Pages

 

Monday, May 7, 2012

BINT ALBINO WA MIAKA 15 ATEKWA NA KUUAWA KINYAMA NCHINI BURUNDI

0 comments
Kikundi cha watu wenye silaha wamemteka,kumuua binti wa albino mwenye umri wa miaka 15 na kisha kuukata kata mwili wake nchini Burundi ikiwa ni tukio la 18 ndani ya miaka minne kutokea nchini humo

Watu wenye ualbino,hali ya kibaiolojia ambayo huzuia kabisa utengenezwaji wa rangi ya ngozi,wamekuwa wakibaguliwa na baadhi ya jamii katika nchi kadhaa za kiafrika

Kutokana na imani za kishirikina zilizotawala katika jamii hizo kwamba albino wana uwezo wa ziada,hupelekea watu hao kuuawa na kisha viungo vyao kuuzwa kwa waganga wa kienyeji

Katika tukio la majuzi kundi la watu waliobeba mikuki,magobole na mapanga walivamia nyumba moja katika eneo lililo karibu na mji mkuu Bujumbura na kumteka msichana mwenye umri wa miaka 15

Kwa mujibu wa maafisa wa serikali,watu hao walimuua binti huyo na kisha kukata mikono na miguu na kutokomea navyo.

Idadi ya maalbino waliouawa kwa staili hiyo imefikia 18 tangu mwaka 2008 na kasi ya mauaji hayo ilpungua baada ya mwezi Agosti 2009 ambapo watu wanane walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya mauaji ya albino

Lakini Kassim Kazungu ambae ni Rais wa kikundi kinachotetea maalbino cha Albinos Sans Frontieres anasema kuwa serikali ya nchi hiyo imeshindwa kulinda maisha ya maalbino nchini humo kwani kila mtu aliehukumiwa kifungo kwa mauaji ya albino ametoroka gerezani.

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797