Pages

 

Sunday, July 7, 2013

MJUE MWANAMKE MWENYE KUCHA NDEFU KULIKO WOTE DUNIANI

0 comments
Anaitwa Chris Walton na pia kimuziki anaitwa `The Duchess` ndie alieingia kwenye kitabu cha rekodi za dunia cha Guinness Book of World Record kama mwanamke mwenye kucha ndefu kuliko wote duniani kwa sasa.
Inasemwa kuwa unapokutana na mwanadada huyo hakuna jinsi bali ni kumwangalia kwa mshangao,lakini angalau kucha zake ni safi na zinang`arishwa kwa dawa maalum
Anaweza akachukuliwa kama mchafu kwa kuwa hajazikata kwa miaka 20 lakini mrembo huyo mwenyeji wa Las Vegas kwa Obama,amewavuta watu wa Guinness World  Book of Record.The Duchess ni muimbaji anaechipukia kwenye fani kwa sasa.Awali mwanamama Lee Redmond ndie aliekuwa  akiongoza kwa kushikilia rekodi ya kuwa na kucha ndefu kuliko wote ambazo zilifikia urefu wa futi 28 kabla hazijavunjika katika ajali ya gari mwaka 2011.Kabla ya ajali ,Bi Redmond hakuwahi kukata kucha za vidole vyake vya mkononi tangu mwaka 1979!
Bibi Lee Redmond


0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797