Pages

 
Showing posts with label jamii. Show all posts
Showing posts with label jamii. Show all posts

Friday, August 2, 2013

HIVI NDIVYO AKINA MASOGANGE WALIVYOPITA UWANJA WA NDEGE DAR

0 comments

CHANZO CHA HABARI:GAZETI LA MTANZANIA
TUKIO la wasichana wawili wa Tanzania waliokamatwa na dawa za kulevya Afrika Kusini, limechukua sura mpya baada ya kujulikana kwamba, siku ambayo watuhumiwa hao walisafiri kupitia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam, mbwa wanaohakiki usalama wa mizigo hawakuwapo. 
 
Chanzo chetu cha habari kiliiambia MTAZANIA, kwamba pamoja na uwepo wa kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya uwanjani hapo, kitengo hicho kina kasoro kadhaa zinazotakiwa kurekebishwa.

“Mimi niko hapa, najua kila kinachoendelea, nakwambia siku hiyo ambayo wale wasichana walipitisha dawa hizo, hapakuwa na mbwa wa kunusa, naamini kama mbwa wangek
uwapo, lazima siri ingefichuka,” kilisema chanzo hicho.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, katika viwanja vya ndege kuna vitengo vingi vikiwamo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Idara ya Uhamiaji na askari polisi ambapo kila kitengo kina majukumu yake.
“Kwa hiyo, ninachotaka kukwambia ni kwamba, jukumu la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) ambayo baadhi ya watu wanasema inachangia kupitisha dawa za kulevya, haihusiki kwa sababu jukumu lake kuu ni kuzuia vitu vinavyohatarisha usalama wa ndege na abiria.

“Kuhusu uzito wa mizigo na malipo, hilo linafanywa na shirika la ndege husika na baada ya shughuli zote kufanyika, mizigo hukaguliwa kwa mashine na kunuswa na mbwa kabla ya safari kuanza,” kilisema chanzo hicho.

Pamoja na hayo, utata mwingine juu ya hali ya usalama na uwajibikaji wa watumishi wa uwanja huo wa ndege umejionyesha kupitia nyaraka zilizopatikana.

Uchunguzi uliofanywa na MTANZANIA kwa siku kadhaa sasa, umebaini dawa hizo kilo 150 aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya Sh bilioni 6.8 zilizokamatwa na wasichana hao, zilimhusisha pia mshirika wao kibiashara aliyefahamika kwa jina la Mangunga ambaye majina yake matatu tunayo.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, wasichana hao, Agness Gerald (25) na Melisa Edward (24) walisafiri ndege moja na Mangunga wakitoka Dar es Salaam kwenda Afrika Kusini.

Nyaraka hizo zinaonyesha kwamba, wakati Manguga na wasichana hao wakisafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA), namba SA 189, Julai 5 mwaka huu, walikuwa na mabegi tisa.

Nyaraka hizo zinaonyesha jina la Agness Gerald, kwamba ndiye aliyelipia mabegi hayo, lakini katika sehemu inayotakiwa kuandikwa barua pepe, imeandikwa barua pepe ya Mangunga inayosomeka, Nmangunga@Gmail.com.

Mabegi hayo, yalikuwa na kilo 150 za dawa za kulevya lakini kila mmoja alitakiwa kusafiri na kifurushi cha kilo 20 na hivyo kutakiwa kuwa na kilo 60 wote kwa pamoja.

Baada ya kila mmoja kuwa na kilo 20, zilibaki kilo 90 ambazo walizilipia Dola za Marekani 94 badala ya Dola 450.

Nyaraka zinaendelea kuonyesha kuwa, Mangunga, Agness na Merisa wakati wa safari yao walikaa kiti kimoja kilichokuwa na namba tofauti.

Agness alikaa kiti namba 23B, Mangunga alikaa kiti namba 23D na Melisa alikaa namba 23A.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Suleiman Suleiman, alipotakiwa kutoa ufafanuzi juu taarifa hizo, alikataa kulizungumzia kwa undani na kusema hana majibu kwa kuwa suala hilo liko katika uchunguzi.

Agness na Melisa, walikamatwa Julai 5 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Oliver Thambo nchini Afrika Kusini wakiwa na dawa za kulevya.

Wakati wanakamatwa, walikuwa na mabegi sita kati ya tisa waliyokuwa nayo wakati wanapanda ndege jijini Dar es Salaam.

Inasemekana mabegi matatu yaliondoka na Mangunga ambaye hadi sasa hajul
Read more...

Sunday, July 28, 2013

WATANZANIA WALIOKAMATWA NA MADAWA HONG KONG WATUMA WARAKA MZITO..WATAJA WAHUSIKA WAKUU..WAMO VIGOGO NA WAFANYABIASHARA MAARUFU

0 comments
WATANZANIA walio gerezani nchini Hong Kong kwa makosa ya kukutwa wakisafirisha madawa hatari ya kulevya,wametuma waraka mzito kwa wananchi wenzao kuelezea  mambo mengi ambayo wananchi wa kawaida hawayajui kuhusu biashara hiyo inayopigwa vita duniani kote,na pia wamewataja wahusika ambao ndio wamiliki wakuu wa biashara hiyo waraka wenyewe ni huu hapa chini..usome kwa makini:


Read more...

