Pages

 

Friday, July 5, 2013

FACEBOOK YAZINDUA HASHTAG

0 comments
Kwa wale watumiaji wa Twitter nadhani wanaelewa inapotajwa HASHTAG...neno ambalo kwa mitandao inaiyotumia huwa ni kama neno linaloweza kuwaunganisha moja kwa moja kuingia kwenye topic (jambo linaloongelewa) inayohusiana nayo ambayo ipo hewani inazungumziwa...ili iwe HASHTAG neno lenyewe lazima lianze na alama (symbol) # na bila kuacha nafasi linafuata neno lenyewe;mfano HASHTAG hii #saidnuhublog...kwahiyo watu wote ambao hujadili Said Nuhu Blog watatumia HASHTAG hii ili kumuunganisha na wengine wanaotaka kuchangia ,huo ni mfano tu...na yeyote ambae yuko mtandaoni akikutana na alama-neno hii,akaibonyeza, basi mtandao utampeleka moja kwa moja kwenye mjadala husika.aidha ataangalia mjadala unavyokwenda au anaweza kuchangia anachojisikia.
Kampuni ya FACEBOOK imezindua matumizi ya HASHTAG kwa ajili ya watumiaji wake wote ikifuata nyayo za kampuni ya Twitter...hatua hii ni jitihada za kampuni hiyo kuboresha huduma zake ili isiachwe nyuma na makampuni mengine,lakini wachunguzi wa mambo ya mitandao ya kijamii wanaona kuwa wazo hili litakuwa na faida zaidi kwa watu wanaotangaza biashara zao kupitia mitandao ya kijamii

CHANZO:THE UNDERCOVER RECRUITER

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797