Pages

 

Monday, June 11, 2012

KITUKO:WAZIRI MKUU WA UINGEREZA ,DAVID CAMERON AMSAHAU BINTI YAKE WA MIAKA 8 PUB JANA JUMAPILI

0 comments
Ilikuwa ni mshike mshike David Cameron alipofika nyumbani na kugundua kumbe Nancy,binti yake mwenye umri wa miaka 8 hayupo kwenye msafara, amemuacha pub

Alipiga simu pub na kuhakikishiwa kuwa Nancy yupo pale na yuko salama

Akachomoka sekunde ile ile na kufunga safari ya maili 2 kurejea kwenye pub inayoitwa Plough Inn ambayo yeye na familia yake walikwenda kupata msosi wa mchana jana Jumapili

Inasemekana Mtoto huyo alikuwa yuko maeneo ya choo cha wanawake kwenye pub hiyo wakati msafara wa Cameron na mkewe unaondoka kurudi nyumbani,na hakuna aliyehisi chochote hadi walipofika myumbani.


Cameron, mkewe Samantha na watoto wao Nancy,Arthur (6)na Florence mwenye umri wa miezi 22, walikuwa wamejumuika na familia zingine mbili kupata chakula cha mchana katika mkahawa wa Plough Inn jana Jumapili.Mkahawa huo ulioanzishwa katika karne ya 16 upo maili mbili kutoka katika nyumba ya mapumziko ya Cameron iliyo maeneo ya vijijini.Baada ya chakula,Cameron na familia yake wakiwa wamezungukwa na walinzi,waliingia kwenye gari kurejea nyumbani,huku Cameron akiwa na dhana kwamba Nancy yumo ndani ya gari jingine alilopanda mkewe na watoto.Huku mkewe akidhani kuwa Nancy yumo kwenye gari alilopanda baba yake.

Waziri mkuu huyo aliporejea kwenye eneo la pub alimkuta binti yake huyo kajichanganya na wafanyakazi wa pub akiwasaidia kazi huku akiwa na furaha.




Plough Inn
Wahusika wa pub hiyo wanasema mara walipomgundua Nancy chooni hawakujua wafanye nini.Mmoja wa wafanyakazi hao alisema"Unaweza kujiuliza kwanini wasihesabu vichwa wakati wanaondoka.Wafanyakazi wa hapa walipomgundua mtoto chooni,hakuna aliepata wazo haraka,kwa sababu ni vigumu kupata namba ya simu ya waziri mkuu kwenye kitabu cha orodha ili kumfahamisha kuwa wamesahau mtoto nyuma"
SOURCE: The Sun

Read more...

FRESH REPORTS AND EXCLUSIVE IMAGES ON SAITOTI`S HELICOPTER CRASH

0 comments
Kenya's Internal security minister George Saitoti and his assistant Orwa Ojode were among six people perished in helicopter crash  occured at 9.05 am on Sunday morning at Kibiku forest near Ngong town.They were heading to Orwa Ojode's Ndhiwa Constituency for a church function.

 Other four people who died on the crash are, Pilots (Nancy Gituanja and Luke Oyugi), Bodyguards (Inspector Tongei & Thomas Murimi.
 The pilot who was flying the ill-fated helicopter was the officer who conducted the final tests for the government to buy the aircraft.

Superintendent Nancy Gituanja, a mother of three, signed the acceptance form after flying the helicopter in Nairobi for one hour.
The government formally accepted the aircraft after it had been confirmed serviceable by Supt Gituanja, who died in the crash. Supt Gituanja and Supt Luke O. Oyugi were the captain and co-pilot respectively.
They are said to have been very experienced and had travelled with Internal Security minister George Saitoti on several missions. They were at Kedong for a rally last week.
Air wing Commandant Rodgers Mbithi said that they normally fly with two pilots for enhanced safety reasons. “It must have been something abrupt and out of their control,” said Mr Mbithi.
The team was supposed to leave at 8am yesterday but Internal Security assistant minister Orwa Ojode delayed, forcing them to leave at 8.30am.
Mr Ojode drove himself to the station and parked his vehicle, a dark blue Mercedes Benz, at the Air wing’s parking lot.
Supt Gituanja and Supt Oyugi had the call signs Falcon 230 and Falcon 233 respectively assigned to them