Friday, July 26, 2013

VYAMA VYA USHIRIKA NI MAGENGE YA WEZI-KIKWETE

0 comments
Rais Kikwete
Bukoba. Rais Jakaya Kikwete, amesema baadhi ya vyama vya ushirika nchini vina mkusanyiko wa wezi wanaokula fedha za wananchi bila hata kunawa.
Kikwete aliyasema hayo juzi jioni alipokuwa akizungumza na wananchi baada ya kufungua jengo la kitega uchumi la Chama cha Ushirika cha Mkoa wa Kagera (KCU), mjini Bukoba.
“Acheni kuwa wachuuzi tu wa kununua na kuuza mazao ya wananchi na badala yake mjiingize katika shughuli za uwekezaji na maendeleo ya kwelikweli ya wanachama wenu,” alinena Rais.
“Hapa Kagera ni kitovu cha ushirika na KCU ni kitovu cha kuboresha na kuleta usasa katika shughuli za ushirika. Siyo kama vyama vingine ambavyo ni mkusanyiko wa wezi wanaokula waziwazi mchana bila hata aibu ….wanakula bila kunawa,” alisisitiza.
Rais Kikwete alisema huko nyuma Serikali ilifanya uamuzi wa kulipa madeni yote ya ushirika nchini ili kuvipunguzia vyama mzigo wa kujiendesha.
Alisema hata hivyo sasa vyama hivyohivyo, vimeanza kujitumbukiza tena katika madeni na kwamba hiyo inatokana na kukosa viongozi waaminifu na waadilifu.
Kabla ya kuzindua jengo hilo, Rais Kikwete aliweka jiwe la msingi kwenye upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Bukoba ambao unapanuliwa ili kuufanya kuwa wa kisasa. Kazi hiyo itagharimu Sh21.015 bilioni, itakapokamilika.
Mradi huo wa upanuzi wa uwanja ulianza Februari mwaka jana na unatarajiwa kukamilika Februari mwakani.
Upanuzi huo ukikamilika uwanja huo utakuwa na uwezo wa kuhudumia wasafiri 500,000 kwa mwaka sawa na wasafiri 150 kwa saa.
Uwanja huo umekuwa ukilalamiwa kuwa ndiyo kikwazo cha kukosekana kwa huduma za uhakika za usafiri wa anga kati ya Kagera na mikoa mingine nchini.
Kwa sasa wananchi wengi wa mkoa huo wanaosafiri lwa ndege, wamekuwa wakiishia katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza na baadaye kusafiri kwa meli.
Read more...

Monday, July 22, 2013

ORPHANED GIRL BURNT WITH HOT WATER BY HER KEEPER IN AN ARGUMENT OVER DISAPPEARED PART OF FOOD

0 comments
Dora after after reciving medical treatment

A twelve years old girl,student of Wazo Hill Primary School in Dar Es Salaam,has claimed that she was burnt with hot water by her niece, Saum Masudi.

The little girl whose name is Dora said she faced that kind of atrocity few days ago in the Wazo area where she lives with Saum, her niece, and keeper after the death of her father.

In her account of the tragedy Dora said that in the morning of that day she woke up early and cleaned the house and in that course visited the den where they keep ducks to clean it.


"After finishing with cleanliness I went inside the main house and found thick porridge which was left over since yesterday.I took few slabs off and gave them to ducks in the den,my sister (niece) was asleep at the time.When she woke up,she found  the thick porridge was halved so she demanded to know what happened to the food.I told her that I served some to our ducks.She didn`t believe me,so she pulled me to the den to prove it.At the time we arrive at the den,there was nothing, the food was long been eaten by ducks.She called me a liar,and started to tie my hands and legs together.After that she splashed very hot water around my body."
Dora shows off severity of inflictions she received

She said she was wounded in different parts of her body and she never received instant medical care after that.After few days the wounds started to rot and stink until the day one of her relatives paid a visit and wanted to shave her untidy hair.In the process the relative told her to take off the T-shirt she was wearing so it doesn`t get covered by her falling hair.That`s when the relative came to the horrific scene of stinking wounds.After recovering from her shock of the day, the relative wanted to know what really happened .Dora explained it all and Dora`s keeper fled the house immediatelly.

Dora poses with her helper Kauthari Isack
After the news of her miseries broke it`s boundaries,Dora said a good samaritan Kauthari Isack who was  emotinally touched by Dora`s story took her to the Police station and then to hospital for medical care.Kauthari confirmed that she helped Dora to hospital after becaming emotinally very touched by her story
"I took her firstly to the police station to get Police Form 3 so she could be accepted by medical staff at the hospital, and people at the police station opened a case no.KW/RB/6034/2013.The search for suspect has just begun and they (police) have husband of the suspect to help the search.

The Kinondoni Regional Police Commander ACP Camillius Wambura has confirmed the incident regarding Dora inflictions and of the ongoing searching of the suspect

"I warn all members of the public, that this kind of cruelty can not be tolerated.People should refrain from doing such things, because we have severe punishment in store for this"
Read more...

HUU NI UKATILI MKUBWA..YATIMA AMWAGIWA MAJI YA MOTO,KISA KIPORO CHA UGALI!

0 comments
Mtoto Dora baada ya kupata msaada kutoka kwa msamaria mwema

Mtoto Dora Juma,12, mwanafunzi wa Shule ya Msingi Wazo Hill, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam imedaiwa ameunguzwa kwa maji ya moto na binamu yake aliyetajwa kwa jina la Saum Masud.
Dora ambaye ni yatima alikutwa na dhahama hiyo hivi karibuni eneo la Wazo Dar alikokuwa akiishi na binamu yake huyo kama mlezi wake baada ya kufiwa na baba yake.
Akisimulia tukio hilo Dora alidai kuwa siku ya tukio aliamka asubuhi kufanya usafi wa uwanja nyumbani na akaingia katika banda la bata kwa ajili ya kulisafisha.
“Baada ya kumaliza usafi niliingia ndani na kukuta kiporo cha ugali nikakata kipande nikawapa bata bandani, wakati huo dada (Saum) alikuwa amelala, alipoamka na kukuta kiporo cha ugali kimekatwa aliniuliza nikamueleza nimewapa bata, hakuamini.
“Akaniambia twende bandani kuangalia kama nasema kweli, tulifika tukakuta bata wameula hali iliyomfanya  dada  kutoamini, alinifunga mikono na miguu na kuniunguza kwa maji ya moto sehemu mbalimbali mwilini,” alidai Dora.
Mtoto Dora akionesha alivyounguzwa mgongoni kwa kumwagiwa maji ya moto
Alisema baada ya kufanyiwa unyama huo hakupewa huduma yoyote na kusababisha vidonda kuoza na aliokolewa na ndugu yao mmoja aliyekwenda kuwatembelea na kutaka kumnyoa nywele.
“Aliniambia nivue fulana ili nywele zisinidondokee, nilipovua alishangaa kuona nina vidonda mwilini, nilipomueleza mkasa mzima aliwapigia simu ndugu wengine hali iliyofanya dada Saumu kukimbia na kwenda kusikojulikana,” alidai.
Dora alisema alichukuliwa na msamaria mwema aitwaye Kauthari Issack ambaye aliliambia kuwa kweli alimchukua binti huyo baada ya kuguswa na unyama aliofanyiwa.
Mtoto Dora akiwa na msamaria mwema Kauthari Isack
 “Baada ya kumchukua nilikwenda polisi kupata PF3 ili akatibiwe na anaendelea kutibiwa, askari wakafungua jalada namba  KW/RB/6034/2013 na wakaanza kumsaka mtuhumiwa lakini wakafanikiwa  kumkamata mumewe aitwaye Hamisi Kayanda ili aisaidie polisi,” alisema Kauthari.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni ACP Camillius Wambura amethibitisha mtoto huyo kufanyiwa kitendo hicho na kusakwa mtuhumiwa. “Niwaonye wananchi kwamba ukatili kama huu hauwezi kuvumiliwa, watu wajiepushe nao maana watachukuliwa hatua kali za kisheria,” alionya Kamanda Wambura.
Read more...

