Pages

 

Wednesday, July 17, 2013

USHINDI WA ARSENAL WAFANYIWA PROPAGANDA ZA KISIASA INDONESIA

0 comments
Sege Gnaby wa Arsenal akikwepa daruga la mchezaji wa Indonesia, Roby
Mgombea urais katika uchaguzi wa Rais wa 2014 kupitia Chama cha Great Indonesia Movement Party (Gerindra) Jenerali mstahafu Prabowo Subianto ameutumia mchezo kati ya timu ya taifa ya nchi hiyo na Arsenal kuishambulia serikali iliyo madarakani katika hotuba ya mkutano wa Kampeni za uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo wa mwaka 2014

Baada ya timu ya taifa ya Indonesia kupokea kipigo cha goili 7-0 kutoka Gunners mgombea Prabowo aliilaumu serikali kwa kutoisimamia vizuri timu hiyo  na kuahidi iwapo ataingia madarakani kama rais wa Indonesia atahakikisha kikosi cha timu ya taifa kinafanya vizuri katika mechi zake

"
 Iweje hata timu yetu ya taifa inashindwa kwenye mechi na wachezaji 11 wa ngazi ya klabu.Tutahakikisha tunalipa umuhimu wa pekee suala zima la timu ya taifa.Kwa hiyo ninachofikiri ni kwamba matatizo haya yanasababishwa na udhaifu katika uendeshaji,na uwezo mdogo wa kufikiri.Matatizo katika uongozi.Tunataka Indonesia iwe na timu ya taifa iliyo imara"
 Jenerali Prabowo ambaye aliwahi kuwa askari wa kikosi maalum,aliwahi kuwania kiti cha umakamu wa rais 2009 ambapo alibwagwa na mpinzani wake Megawati Sukamoputri.Ni mmoja kati ya wagombea wanaopewa nafasi kubwa ya kuingia ikulu ya nchi hiyo ya mashariki ya mbali 2014

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797