They met Mr Mbithi at 7am and checked the location of their destination, Ndhiwa, Nyarungi Parish Church, through Google and came up with the coordinates.
The two were on a mission to take the VIPs for a church service where they were also supposed to conduct a fund-raiser. They were also supposed to take Prof Saitoti to Borabu at around 9am today to attend a peace rally.
Pilot Gituanja underwent training in the Ukraine in April 2009. She also went through specialized training regarding the aircraft in South Africa.
Last December, she went to South Africa together with the Kenya Police Airwing commandant for a two-week training.
At the same time, Supt Oyugi’s widow, Ms Patricia Adhiambo Owino, 37, said she was shocked to receive news about the death and is struggling to come to terms with it.
Ms Adhiambo Owino, who is based in Homa Bay, said she last talked with her husband over the phone at 5pm on Saturday when he had just come from work. She last saw him two weeks ago.
“We happily discussed family issues and agreed that I would travel to meet him in Nairobi next week. That was never to be and I did not know that I was talking to my lovely husband for the last time,” she said
 Here are some of the images from the crash scene.
Kenya`s artist imagination in the wake of  the crash

Late Superintendent Nancy Gituanja one of the two pilots who were flying the ill-fated chopper
 Late Superintendent Luke Oyugi co-piloted the flight before the chopper went down
The ill-fated chopper on it`s helipad at Kenya Police Air wing
Cockpit of the ill-fated chopper



Investigators busy to find clues



Military presonnel guarding the crash scene











Read more...

Sunday, June 10, 2012

PICHA 20 ZA JUMBA JIPYA LA KISASA LA WEMA SEPETU..

0 comments
Read more...

FLOYD MAYWEATHER SR. BELIEVES PACQUIAO WON LAST NIGHT FIGHT

0 comments
 Everyone has an opinion on who won the fight last night (sunday morning in Tanzania) and that includes Floyd Mayweather’s Dad, Floyd Mayweather Sr.  He spoke with a couple ESPN reporters last night after watching the Pacquiao/Bradley fight.  Check out who he thought won.... reporters tweeted

Read more...

AJALI YA NDEGE:WAZIRI SAITOTI AFARIKI DUNIA

0 comments
Hayati George Saitoti



Hayati Joshua Ojode

Waziri wa Usalama wa ndani wa Kenya Profesa George Saitoti na Naibu wake Orwa Ojode wamefariki dunia katika ajali ya helikopta ya polisi iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Kibiku, karibu na mji wa Ngong takriban kilometa ishirini kutoka mji mkuu wa Nairobi.
Abiria wote sita, wakiwemo marubani wawili na walinzi wa mawaziri hao waliokuwa kwenye helikopta hiyo wamefariki dunia na miili yao kuteketezwa kwa kiasi cha kutoweza kutambulika.
Kilichosababisha ajali hiyo bado hakijajulikana

Kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Habari la Uingerza BBC waziri Saitoti na maafisa wengine wa juu katika wizara ya usalama wa ndani walikuwa wakielekea katika eneo la Sotik kwa mkutano unaohusu mambo ya usalama.

 Saitoti alikuwa miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini Kenya waliokuwa wakipania kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao.

Walioshuhudia ajali hiyo wamesema waliona helikopta hiyo ikizunguka angani kabla ya kuanguka katika msitu wa Ngong.
Polisi wamezingira eneo la ajali hiyo na kamishna wa polisi Mathew Iteere aliyepo katika eneo la ajali anatarajiwa kutoa taarifa kamili kuhusiana na ajali hiyo.

Ajali hiyo ya helikopta imetokea katika siku ambapo Kenya inaadhimisha miaka minne tangu kutokea ajali ya ndege iliyowauwa mawaziri wengine wa serikali, Kipkalya Kones na Lorna Laboso

SOURCE: BBC.http://www.bbc.co.uk/swahili/habari
Read more...

Monday, June 4, 2012

WARAKA WA GODBLESS LEMA KWA RAIS KIKWETE HUU HAPA: "IKULU iliingilia kesi yangu ya Ubunge"