MJANE WA MWANAJESHII ALIEUAWA DARFUR `ATOLEWA NDUKI`

0 comments
Hata kabla ya maziko askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa Darfur, Sudan hayajafanyika, mchumba wa mmoja wa wapiganaji hao, Amina Juma ameonja chungu nyingine baada ya kutimuliwa kwenye nyumba aliyokuwa akiishi na marehemu mwenza wake.
Amina ambaye inadaiwa kuwa alikuwa akiishi na Fortunatus Msofe aliyekuwa askari katika Kambi ya Msangani, 36KJ Pwani alisema jana: “Kumekuwa na mzozo wa hali ya juu na ndiyo maana tumeshindwa hata kufika Uwanja wa Ndege kuupokea mwili na hata kesho (leo) sidhani kama nitakwenda... kuna mtafaruku mkubwa wa kifamilia.”
Amina Juma
Baada ya kutimuliwa, Amina ambaye hawakuwahi kupata mtoto na marehemu Msofe, alilazimika kuondoka kwenye nyumba hiyo na kwenda Mlandizi kwa wazazi wake.
“Nimeishi na Msofe kwa miaka mitatu, akiwa kambini mimi niko hapa na wakati mwingine alikuwa analala huku... lakini leo wamenitimua,” alisema huku akilia.
Habari zilizothibitishwa na baadhi ya waombolezaji waliokuwa nyumbani kwa marehemu Visiga, Kibaha zinasema baadhi ya wanandugu walimkana Amina siku chache baada ya kutangazwa vifo hivyo.
Ilidaiwa kwamba Amina alitimuliwa katika nyumba hiyo Ijumaa iliyopita, saa saba mchana baada ya ndugu watatu wa marehemu kufika hapo wakitokea Tanga.
Walipofika inadaiwa kuwa walitangaza kusitishwa msiba huo katika nyumba hiyo na kutangaza kutomtambua mke huyo.
Watu hao waliwaeleza waombolezaji kuwa walitumwa na baba mzazi wa marehemu, Willbad Msofe kutoka Kange, Tanga kufika Kibaha kusitisha msiba uliokuwa ukiendelea nyumbani kwa mtoto wake huyo.
Inadaiwa pia kuwa katika msafara huo,  alikuwapo mdogo wa marehemu ambaye aliwahi kuishi kwa miaka miwili na Amina hapo Visiga.
Ilidaiwa kuwa walipofika nyumbani hapo walionana na mfiwa, Amina na wazazi wake ambao pamoja na majirani na watu wengine wengi, walikuwa wakimfariji binti yao huyo.
Mmoja wa waombolezaji alisema baada ya salamu wanandugu hao walianza kuulizia mali za marehemu na walikuwa wakimuuliza Amina ambaye aliwaleza kila kitu kilipo na baada ya hapo ndipo walipomweleza kuwa wametumwa na baba wa marehemu kuwa watu hawatakiwi kuomboleza kwenye eneo hilo kwani msiba upo Tanga tu ambako ndiko iliko familia yake.
Alipoulizwa baba wa marehemu, Mzee Msofe alisema: “Mimi ndiye niliyeagiza nyumba ifungwe na ukweli ninamfahamu Amina, lakini simtambui kama mkewe kwa kuwa hawajafunga ndoa... Hata wewe si unayafahamu haya? Uchumba si ndoa na ukifunga ndoa ndipo unatambulika rasmi,” alisema

Akiwa kwa wazazi wake Mlandizi jana, Amina alisema:
“Namwachia Mungu maana hayo yote nashangaa yanatokea wakati huu mume wangu ‘Fortu’ amekufa, mbona kipindi chote cha miaka mitatu iliyopita familia ya Tanga dada zake na mdogo wake tuliishi nao vizuri kwangu nilipokuwa na marehemu? Nimeishi na ndugu wote lakini hawakuwahi kuhoji, hata nilipokwenda na mume wangu Kange baba na mama Msofe nilikaa nao zaidi ya wiki na hawakunikana, ila nashangaa,” alisema na kulia kwa uchungu.
Akizungumzia kitendo hicho, baba yake Amina, Juma Juma alisema: “Nimeshangaa hizi taarifa. Tulikuwa tunajiandaa kupokea msiba wa mwanetu, lakini leo yanakuja mengine kwa kweli imetushangaza sana.”
“Nasubiri baada ya kumzika marehemu, nitazungumza nao... Kinachonishangaza ni kwamba walituandikia barua ya kumposa binti yangu na tukawajibu na gharama zilikuwa Sh1.2 milioni... Tutazungumza, ngoja hili lipite kwanza,” alisema mzee Juma.

WALIVYOISHI NA MAREHEMU
Akisimulia maisha yao, Amina alisema: “Tulianza kuishi Mbezi Luis mwaka 2010 katika nyumba ya kupanga na nikamshawishi tununue kiwanja na kwa kuwa mimi ni mwenyeji wa Kibaha, niliwatumia marafiki wa familia yangu Mlandizi wakatafutia eneo na mwaka 2011 tulipata na tukaanza ujenzi.
“Tukiwa Mbezi, tulianza kufyatua matofali kisha ujenzi ukaanza Visiga mwaka 2012 mwanzoni na  Septemba mwaka huo tulihamia kwenye nyumba yetu na hapo ndiyo ilikuwa makazi yetu hadi marehemu anaondoka kwenda Darfur.
“Wakati wote huo ‘Fortu’ alikuwa keshaniposa na hata barua zote za posa zipo na tulikuwa tukisubiri utaratibu wa kijeshi marehemu kukamilisha miaka sita ya kukaa kambini kisheria ndipo aruhusiwe kuoa.
“Fortu alikamilisha miaka hiyo mwaka 2012 mwishoni na wakati akijiandaa kwa kufunga ndoa ndipo ikatokea safari ya Darfur mwanzoni mwa mwaka huu na tukakubaliana tusitishe kwanza akirudi tukamilishe, lakini haikuwa.... Halafu wananifukuza wanasema hawanijui,” alieleza huku akiangua kilio.

