Pages

 

Saturday, July 13, 2013

VITA UWANJA WA TAIFA JIONI YA LEO

0 comments
LEO, kuanzia saa 9 alasiri,Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, inatinga Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kucheza na wenzao, Uganda Cranes, kusaka nafasi ya kucheza Fainali za CHAN, African Nations Championship, zitakachezwa kuanzia Januari 10 hadi Februari 1, 2014 huko Afrika Kusini.

Mashindano haya yalianza kuchezwa huko Nchini Ivory Coast Mwaka 2009 na Tanzania ilishiriki Fainali hizo na yanahusisha Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wanaocheza Ligi za ndani ya Nchi zao pekee.
Wachezaji wanaocheza Soka nje ya Nchi zao hawaruhusiwi kushiriki.

KUMBUKUMBU:
CHAN 2009
Tanzania walishiriki Fainali za Kwanza za CHAN Mwaka 2009, wakiwa chini ya Kocha Marcio Maximo, huko Nchini Ivory Coast wakiwa Kundi A pamoja na Wenyeji Ivory Coast, Zambia na Senegal na kumaliza Nafasi ya 3.
Katika Mechi hizo za CHAN Tanzania ilifungwa na Senegal 1-0, kuifunga Ivory Coast 1-0 na kutoka sare 1-1 na Zambia.
AFCON 1980
Tanzania haijawahi kufuzu kucheza Fainali za AFCON tangu Mwaka 1980 walipocheza huko Nchini Nigeria, chini ya Kocha kutoka Poland Slawomir Wolk, wakiwa Kundi moja na Wenyeji Nigeria, Egypt na Ivory Coast ambako walifungwa Mechi ya kwanza 3-1 na Nigeria, 2-1 na Egypt na kutoka 1-1 na Ivory Coast.

Kikosi cha Uganda tayari kipo Nchini kikiwa na Kocha wao Sredojvic Micho na jana kwenye Mkutano wa Waandishi wa Habari Kocha huyo alisema Taifa Stars imekuwa ikifanya vizuri tangu iwe chini ya Kim, na itakuwa na Wachezaji tisa wa Kikosi cha Kwanza kinachocheza Mechi za Mchujo za Kombe la Dunia wakati kwa upande wake atakuwa na Wachezaji wawili tu.
Pia Kambi ya Uganda imekuwa ikilalamikia joto kali la Jiji la Dar es Salaam ambapo wao kwao wamezoea hali ya wastani wa Nyuzijoto 25 wakati wamekumbana na Joto la zaidi ya Nyuzijoto 30.
Kwenye Mechi ya leo Uganda Cranes wanatarajiwa kutumia Mfumo wa 4-3-3 kwa mujibu wa Mdau wao mmoja aliekuwepo wakati Timu hiyo ikifanya Mazoezo wa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

VIINGILIO:
-Sh. 5,000 kwa Viti vya rangi ya kijani [Viti 19,648]
-Sh. 7,000 Viti vya rangi ya bluu [Viti 17,045]
-Sh. 10,000 Viti vya rangi ya chungwa [Viti 11,897]
-Sh. 15,000 VIP C [Viti 4,060]
-Sh. 20,000 VIP B [Viti 4,160.]
-Sh. 30,000 VIP A [Viti 748]

TAHADHARI:
Washabiki wanakumbushwa kutonunua Tiketi mikononi mwa Watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua Tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.
++++++++++++++++++++++++++++++++
Nae Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen, alisema ni muhimu kwao kushinda Mechi hii ili kujiweka katika mazingira mazuri kwa ajili ya Marudiano lakini pia alisema Uganda ndiyo inayoongoza kwa Ubora wa Viwango vya FIFA katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, na hivyo ni changamoto kwao.
Kim Poulsen pia alisema Wachezaji wake tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya Mechi hiyo.
Hapo Jana, Rais wa TFF, Leodegar Tenga, aliitembelea Kambi ya Taifa Stars kwenye Hoteli ya Tansoma, Dar es Salaam na kuwapa moyo Wachezaji kwa kuwaambia kuwa kiwango walichoonesha kwenye Mechi zilizopita za Mchujo za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco na Ivory Coast kimetoa uhakika wa uwezo wao wa kushindana katika Mashindano yoyote, kwani tayari wameiva.
Rais Tenga, akiwahimiza Wachezaji kupigana kwa ajili ya Tanzania, alitamka: “Kiwango mlichoonyesha katika mechi hizo kila Mtanzania anayewafuatilia amekiona, hivyo hatuna shaka kuwa mtatuwakilisha vizuri kwenye mechi ya kesho dhidi ya Uganda.”