0 comments

“ Ndugu Wananchi;
 Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi na shukrani nyingi kwa ndugu zetu wa Arusha kwa kuwapokea vizuri na kuwakarimu vyema wageni wetu hao. Nawaomba waendelee na moyo huo mpaka watakapoondoka wote. Naomba kuwepo kwa mkutano huu kuwakumbushe umuhimu wa mji wenu kuwa tulivu. Miaka miwili iliyopita isingekuwa rahisi kwa watu au shirika kubwa la kimataifa kama Benki hii kuamua kufanya mkutano wake Arusha. Isitoshe hata sisi wenyewe tusingeshawishika kuomba au kukubali maombi ya namna hiyo. Lakini sasa imewezekana. Naomba kila mmoja wetu aweke azimio moyoni mwake la kuhakikisha kuwa hali ile haijirudii tena. Nyota ya Geneva ya Afrika lazima iendelee kuangaza. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo . ( J.K . KIKWETE.)
“Narudia tena , IKULU iliingilia kesi yangu ya Ubunge”.
Mh Rais nimekusikiliza kwa makini sana ila nakupa pole kwani bado unafikiri unaongea na Tanzania ya mwaka 1961 , umesema sasa Arusha ni shwari tofauti na miaka miwili iliyopita kwani sasa kuna amani na utulivu wa kutosha ndio maana hata mkutano wa AFDB umefanyika Arusha .
Mh Rais , najua IKULU iliingilia kesi yangu kama ilivyoonekana na ndio sababu hata Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakati anaapisha Wakuu wa Wilaya alimpongeza Jaji kwa hukumu nzuri aliyowafurahisha wakati kesi hiyo iko mahakama ya Rufaa , lakini jambo moja la msingi ambalo huwezi kulitambua kwa sasa ni kuwa Haki na Ukweli haviwezi kushindwa na dhuluma, ubaya wala mamlaka , natambua wewe ni Rais na unayo mamalaka makubwa katika Taifa hili lakini vile vile nataka utambue kuwa huna mamlaka makubwa dhidi ya haki , utu na ukweli.
Mh Rais hakuna Amani Duniani inayozidi Haki na usawa ,utu na ukweli , haipo na wala haitakuwepo , ndio maana kila siku nasema ni “Afadhali Vita Inayotafuta Haki na usawa kuliko Amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa Mwanadamu “ umefurahia sana mkutano uliokupa fursa ya kutoa maneno ya kebehi na kudhihirisha ila chafu iliyofanywa na Serikali yako na kujaribu kuhadaa Umma kama ilivyo kawaida ya Serikali yako na Chama chako , hata hivyo wakati huu kuna mambo ya msingi yakushughulikia zaidi ya kebehi na hadaa , Uchumi wa Nchi umeyumba, huduma za msingi za jamii zimepuuzwa, Mpasuko katika suala la Muungano na vururugu zinazoendelea Zanzibar , mfumuko wa bei hizi ni sababu chache ambazo haziwezi kuruhusu wakati huu kuwa wakati wa kebehi na mizaha isipokuwa kazi .
Mh Rais , Mama Theresa , Nelson Mandela , Martin Luther Jr na Malcom X hawakuwa Wabunge kupigania haki za Nchi yao na watu wao , sihitaji Ubunge kupigania ukweli, haki na utu , nahitaji dhamira safi , nia njema na huu utakuwa wajibu wangu mpaka nakwenda kaburini , nitakapomaliza mbio hizi najua nitapata fursa ya kutazama nyuma yangu nione nini nilifanya , ukweli nisingependa kuona vituo vya mafuta , magorofa , magari na viwanja vingi kila kona ya Nchi bali Haki ,Usawa na utu vikiwa kama nguzo ya imani ya watawala wetu watakaokuwepo, pengine sitaishi miaka mingi sana kama utachukizwa sana na waraka wangu huu kwani Polisi , Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi wanakutii wewe , hata hivyo siogopi kufa kwani nisipokufa kesho , nitakufa siku moja ambayo siijui , napenda kuishi maisha marefu nimwone mke wa mtoto wangu kama itawezekana , lakini kuliko iwezekane kwa kuishi kwa hofu ni bora ishindakane kwa kuthamini haki , kwa hiyo kama utakuwa umekasirika sana , unaweza kufanya jambo lolote baya kwa kutumia mamlaka yako , niko tiyari sio kesho wala leo isipokuwa sasa hivi, najua IKULU imewazulumu watu wa Arusha Mbunge wao.
Mh Rais ninajua wazi njama zote na hasira hizi zinaweza kuwa zimetokana hasa na mkutano tuliokaa Osterbay Dar mimi na wewe kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 hata hivyo sikupuuza maongezi yetu isipokuwa nilichagua kufuata dhamira yangu na wito wangu wa utumishi wa kweli katika Jimbo langu na Nchi yangu.
Mh Rais nimekuelewa na Wananchi wamekuelewa kila mahali , wewe ni Rais unayo mamlaka makubwa na mimi ni mwananchi mamlaka yangu makubwa ni kwa mke wangu tu , sina Polisi wala Usalama wa Taifa lakini nitawaomba wanyonge wafunge na kusali tuone kama mamlaka yako inaweza kushindana na haki na ukweli .
Mh Rais “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” Serikali na Chama cha Mapinduzi kimepuuza watu na haki zao kwa muda mrefu , lakini wakati umefika ambapo hawatapuuzwa tena hata hivyo kwa kauli yako hii naamnini haiwezi kuwafundisha kazi majaji wa mahakama ya rufaa .
“ ONLY TIME WILL TELL”.
GODBLESS .J. LEMA.
Read more...