CHANZO:GAZETI LA MWANANCHI
Read more...

Sunday, July 21, 2013

NUSU YA WAZAZI WA KIUME NCHINI WANALEA WATOTO WA KUBAMBIKIWA

0 comments

Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali nchini imesema karibu nusu ya watu waliojitokeza kupima vinasaba (DNA) ili kubaini uhalali wa watoto wao, vipimo vimeonesha si wazazi halisi wa watoto waliopimwa.
 
Takwimu hizo ni kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2010, ikionesha kuwa, asilimia 48.32 ya wazazi 'wanalea' watoto wasio wa kwao wakati asilimia 51.68 ndio wazazi halali.
Hayo yameelezwa jana na Mkuu wa Kitengo cha Makosa ya Jinai, Vinasaba na Baiolojia wa ofisi hiyo, Gloria Machuve katika mkutano na wanahabari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dar es Salaam.
 
Ingawa hakutaja idadi kamili ya waliojitokeza kupima DNA, alisema idadi hutofautiana mwaka hadi mwaka. Ili kufanya vipimo vya DNA, wazazi hulazimika kulipia Sh 100,000.

Machuve alisema kazi ya DNA si kutambua watoto halali na wasio halali pekee, bali vipimo hivyo vina umuhimu mkubwa kwa jamii. 
 
Alitoa mfano kuwa, matumizi ya Teknolojia ya vinasaba vya binadamu yamewezesha kesi mbili za mauaji ya vikongwe na albino kutolewa hukumu katika mikoa ya Shinyanga, Kagera na Sumbawanga baada ya kufanyika kwa uchunguzi katika matukio manane.

Aidha, alisema katika majanga mbalimbali yaliyokumba nchi ikiwa pamoja na milipuko ya mabomu yaliyotokea Mbagala, Dar es Salaam mwaka 2010 walitambua mabaki ya askari sita ambao baadaye walichukuliwa na ndugu zao na kuzikwa.
 
Alitolea pia mfano wa tukio la moto katika Shule ya wasichana ya Idodi mkoani Iringa ambako licha ya kuungua vibaya, miili ya wanafunzi 12 ilitambuliwa hivyo makaburi yao kutambuliwa. Katika Jengo la ghorofa lililoporomoka mtaa wa Kisutu mwaka huu, marehemu 23 walitambulika. 

Aidha, katika ajali ya Ndege ya Comoro mwaka 2010 mabaki ya miili ya marehemu 25 ilitambuliwa huku katika masuala ya uhamiaji teknolojia hiyo ilitumika kudhihirisha hawana uhusiano na wananchi wa Tanzania.

Machuve alisema katika masuala ya ubakaji na mimba za utotoni  teknolojia hiyo imesaidia kuwa fikisha wahusika mahakamani pamoja na katika wizi wa kutumia silaha.
Read more...

WAENDA JELA KWA KUPOST NYAMA YA NGURUWE NA KEJELI KWENYE FACEBOOK WAKATI WA MFUNGO

0 comments
Alvin Tan na Vivian Lee wakiwa chini ya ulinzi
Wamiliki wa Blog moja inayojihusisha na masuala ya ngono Alvin Tan na Vivian Lee wamefunguliwa mashtaka na kuwekwa ndani bila ya dhamana nchini Malaysia baada ya kuweka picha inayowakosea waumini wa kiislam kwenye Facebook.Wanakabiliwa na adhabu ya kifungo cha miaka minane jela.

Alvin na Vivian kwenye picha iliyowaponza ambayo ina ujumbe unaotafsirika kama"Futari njema furahi na nyama ya nguruwe,harufu nzuri, tamu, inayotia hamu ya kula"
Picha iliyowaponza  ilikuwa ikiwaonesha wakila nyama ya nguruwe ikiwa na ujumbe wa kuwatakia waislam ramadhan njema.Mamlaka inayosimamia sheria nchini humo imelichukulia tuko hilo kuwa ni kosa kubwa,ikizingatiwa kuwa nyama ya nguruwe ni haram (hairuhusiwi) kwa waumini wa kiislam.Ingawa watu hao walijitetea kuwa walilenga katika kuonesha ucheshi wao,imechukuliwa kuwa inawavunjia heshima baadhi ya watu katika jamii na pia kuzingatia na kazi wanayojihusisha nayo wakosaji pia si nzuri ambapo wamekuwa wakiweka video za ngono kwenye ukurasa wao wa Youtube uitwao `Sexcussions with Alvin` na pia wanamiliki blog inayoegemea kwenye masuala ya ngono.

Picha za ngono ni marufuku kwenye nchi za Malaysia na Singapore,hivyo tukio hilo limesababisha Tan mwanafunzi wa sheria Chuo Kikuu cha Malaysia kunyang`nywa hati za masomo ya juu (Scholarship) ya nchi za ASEAN,baada ya malalamiko ya wananchi dhidi ya blog yao.

Tan na Lee wameshakana mashtaka yao na wamewekwa ndani bila dhamana hadi kesi yao itakapoanza kusikilizwa Agosti 23 mwaka huu.Baada ya tukio hilo waliomba radhi kwenye ukurasa wao wa Youtube kwa kusema:
 "Tunarekodi video hii ili kuwaomba radhi waumini wa kiislam kwa kuwa tumewakosea kwenye mwezi huu mtukufu wa Ramadhan"


Read more...

Wednesday, July 17, 2013

ASKARI POLISI AELEZEA KILICHOTOKEA KATIKA SHAMBULIO LA DARFUR

0 comments
Askari wa JWTZ walionusurika wakiwa Hospitali

WAKATI Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), likiwa bado halijatangaza rasmi majina ya wapiganaji wake waliofariki huko Sudan, askari polisi aliyeko huko ameeleza chanzo na mazingira ya tukio hilo. Wapiganaji saba na wengine 14 walijeruhiwa Jumamosi iliyopita.

Askari polisi huyo anayefanya kazi katika Mji wa Nyala uliopo Darfur, alisema mauaji hayo yalitokea wakati askari hao walipokuwa wakifuatilia magari yao yaliyokuwa yameporwa na kundi mojawapo la waasi.
Usalama katika Mji wa Nyala ambao ndiyo mkubwa zaidi katika eneo la Darfur, umekuwa mdogo katika siku za hivi karibuni. “Wale wanajeshi walikuwa doria ya kawaida, ila kama wiki moja iliyopita waasi walivamia tena doria ya wanajeshi wetu na kupora magari manne bila kuua mtu.
 
