Pages

 

Sunday, July 7, 2013

USAIN BOLT KUCHEZEA MANCHESTER UNITED!

0 comments
Usain Bolt
Ile ndoto ya gwiji wa mashindano ya kukimbia mita 200, Usain Bolt wa Jamaica,kuchezea timu ya Manchester United,  imeonekana kutimia baada ya kujumuishwa kuwa kati ya wachezaji watakaochezea timu hiyo katika mechi maalum ya kumuenzi  mlinzi mahiri wa timu hiyo,Rio Ferdinand, mwezi Agosti.
Mwanariadha huyo, ambaye inasemekana ndie binadamu mwenye kasi kuliko wote duniani,atakuwepo katika kikosi kitakachomenyana na timu ya Seville kutoka Hispania,katika dimba la Old Trafford, siku ya tarehe 9 mwezi ujao.
"Matamanio yake sasa yatatimia,Bolt atakuwemo kwenye kikosi na kucheza sambamba na Rio.Utakuwa mchezo wa aina yake,kwa kuwa watu watapendeza kuona kama kasi yake inaweza kwenda na uwezo wake wa kumiliki mpira."Kimeongea chanzo cha ndani ya klabu hiyo.
Uteuzi wa Bolt kwenye kikosi hicho unatarajiwa kutangazwa wiki ijayo.

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797