Pages

 

Saturday, July 6, 2013

REFA NA MCHEZAJI WAUAWA KINYAMA BRAZIL

0 comments
Baada ya kwisha kwa pilikapilika za Kombe la Mabara nchini Brazil,sambamba na vurugu mitaani,huku nchi hiyo kubwa ya Amerika ya Kusini ikikabiliwa na changamoto nyingine ya kuwa mwenyeji wa mashindano yajayo ya Kombe la Dunia 2014,nchi hiyo imeingia kwenye taswira mbaya-kwa mara nyingine-baada ya kuripotiwa kutokea mauaji ya kutisha ya mchezaji na mwamuzi katika mechi mjini Maranhao ,kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Taarifa zinasema kuwa Otávio Jordão da Silva ambae alikuwa mwamuzi wa mechi hiyo na ambae alikuwa akishambuliwa kwa matusi muda wote wa mechi, alichomoa kisu baada kumaliza mechi na kisha kumchoma nacho mchezaji mmoja mwenye umri wa miaka 31 aitwae Josemir Santos na kumsababishia majeraha ambayo hatimae yalisababisha kifo chake.

Ndugu na marafiki wa mchezaji huyo walipogundua kuwa Santos ameshafariki,walilipiza kisasi kwa kumchoma kisu mwamuzi huyo,ambae baadae kundi la watu liliendelea kumpiga,na kummalizia kwa kumkata vipande vipande na kunyofoa kichwa chake kabla hawajakichomeka kwenye mti na kukiweka kama bendera katikati ya uwanja.
Hakuna taarifa zaidi juu ya tukio hilo, lakini picha zilizowekwa mtandaoni na mtandao wa 101GREAT GOALS zimethibitisha kutokea kwa tukio hilo

Marehemu Josemir Santos Abreu

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797