Miili ya askari wa JWTZ waliouawa Darfur ikipewa heshima za mwisho
“Siku ya mauaji hayo wanajeshi wetu wakiwa tena katika doria waliyaona yale magari yaliyoporwa kwa mbali yamepaki, waliyafuatilia, walipokaribia kumbe ulikuwa mtego, wakashambuliwa,” alisema askari huyo na kuongeza: “Mauaji hayo yametokea takriban kilometa 70 kutoka katika kambi niliyopo mimi, lakini wote tupo eneo la kusini na hiyo kambi ya Korabeche inaongozwa na jeshi letu.” Tofauti na chanzo chetu cha habari huko Darfur, Kanali Mgawe alisema wanajeshi hao walishambuliwa walipokuwa kwenye msafara wa kusindikiza walinzi wa amani.
Askari huyo aliyeko Darfur alisema: “Makundi yanayopambana huku yapo mengi ila makubwa yapo kama matano. Kuna moja linaitwa Jeshi la Ukombozi la Watu wa Sudan (SPLA), ambalo limegawanyika katika makundi mawili pia kuna mengine kama JEM, Janjaweed na mengineyo.”
 
Akizungumzia mshtuko walioupata baada ya mauaji hayo, askari huyo alisema wafanyakazi wote wanaohusika na ulinzi wa amani wamepatwa na ganzi… “Huku kwa kweli hali imekuwa chungu, tangu askari hao wauawe hali haitabiriki kabisa, tupo nje hapa (hospitali walimohifadhiwa), tunasubiri uhakika.”
 
“Hawa jamaa (waasi), wamesheheni silaha na wana vifaa vya kisasa kiasi kwamba hata ndugu zetu walizidiwa kutokana na wenzao kuwa na silaha nzito, nikija Tanzania nitakuonyesha picha za mapambano yao,” alisema. Akizungumzia kazi ambazo polisi wanazifanya huko, alisema hawaruhusiwi kushika silaha, bali kuwashirikisha wananchi katika masuala ya amani.
 
“Sisi majukumu yetu ni kuungana na jamii na kuwafundisha masuala mbalimbali, hivyo sisi tunawasiliana moja kwa moja na wananchi waliopoteza makazi kisha tunaandaa taarifa. Haturuhusiwi kushika silaha, wanajeshi wao wanatulinda na kusimamia usalama na kutusindikiza wakati wa doria,” alisema.
 
“Huku hali ya usalama haitabiriki. Mpaka sokoni tunakwenda chini ya ulinzi.”  Akizungumza kwa simu jana, Kanali Mgawe alikanusha uvumi wa majina yaliyosambaa mitandaoni huku akisema kwa utaratibu uliopo, jeshi haliwezi kutangaza majina hayo hadi ndugu watakapotaarifiwa. “Hayo majina yanayotajwa kwenye mitandao ni ya uongo. Kwa sasa mimi sijaletewa majina na utaratibu uliopo ni hadi ‘next of kin’ (ndugu) wao wajulishwe kwanza,” alidai Kanali Mgawe.
 
Hata hivyo, alisema Tanzania imewasilisha maombi ya kubadilisha kanuni za kulinda amani ikitaka kuruhusiwa kujihami kwa silaha za moto pale wanajeshi wake wanaposhambuliwa kwa kutumia kanuni namba saba ya Sheria za Majeshi ya Kulinda
Read more...

VITAMBULISHO VYA TAIFA:MAMLAKA YAANZA KUCHUKUA ALAMA ZA VIDOLE,SAINI NA PICHA

0 comments
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), imeanza zoezi la kuchukua alama za vidole vyote kumi, kupiga picha na kuweka saini ya kielektroniki kwa wakazi wa Wilaya ya Temeke tayari kwa kutoa vitambulisho hivyo.
Kaimu Mkuu wa Mawasiliano na Machapisho, Thomas William aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, kutokana na wingi wa watu katika Jiji la Dar es Salaam, zoezi hilo limegawanywa katika ngazi ya wilaya hadi wilaya.
“Hili zoezi tumelianza juzi, tunachukua alama za vidole kumi, kupiga picha na kuweka saini za kielektroniki kwa wakazi wa Temeke, tumeanzia Kigamboni na kutokana na ukubwa wake tumeigawanya kwa kanda saba,” alisema.
  William alisema,  kanda ya kwanza inahusisha mitaa yote katika kata za Kimbiji, Pemba Mnazi, Kigamboni, Vijibweni, Kibada, Mji Mwema, Somangila, Kisarawe 11, Tungi na mitaa ya Mtoni Kijichi, Mgeni nani na Misheni iliyoko katika Kata ya Kijichi.
Alisema, ili kuboresha mwonekano mzuri wa picha kwenye kitambulisho hicho, mwombaji anashauriwa kutokuvaa nguo nyeupe, kijivu, bluu mpauko, pinki na kofia au kapelo wakati wa kupiga picha.
Aidha, William aliwataka waajiri wa mashirika mbalimbali kuwaruhusu watumishi kushiriki katika zoezi hilo siku watakayokuwa wamepangiwa ili kurahisisha zoezi hilo na kuepuka usumbufu wa kurudia eneo.
“Tunawaomba waajiri katika mashirika mbalimbali nchini wawaruhusu watumishi wao kufika katika eneo muhimu kwa kuzingatia tarehe aliyopangiwa ili kufanikisha zoezi. Hata wale ambao walikuwa hawajajaza fomu za kujiandikisha wanatakiwa kufika katika kata zao ikiwa zoezi linafanyika katika halmashauri hiyo,” alisema William.
Alisema, zoezi hilo limetoa kipaumbele kwa makundi maalumu ya walemavu na wazee wasiojiweza na kuwa walemavu wa mikono watapigwa picha bila kuchukuliwa alama za vidole.
Katika Jiji
la Dar es Salaam, zoezi hilo limeanzia Wilaya ya Temeke, likifuatiwa na Ilala na kumalizikia Kinondoni
Read more...

