Pages

 

Monday, May 7, 2012

MAHAKAMA YAKATAA KUTAMBUA CHETI CHA KUZALIWA CHA LULU

0 comments

Msanii wa kike wa filamu nchini Elizabeth Michael leo alifikishwa tena katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Dar Es Salaam kwa ajili ya kusomewa kesi mauaji inayomkabili.Elizabeth anahusishwa na kifo cha msanii mwenzake Steven Kanumba,baada ya msanii huyo kafariki ghafla wakiwa pamoja usiku wa  Aprili 7 mwaka huu

 Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Bi.Augustina Mmbado,Elizabeth alisomewa tena mashtaka na hakutakiwa kujibu chochote kuhusiana na kesi hiyo.Hata hivyo mawakili wanne wanao mtetea Elizabeth waliomba udhuru ambapo wakili Keneth Fungamtama kwa niaba ya wenzake,aliiomba mahakama itoe udhuru kwa mshtakiwa kesi ikasikilizwe kwenye mahakama ya watoto,kwani mshtakiwa bado ana umri mdogo ambao hauruhusu kushtakiwa kwenye mahakama za kawaida, huku akikabidhi cheti cha kuzaliwa cha mshitakiwa kikionesha kuwa ana umri wa miaka 17, na pia kesi yake isikilizwe INCAMERA,(faragha)ombi ambalo mahakama  ililikataa kwa kutumia kifungu namba 198 cha sheria,kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.Pia mahakama ilikataa kutambua cheti cha kuzaliwa cha mshitakiwa kwa madai kuwa cheti kiliandikwa jina la Diana, jina ambalo mshitakiwa hakuwahi kulitumia.Elizabeth anatetewa na mawakili Keneth Fungamtama,Fulgence Massawe,Peter Kibatara na Jackline De Melo.

 Kesi imehairishwa tena hadi  Mei 21 itakapotajwa tena na Elizabeth amerudisha rumande  

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797