Pages

 

Monday, April 23, 2012

MAELFU HUENDA WAKAKOSA INTERNET IFIKAPO JULAI

0 comments

Kwa mujibu wa habari nilizozinyaka kitu ambacho watumiaji wengi wa kompyuta duniani hawakuwa wanakijua kuwa wezi wa kimataifa wanaotutumia mitandao ya kompyuta (international hackers)waliingiza tangazo feki kwenye mitandao duniani kwa lengo la kudhibiti mienendo ya kompyuta dunia nzima.Baada ya hujuma hiyo, kwa kasi ya kushangaza, Shirika la Upelelezi la Marekani, FBI, kwa kutumia kompyuta za serikali ya nchi hiyo, lilijanzisha mfumo salama wa mtandao wa dharura kuzinusuru kompyuta zilizoshambuliwa duniani kote zisijifunge…lakini
ifikapo Julai mfumo huo utalazimika kuzimwa.

FBI wanawashauri watumiaji wa kompyuta kutembelea tovuti ya http://www.dcwg.org, tovuti ambayo ni ya washirika wao katika mambo ya usalama wa kompyuta,nao watawafahamisha watumiaji iwapo kompyuta zao zimeshambuliwa au la na jinsi ya kupambana na tatizo hilo. Inasemekana kuwa wale wote ambao kompyuta zao zimeshambuliwa hawatakuwa hewani  baada ya Julai 9

Watumiaji wengi hawajui kuwa  kompyuta zao zimeshashambuliwa,ingawaje virus hatari vimeshaanza kupunguza kasi ya kuperuzi mitandao na pia kuharibu kinga  (antivirus) kwenye kompyuta zao,na hivyo kuwa hatarini kupatwa na matatizo

Mwezi Novemba mwaka jana FBI kwa kushirikiana na mamlaka zingine za usalama,walikuwa wanajiandaa kuusambaratisha mzingo mkubwa wa wezi wa mitandaoni ambao ulikuwa unaendesha wizi kwa kutumia matangazo ya internet(internet ad) wakitumia lundo la kompyuta zenye virus.

“Tuligundua kuwa tunaweza kuja kupata matatizo kidogo kwa sababu tungesema tukamate mtandao mzima wa hawa waharifu na kuwasweka jela…baadhi watumiaji wangekosa huduma ya internet”alisema Bw. Tom Grasso msimamizi maalum kutoka FBI.”Mtumiaji wa kawaida angeweza kufungua Internet Explorer na kukuta `page not found` na kudhani kuwa ni matatizo tu ya network”

Usiku ule walipovamia na kuwakamata,shirika hilo la upelelezi lilimleta Paul Vixie Mwenyekiti na mwanzilishi wa Kituo Kinachounganisha Mifumo ya Internet(Internet Systems Consortium) ili aunde server mbili za internet kuchukua nafasi ya server ambazo zilikuwa zinashambulia kompyuta za watumiaji duniani ambazo tayari zilikamatwa na kujazwa katika lori

Maafisa wa serikali mwanzoni walikubaliana kuziacha server za serikali kuendelea kusaidia  hadi mwezi Machi ili kuwapa muda watumiaji kusafisha kompyuta zao, lakini ilionekana kuwa muda huo ni mfupi.Jaji wa New York aliamuru server hizo  za serikali ziendelee kutoa huduma hadi mwezi Julai.