Sunday, July 14, 2013

BREAKING NEWS:..BASI LA NAJMA LAPATA AJALI DARAJANI RUFIJI

0 comments
Bus la kampuni ya Najma linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Nachingwea, limepata ajali kwenye daraja la Mkapa, Ikwiriri baada ya kugonga pikipiki na kusababisha vifo vya watu wawili papohapo.
Chanzo cha ajali hiyo ni moshi mkali uliotanda kwenye eneo la ajali kutokana na moto uliokuwa unaunguza majani yaliyopo pembezoni mwa barabara ya kusini mara baada ya kumaliza daraja la Mkapa. Basi hilo lilikuwa linatokea Nachingwea kwenda Dar es Salaam.
Watu waliofariki ni wale waliokuwa kwenye pikipiki. Ajali hiyo imetokea majira ya saa 6:40 mchana. Hata hivyo gari hilo halikupinduka isipokuwa imeharibika vibaya sehemu ya mbele. Baada ya ajali hiyo, dereva alisogeza gari kwenye kituo cha polisi cha Ikwiriri na baada ya kutoa maelezo, polisi wameenda eneo la tukio kuchukua maiti.
Mtoa habari hii ni miongoni mwa watu waliokuwa abiria kwenye basi hilo. Namba ya gari ni T 599 CBL aina ya YUTONG
.
Read more...

Saturday, July 13, 2013

BODABODA TISHIO LA NDOA ZA WATU.

0 comments
Madereva  wa  bodaboda licha ya biashara ya kusafirisha abiria, wamezua tabia nyingine ya kufanya ngono na  wateja wao wa kike, hasa wanafunzi na wake za watu.
Imebainika kuwa baadhi ya madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda wanatumia usafiri huo kuwarubuni na kuwashawishi wanafunzi wa kike wa shule za msingi na sekondari na kufanya nao ngono.
Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumapili jijini Dar es Salaam katika Wilaya za Temeke, Ilala na Kinondononi, umebaini kuwa wanafunzi wengi wamejiingiza katika vitendo vya ngono baada ya kunaswa na ulaghai wa madreva bodaboda wengi wakiwa vijana wadogo.
Madereva hao wamekuwa wakifanya ngono na wanafunzi, baada ya kuahidi kuwasafirisha bure kwenda na kurudi kutoka shuleni, hasa kwa maeneo ambayo hakuna usafiri wa daladala au eneo lililo mbali na kituo cha basi wakati wa kutoka au kwenda shuleni.
Gazeti hili limebaini kwamba, baadhi ya walimu pia wamejiingiza katika mchezo huo mchafu na kufanya ngono na vijana wadogo wanaoendesha bodaboda.
Madereva hao wanaoonekana katika vituo vya daladala, huwafuata wanafunzi hao wanaosumbuliwa na shida ya usafiri wakikataliwa kupanda daladala makondakta wa daladala hasa wakati wa asubuhi na jioni.
“Njoo asubuhi utaona wanafunzi wanavyohangaika kupata usafiri, mtu amefika kituoni toka saa kumi na mbili hadi saa mbili bado yupo hapa kila basi linalokuja anaambiwa wanafunzi wametosha. Katika mazingira haya kwanini asirubuniwe na mtu wa bodaboda?” alihoji mmoja wa wazazi alijitambulisha kwa jina la Mwambene na kuongeza:
 “Kuna baadhi ya madereva ninawafahamu wana uhusiano na wanafunzi wawili hadi watatu, tena hawachagui mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari, lazima wazazi wawafuatilie watoto wao vinginevyo wanafunzi hawatamaliza masomo.”
Baadhi ya madereva bodaboda walisimulia wanavyowashawishi na kuwanasa wanafunzi, wakikiri kulitumia tatizo la usafiri wa kwenda na kurudi kutoka shuleni kuwapata kirahisi wanafunzi.
Akionekana kuvifurahia vitendo hivyo, mmoja wa madereva wa bodaboda katika kituo cha daladala cha Temeke mwisho, (jina tunalo) alisema baadhi ya wanafunzi wanaona ufahari kupelekwa shuleni kwa pikipiki jambo linalowafanya wawe tayari kukubali kufanya ngono.
“Wapo wanafunzi wanaopenda kuonekana wanatoka katika familia bora, ...hao ndiyo rahisi sana kuwapata, ukimpeleka shuleni mara ya kwanza, mara ya pili basi umemaliza mchezo,” alisema dereva huyo akijinasibu.
Alisema baadhi ya wanafunzi hutoka nyumbani kwao wakiaga wanakwenda shuleni lakini badala yake hukutana na madereva wa bodaboda ambao huwapeleka mafichoni na kufanya nao ngono.

Dereva mwingine wa bodaboda, mkazi wa Keko Machungwa, Elikunda Kileo alikiri kuwepo kwa matukio hayo akisimulia kuwa mmoja wa madereva wa bodaboda alipigwa na wananchi baada ya kukutwa akimtomasa mwanafunzi wa shule ya sekondari akiwa ndani ya mabanda ya kutengenezea samani.
Kwa mujibu wa Kileo, dereva huyo alimhaidi mwanafunzi kuwa angempeleka shuleni, lakini muda mfupi baadaye alimwingiza kwenye banda la mafundi seremala na kuanza kumdhalilisha kwa kumtomasa maeneo mbalimbali ya mwili wake.
“Jamaa aliingia na mwanafunzi kwenye banda la mafundi seremala linalomilikiwa na kaka yake, cha kushangaza tuliona anataka kufanya vitu vya ajabu, maana alianza kumshikashika yule binti, ingawa binti mwenyewe hakuwa na wasiwasi wowote,” alisema Kileo na kuongeza kuwa:
“Mafundi wakamwambia aondoke, lakini jamaa akaanza kuwatukana ndipo walipoamua kumpa kipigo.”
Dereva mwingine wa bodaboda anayefanya kazi Mbezi Msumi alikiri kuwa na uhusiano na wanafunzi wawili na mwalimu mmoja kutokana na kuwapa lifti ya pikipiki mara kwa mara.
“Si unajua tena kaka, mi ninao wawili, mmoja kidato cha pili mwingine cha nne, tena nina mwalimu, wote nawachukua, ingawa wakati mwingine naona aibu kuwa naye kwani yeye ni mkubwa kuliko mimi,” alisema dereva huyo.
Hata hiyo, baadhi ya madereva wa bodaboda waliwatupia lawama wanafunzi kuwa wao ndiyo wanaowashawishi madereva hao kufanya nao ngono.
Renatus Kitwana dereva wa bodaboda anaefanya biashara yake katika kituo cha Ukonga Mombasa, alisema baadhi ya wanafunzi hufika kituoni hapo na kusimama muda mrefu wakiwasubiri ‘watu wao’. “Kuna wanafunzi huja hapa kutafuta pikipiki, lakini wakiwakosa watu wanaowataka watasubiri muda mrefu hadi jamaa watakaporudi kitu kinachoonyesha kuwa nao wanapenda kufanya vitendo hivyo,” alisema Kitwana.
Wanafunzi wananena
Agnes Tarimo, mwanafunzi aliyehitimu kidato cha nne mwaka 2012 katika shule ya sekondari Jangwani, alisema kuwa kuna baadhi ya wanafunzi wasichana walikuwa wanakwenda shuleni wakiwa na nguo za kubadilisha kwenye mabegi yao kwa ajili ya kutoka shuleni na kuingia mitaani bila kujulikana.
“Kuna wanafunzi wenzetu walikuwa wanabeba nguo za kubadilisha kwenye mabegi yao. Jamaa wa bodaboda wakija wanakwenda nao sehemu wanabadilisha nguo, halafu wanakwenda kufanya mambo yao huko mafichoni,” alisema Agnes.
Naye Mwanaidi Seif mwanafunzi wa kidato cha Tatu, shule ya sekondari Perfect Vision, alisema kuwa  tamaa ya usafiri wa bure (lifti) na chips imewafanya wanafunzi wengi kujihusisha na vitendo vya ngono
 
