Pages

 

Sunday, July 7, 2013

BEYONCE APATA MAMA WA KAMBO

0 comments
Wanamuziki Beyonce na Solange ambao ni mtu na dada wamepata mama wa kambo baada ya baba yao kufunga ndoa na mwanamke mwingine,kufuatia kuachana na mama yao mzazi akina Beyonce
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AP, Mathew Knowles,baba wa akina Beyonce,ambae pia alikuwa meneja wa Beyonce alifunga ndoa na rafiki yake wa kike,mwanamitindo Gena Charmaine Avery huko Houston Texas,mwishoni mwa wiki iliyopita.Mathew Knowles mwenye umri wa miaka 61 na Gena Avery mwenye umri wa miaka 48,walikuwa wameshachumbiana mwaka mmoja na nusu uliopita.Beyonce na Solange hawakuhudhuria harusi.
Mathew Knowles alitalakiana rasmi na mama mzazi wa akina Beyonce,Tina Knowles,mwaka 2011 baada ya mama huyo kufungua kesi ya kudai talaka mwaka 2009.Ndoa yao ilidumu kwa miaka 29.

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797