CHAN 2014
RATIBA
KANDA KASKAZINI
(Timu 2 zitafuzu)
05-07/07/13: Tunisia v Morocco
26-27/07/13: Morocco v Tunisia
Algeria v Libya - Imefutwa
Libya watacheza Fainali huko South Africa baada Algeria kujitoa.
KANDA MAGHARIBI A
(Timu 2 zitafuzu)
Raundi ya Awali
30/11/12-2/12/12 : Liberia 0-1 Mauritania; Guinea 0-0 Sierra Leone
14-16/12/12: Mauritania 2-1 Liberia; Sierra Leone 1-1 Guinea
Mauritania wamepita Jumala ya Bao 3-1
Guinea wamepita kwa Magoli ya Ugenini
Raundi ya 1
05-07/07/13: Senegal v Mauritania; Mali v Guinea
26-27/07/13 : Mauritania v Senegal; Guinea v Mali
KANDA MAGHARIBI B
(Timu 3 zitafuzu)
Raundi ya Awali
30/11-2/12/12/12: Burkina Faso 2-1 Togo
14-16/12/12: Togo 0-1 Burkina Faso
Burkina Faso wamepita Jumla ya Bao 3-1
Raundi ya 1
05-07/07/13: Benin v Ghana; Nigeria v Ivory Coast; Burkina Faso v Niger
26-27/07/13: Ghana v Benin; Ivory Coast v Nigeria; Niger v Burkina Faso
KANDA KATI
(Timu 3 zitafuzu)
Raundi ya Awali
Central African Republic v Congo - cancelled
Congo inasonga baada ya kujitoa Central African Republic
Raundi ya 1
05-07/07/13: Cameroon v Gabon; DR Congo v Congo
26-27/07/13: Gabon v Cameroon; Congo v DR Congo
Washindi watatinga Fainali
Mchujo Raundi ya 1
Watakaofungwa Mechi za Raundi ya 1 watapambana kati ya Tarehe 26-28/07/13 na 09-11/08/13 na Washindi wawili kusonga Fainali.
KANDA KATI MASHARIKI
(Timu 3 zitafuzu)
Raundi ya Awali
14-16/12/12: Burundi 1-0 Kenya; Eritrea v Ethiopia ( Ethiopia wamesonga baada Eritrea kujitoa)
06/01/13: Kenya 0-0 Burundi (Burundi wamesonga Jumla ya Bao 1-0)
Raundi ya 1
05-07/07/13: Burundi v Sudan
12-13/07/13: Ethiopia v Rwanda; Tanzania v Uganda
26-27/07/13: Sudan v Burundi, Rwanda v Ethiopia, Uganda v Tanzania
KANDA KUSINI
(Timu 3 zitafuzu pamoja na Wenyeji South Africa)
Raundi ya Awali
30/11-2/12/12 : Mauritius 2-0 Comoros
14-16/12/12: Comoros 0-0 Mauritius
Mauritius yasonga Jumla ya Bao 2-0
Raundi ya 1
23/06/2013: Swaziland 0-1 Angola
29/06/2013: Angola 1-0 Swaziland
Angola yasonga Jumla ya Bao 2-0
26-7/07/13: Mauritius v Zimbabwe; Mozambique v Namibia; Botswana v Zambia
02-04/08/13: Zimbabwe v Mauritius, Namibia v Mozambique; Zambia v Botswana
Raundi ya 2
26-28/07/13 : Mechi za Kwanza
09-11/08/13: Mechi za Pili
Raundi ya 2
Washindi wawili wa Raundi ya 2 wanaungana na Wenyeji South Africa kucheza Fainali.
Mshindi Mauritius/Zimbabwe v Mshindi Mozambique/Namibia
Botswana/Zambia v Angola

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797