“Sasa tunawaachia uwanja watu wa habari muwafahamishe watu juu ya tatizo lililopo…na ni juu ya watumiaji iwapo watapenda kuzikagua  kompyuta zao”alisema Grasso

HIVI NDIVYO ILIVOTOKEA

Wezi hao wa kwenye mtandao wa kompyuta wameshambulia kompyuta zipatazo 570 000 dunia nzima.Kutokana na udhaifu wa mfumo wa uendeshaji wa Microsoft Windows(Microsoft Windows operating sytem) waliweza kupenyeza virus kwenye kompyuta za watumiaji.Kitendo hicho kiliondoa uwezo wa  programme za kuboresha kinga(antivirus updates) na hatimaye kubadili mwenendo wa kompyuta zinavyofasiri anuani ndani kwa ndani, kwenye mfumo wa internet unaotafsiri majina (Domain Name System)
Mfumo huu wa DNS ni mjumuiko wa server ambazo kazi yake ni kutafsiri anuani za mtandao kwa mfano  http://saidnuhu.blogspot.com/ na kadhalika.Iwapo kompyuta yako ilishambuliwa, jua kuwa wezi hao walipenyeza programme zao na kuiongoza kuelekea kwenye kitafsirio (DNS) kilicho kwenye server zaoHii imewawawezesha wezi hao kuzielekeza kompyuta  kwenye aina yoyote ya website za uhalifu.

Watu hao wamevuna mapato kutokana na matangazo ya biashara (advertisements) mbalimbali ambayo yanatokea kwenye website za kizushi ambazo watumiaji wamekuwa wakishawishiwa kuzitembelea.Wameingiza kiasi cha dola za kimarekani milioni 14 kulingana na maelezo ya FBI na pia wamewafanya maelfu ya watumiaji kutumia internet kwa kuzitegemea server za wahalifu hao bila kujua

Siku ambayo FBI na mamlaka zingine za usalama zilipowakamata watu sita wenye asili ya  Estonia mwezi November, shirika hilo liliamua kutumia server  salama za Bw. Vixie ili kuziba nafasi za server za wahalifu.Kufunga na kuziendesha sever mbili kwa miezi minane kumeighali serikali ya Marekani kiasi cha dola 87 000

Ni vigumu kujua idadi  sahihi ya kompyuta zilizoathirika ,lakini FBI wanaamini kuwa hadi siku walipowakamata waliohusika na uhalifu huo, kiasi cha anuani 568 000  za   mitandao ya kompyuta zilikuwa zikitumia server za wahalifu hao

Ikiwa ni miezi mitano sasa imeshapita FBI wanakisia kuwa kiwango cha watumiaji walioathirika kimeshuka hadi 360 000,huku Marekani yenyewe ikiwa na idadi kubwa ya  watumiaji  85 000.Nchi zingine kila moja zina watumiaji waliathirika wasiopungua 25 000 ikwemo Italia,India,,Uingereza, na Ujerumani.Kiasi kidogo cha watumiaji walioathirika kipo Hispania,Ufaransa,Canada,China na Mexico

Vixie amesema ni dhahiri kuwa wengi wa watumiaji walioathirika na hili tatizo ni wale wa majumbani na sio makampuni,kwa kuwa yana wataalam wao wanaokagua kompyuta kila mara

Maofisa wa FBI wamesema kuwa wameunda mfumo wa kompyuta usiokuwa wa kawaida  ili kuepusha mtandao wa kompyuta za serikali usiingiliane na mtandao wa internet au kompyuta za watumiaji binafsi na ingawaje ni mara ya kwanza FBI kuutumia mfumo huo,haitakuwa mara ya mwisho kuutumia.

“Hii ndio hatua tutakayochukua hata hapo baadae”,Eric Strom, mkuu wa kitengo cha FBI cha mambo ya kompyuta  alisema.”Labda kuwe na mabadiliko ya kisheria ndani na nje ya Marekani,lakini ili tushughulikie matatizo kama haya kwa haraka zaidi ni lazima tutumie njia hizi,kufuatilia na kuangalia njia zote,katika upelelezi wa mambo kama haya”

Alisema sasa hivi kila mara FBI wanapokaribia kumaliza kesi inayohusiana na kompyuta “inafikia hatua fulani tunajiuliza sasa tufanyaje,tufanye nini ili tuusafishe mfumo wote bila ya kuzua tatizo lingine kubwa zaidi ya hili”











0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797