
Mama huyo kutoka Kenya vile vile amedai, kunyang`anywa paspoti yake ya kusafiria na alirudishiwa muda mfupi tu kabla ya wao kusafiri kwenda Carlifonia na Bi Alayban.
Akiwa Carlifonia, alilazimishwa kufanya kazi nyingi za nyumbani kwa familia nane zilizoishi katika vyumba vinne tofauti, ambako amedai alishikwa kama mateka .
Wakati alipofanikiwa kutoroka, alisimamisha basi moja na kwenda moja kwa moja hadi kituo cha polisi.
Bi Alayban alikamatwa siku ya Jumatano ya juzi na kufikishwa mahakamani jana.
Aliachiliwa huru kwa dhamani ya dola milioni tano na kuamriwa kurejesha pasi ya kusafiria ya mama huyo kutoka Kenya.
Aidha Bi Alayban sasa atavalia chombo maalum ambacho kitatoa maelezo ya mahala aliko na hataruhusiwa kuondoka Marekani hadi kesi hiyo itakapokamilika.
 Waendesha Mashtaka walitaka jaji kumuachilia kwa dhamani ya dola milioni Ishirini au anyimwe dhamana kwa kuwa yeye ni tajiri mkubwa na angeweza kutoroka

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797