Pages

 

Saturday, July 13, 2013

BOMOA BOMOA:FAMILIA NZIMA YAJICHOMA MOTO MBELE YA OFISI ZA MANISPAA!

0 comments
Moshi ukiwa umezagaa angani mbele ya jengo la serikali muda mfupi baada ya tukio hilo
Watu watano wa familia moja wamejichoma moto mbele ya ofisi za serikali kwa kile walichodai kupinga mpango wa serikali kubomoa nyumba waliyokuwa wakiishi.

Tukio hilo la kutisha na kusikitisha limetokea magharibi mwa India katika mji wa Rajkot,ulioko katika jimbo la Gujarat na limehusisha mama,watoto wake wawili wa kiume na wake zao.

Hasumati Dalvani mama mwenye umri wa miaka 62,wanawe ,Bharat Masingh,40 na Girish Masingh,38 pamoja na wake zao Asha na Rekha,walijimiminia mafuta ya taa mwilini kabla ya kujilipua.

Familia hiyo imekuwa ikipambana kupinga mpango wa serikali kubomoa nyumba yao waliyoishi kwa miaka 35 sasa,baada ya wakazi wa eneo hilo kulalamika kuwa haikuwa salama.
Mmoja wa majeruhi waliojilipua akisaidiwa kupelekwa hospitali

Watu walioshuhusia tukio hilo walijaribu kuzima moto kwa kutumia vipande vya mapazia,lakini walikuwa wameshachelewa.Watoto  na wake zao walifariki baada ya kufikishwa kwenye Hospitali ya Umma ya Rajkot.

Msemaji wa Hospitali hiyo Dakta Sanjay Shah amesema kuwa majeruhi walifikishwa wakiwa wameungua asilimia 90 hadi 95 ya miili yao,walikuwa katika halimbaya sana.Madaktari walijaribu kuokoa maisha yao lakini ilishindikana.Mama mtu bado yuko hai lakini yuko katika hali mbaya sana

Katika hatua nyingine Meya wa jiji la Rajkot,wakati akitoa rambirambi kwa familia hiyo alisema Manispaa yake haikuwa na mpango wa kubomoa nyumba ya familia hiyo.

Polisi wa huko wamewadaka watu wengine wanne ambao wanadaiwa kuchochea tukio hilo la kujiua.Manispaa tayari imethibitisha kutoa  ya kiasi cha Rupia Milioni 2 na laki 5,sawa na wastani wa Shilingi milioni 66 za kitanzania kama fidia kwa familia hiyo

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797