“Wanafunzi wengi wanatamaa ya kupata vitu vizuri, wengi wamejikuta wakifanya ngono na kupata mimba kwa kupenda kupewa lifti na chipsi,” alisema Mwanaidi.
Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mtakatifu Anthony, Mbagala ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini kwa kuwa si msemaji wa shule, alisema kuwa suala la wanafunzi kuwa na uhusiano na madereva siyo geni na kwamba lipo tangu siku nyingi.
“Ingawa hapa shuleni hatujapata kesi kama hiyo, lakini suala hilo si geni lipo toka siku nyingi na siyo madereva wa bodaboda tu wanaofanya vitendo hivyo hata madereva wa taxi na daladala,” alisema mwalimu huyo. Alisema baadhi ya madereva wanaojihusisha na ‘mchezo’ huo ni watu wazima ambao umri wao ni sawa na wazazi wa wanafunzi wanafanya nao ngono.
“Wengine ni watu wazima kabisa sawa na baba zao... wazazi lazima wawaangalie sana watoto wao hali ni mbaya,” alisema mwalimu huyo.
Wazazi walonga
Meshack Kilave, mkazi wa Tabata ambaye binti yake anasomoma kidato cha kwanza kati shule ya sekondari Magomeni alisema tatizo la wanafunzi kujihusisha kimapenzi na madereva lipo toka siku nyingi na kwamba wanafunzi wanabuni mbinu mpya kila siku za kuwaficha wazazi wao.
“Baadhi ya wanafunzi huaga nyumbani kuwa wanakwenda kwenye masomo ya ziada kumbe wameshatekwa na jamaa wa bodaboda,” alisema Kilave.
Alishauri wazazi kuwafuatilia kwa kuwauliza watoto wanapowabaini kumiliki vitu ambavyo hawakukinunua wazazi.
“Wazazi watawafuatilie watoto wao kwa karibu, watabaini mambo mengi yaliyofichika, badala ya kukaa na kusikia ukiambiwa mwanao ni mjamzito.”
Naye Stumai Ng’ingo, mkazi wa Kongowe alisema ameshtushwa na taarifa za madereva wa bodaboda kufanya ngono na wanafunzi akieleza kuwa ndio kwanza amezisikia taarifa hizo.
“Ndiyo ninasikia kwa mara ya kwanza kuwa madereva wanaweza kufanya hivyo, sijui kama wadogo zangu wanaosoma sekondari wanaweza kupona wasitumbukie mikononi mwa hao jamaa,” alisema Stumai. George Daffa, mkazi wa Mtoni kwa Azizi Ali aliwatupia lawama baadhi ya wazazi kuwa wanachangia watoto wao kufanya vitendo vibaya kutokana na kukosa uangalizi wa kutosha.
“ Baadhi ya wazazi wanahitaji kubadilika, waache tabia ya kudhani wakishawalipia watoto  wao ada basi jukumu la kuwafuatilia limeisha,” alisema Daffa
Read more...

FAMILIA YAPATA KICHAA BAADA YA MGANGA KUWAPA DAWA

0 comments
Mwalimu aliyetumia uchawi kuwaroga wezi, amejikuta akiwaroga shemeji zake waliopata uchizi huko Butiama. Ilikuwa kama simulizi ya kwenye filamu, baada ya mganga wa kienyeji aliyeletwa toka Kenya kuja kuwaroga wezi walioiba nyumbani kwa Mwalimu mstaafu, Raphael Omwando (60), baada ya dawa yake kuwatia uchizi ndugu wa mke mkubwa wa aliyeibiwa.
Mwalimu Omwando ambaye ana wake wawili alivamiwa na wezi waliomwibia pikipiki na mali nyingine, ikiwemo kumjeruhi yeye (Omwando) na mkewe mkubwa. Mke mdogo aliyemuoa hivi karibuni anaishi kwenye nyumba nyingine na hakuweza kuvamiwa na wezi hao, lakini mke mkubwa alipigwa hadi kulazimika kupewa matibabu hospitali.

Watu walio karibu na familia hiyo walisema kutokuelewana kati ya mke mkubwa na mdogo, kulimfanya mke mkubwa aliyejeruhiwa na majambazi kumtuhumu mke mdogo kwamba alishirikiana na majambazi hao.
Filamu hiyo ya familia ilianza kwa ndugu wa mume (Omwando) wanaoishi Kenya, kuleta sangoma kwa ajili ya kubaini wezi waliomwibia ndugu yao.
“Sijui nimefikaje hapa hospitali…maana kumbukumbu zinaishia pale nilipolazimishwa kunywa dawa na mganga wa kienyeji (Sangoma) anayedaiwa kutokea nchini Kenya …ili wezi wa pikipiki na vifaa vya mwalimu mstaafu virudishwe,” hiyo ni kauli ya mmoja kati ya watu wanne waliolazwa hospitali kwa madai ya kurukwa na akili.
Wagonjwa hao ni vijana wanne wa Kijiji cha Kirumi  Kata ya Bukanga, Tarafa ya Makongoro, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara waliolazwa hospitali ya Mkoa wa Mara baada ya kunywa dawa hiyo na kupoteza fahamu huku wakionekana kama mazuzu (Mazombi).

Waathirika
Matiko Joseph (25) anasema yeye alilazimishwa kunywa dawa nyingi pamoja na makapi yake,” …Baada ya kumtajia mganga hivyo akasema ninyi kunyweni nyingi…dawa ilikuwa na ukakasi ilinikereketa sana. Baada ya kunywa niliondoka lakini baadaye hali ikabadilika sana,” anasema na kuongeza,
“Nilishtukia niko hospitali tayari ikiwa ni siku ya pili …Nikisimuliwa ilivyokuwa nazidi kushangaa…huyo mganga alilenga kutuua kabisa….maana wakati anatoa dawa alisema atakayepata madhara hatapona hata akipelekwa wapi mpaka vitu virudi ama fedha…akaondoka kwenda Kenya na hakuacha simu wala jina lake kujulikana,” anasema Joseph huku akipumua kwa harakaharaka.
Tura Joseph (30) anasema wengine walikunywa kidogo lakini wao wana ndugu walilazimishwa kunywa zaidi kwa kile kinachodaiwa kuwa walihisiwa kula njama za kumdhuru shemeji yao, na ndiyo walidhurika zaidi.
Anasema baada ya kunywa alihisi kitu kinamkaba shingoni na kuishiwa nguvu, akawa hoi na kuanza kuongea maneno yaliyowatia shaka, ndugu wakawabeba kwa bajaji hadi hospital

Boniphace Joseph (20)huku akisitasita, anasema ana habari kabla ya kunywa dawa lakini baada ya kunywa hakumbuki kilichoendelea mpaka alipopata fahamu na kuona watu wanamshangaa naye akiwashangaa.
Msira Magesa (17) anasema yeye baada ya kunywa alitoka kwenda kwenye shughuli zake, ghafla akazidiwa na kupewa dawa ya kutuliza maumivu aina ya panadol hali ikazidi kuwa mbaya na kufikishwa hospitali kwa matibabu

Hali ilivyokuwa
Julai 5, majira ya saa 5:15 usiku mwaka huu, Mwalimu mstaafu, Raphael Omwando (60) alivamiwa na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi, wakamkata yeye, mkewe akapigwa na majambazi hao na baada ya kipigo waliiba pikipiki, mabegi ya nguo, sola, sanduku dogo la kuhifadhia nyaraka, simu ya mkononi na vitu vingine.
Omwando kutokana na majeraha aliyoyapata akapelekwa hospitali ya mkoa alikolazwa kwa matibabu, lakini ndugu zake wanaoishi Shirati na wale wanaoishi nchini Kenya baada ya kupata taarifa waliamua kuchukua mganga wa kienyeji kutoka Kenya, ambaye aliwahakikishia kuwa wahusika baada ya saa 3 watarudisha vitu walivyoviiba wakiwa wamejitwisha na pikipiki wakiwa wanaisukuma.
Mganga huyo alieleza dalili za awali zitakazowapata wezi hao kuwa ni kuchanganyikiwa, wengine watakuwa wanakula nyasi kama ng’ombe. Mganga huyo alitoa tangazo kwamba  Julai 9 majira ya saa 9:00 alasiri wanakijiji wote wajitokeze kunywa dawa hiyo ili kuwapata wahusika.

Vituko vyao walikojoleana, kutapikiana
Mmoja wa wauguzi katika hospitali hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe anasema, walipofikishwa hapo aliogopa,“ walikuwa wanakojoleana midomoni, wanatapikiana, huku wakiongea lugha za ajabuajabu, tuliogopa maana ni tukio la kwanza kutokea,” anasema.
Anasema walipewa dawa za kuwafanya walale lakini wakaonekana wanaendelea kuongea wengine kukimbia huku wakidai kuna watu wanataka kuwaua, lakini sasa wametulia wanaongea wenyewe.
Shuhuda mwingine Isa Magesa anayemuuguza ndugu yake anasema Matiko, mmoja wa waathirika hao alikuwa akikimbia kasi kwenda nje huku akipiga kelele, “Nililazimika kutoa msaada, nilipomkamata alionekana ana nguvu sana huku akisema…acheni kuniua…hao wanakuja kuniua…nisaidie …wabaya hao, huku akionyesha kwa vidole lakini wao hawawaoni,” anasema.

Mganga Mfawidhi.
Dk Iragi Ngerageza, Mganga Mfawidhi Hospitali ya Mkoa, anasema vijana hao walifikishwa hapo wakiwa hawajitambui huku ikidaiwa kuwa walipewadawa na mganga wa kienyeji na kuwapokea wakiwa na hali mbaya  na kuwa hali hiyo bado wanaendelea kuichunguza


“Inakuwa vigumu kujua madhara ya hiyo dawa, kama tungeweza kuipata na kupeleka kwa mkemia ingetoa majibu, lakini kwa sasa sisi tunaendeleakuwatibu…lakini ni hatari maana kama walikunywa wakafikia hatua hiyo lazima kuna kitu, ikipatikana itatusaidia,” anasema.

Mke wake akamatwa.
Pilly Esther mke mdogo wa Mwalimu Omwando amekamatwa kwa kuhusishwa na tukio hilo,  kusaidia kumpata mganga aliyehusika na anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Butiama.
Hata hivyo akizungumzia tukio hilo anasema, wakati mume wake anavamia yeye alikuwa kwake na alisikia kelele za mbwa, lakini hakuelewa kilichotokea mwishoni akapigiwa simu na mke mkubwa kuwa wamevamiwa na kuumizwa. “Ndugu wa mume wangu akiwemo mke mkubwa ambaye ni Mjaluo wa kwao walinituhumu mimi kuwa ndugu zangu ndiyo wameiba mali kwa kuwanimeolewa hivi karibuni..au mpenzi wangu wa zamani ndiye amehusika, nilipokataa wakasema wanakuja na mganga kutoka Kenya ambayeanatoa majibu haraka,” anasema.
Anasema mganga aliomba mtendaji kualika wananchi wote lakini akakataa wakafika kama 40 wakiwemo kinamama, lakini kabla ya kutoa dawa akawaanasema wahusika ni kama anawaona hapo anawaomba wasinywe dawa, ajabuwaliopata madhara ni ndugu wa mke mkubwa
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797