Saturday, June 2, 2012

ZANZIBAR UAMSHO `BUDDING NEW AL-SHABAAB`-TIPF WARNS

0 comments
Demonstrations was supposed to be peaceful until things came out of hand shortly afterwards. Here Uamsho senior leaders kick starting demonstration on the day of Zanzibar violence
Few days following last week Zanzibar violence, Tanzania Islamic Peace Foundation have urged government to take a closer look on the group Uamsho( THE AWAKENING)

Director of  TIPF Sheikh Sadik Godigodi was issuing the foundation`s statement condemning recent Zanzibar violence which saw arsonic acts against churches and looting

In its statement, the foundation expressed its concern that Uamsho has the same trend Somali extremist group Al-Shabaab had when it began. TIPF  also claimed to have full understanding of  religious movements in the island and refused to believe Uamsho denial that they are not responsible for the Zanzibar`s last week violence.TIPF see the violence as meaningless and abusive by damaging churches and looting shops because if nature of violence was political claims it is irony that religious and other non-political areas were involved.

Suspects being arrested during last week`s Zanzibar violence
Roads were blocked by rocks and bon fire until security forces interfered

Sheikh Godigodi said churches do not belong to neither goveenment nor any political party or NEC(National Electoral Commission) and TIPF understand that Uamsho was centered in organizing  open religious meetings aiming to providing islamic teachings to muslims and others interested people but they long  have been instilling hates instead


Muungano (the union of Tanganyika and Zanzibar) has been  strongly debated among Zanzibaris in recent years,questioning  interests of its being.The pact was installed by the then Tanganyika President late Mwalimu Nyerere and Zanzibar`s first president late Abeid Karume in late April of 1964,by mixing sands from either part.


Sheikh Godigodi urged Zanzibaris to realise that christianity and churches were run in the island since 1870,so they should stop questioning their elligibilities and connecting Zanzibar political problems with christianity.
Senior leaders of  Uamsho denying direct involvement in violence

"We,islams,know the history of Al-Shabaab.They set out by ignoring islamic teachings and installed their own ideas for their own interests under the shadow of islam."


He revealed that his foundation once had advised authorities to scrutinize movements of  Uamsho which they claimed was sowing discriminations within muslims in mosques.His foundation requested that government appoint a special committee to closely investigate the group, but the request had fallen into deaf ears.So they rested their case, warning that if anything serious happened,the government should not seek any excuse

Peace was restored in the island and tourists were back inthe streets of Zanzibar



Now the group has taken it all to the streets of  Zanzibar,chanting against Muungano while burning churches and looting along the way,shooing  mainlanders off the island, ignoring all constitutional principles set for any citizen to demonstrate their itching issues.

Sun is setting in Zanzibar
TIPF has also condemned individuals who have positioned themselves against Muungano citing that God Himself does not allow discrimination,racism and disunities.And that God also has implemented His own principles for people of different knowledges,colors,faiths and backgrounds to preserve respect amongst themselves.
Civilians were back to work few days after violence

The foundation urged muslims to live by principles of God while abiding with constitutional laws


Read more...

Friday, June 1, 2012

MAUAJI YA KUTISHA! VIFURUSHI VYENYE VIPANDE VYA MWILI VYAOKOTWA

0 comments
Kijana Lin Jun katiaka picha yake ya facebook,Jun alitoweka Mei 24 na kuripotiwa kupotea kwake Mei 29


Polisi nchini Kanada wanahangaika kumsaka mtu aliehusika na mauaji ya kinyama ya kijana raia wa China aliekuwa masomoni nchini humo.Kamanda wa Polisi wa jiji la Montreal Ian Lafreniere amesema wapelelezi wanaamini kuwa mauaji hayo yalifanyika siku ya Alhamisi au Ijumaa ya wiki iliyopita.


Lin Jun kijana kutoka China aliekuwa akisoma katika chuo kikuu cha Concordia alitoweka tangu Mei 24, na Mei 25 video ya kutisha inayoonyesha mauaji ya Lin iliwekwa kwenye internet.

Tarehe 26 Mei mtuhumiwa wa mauaji hayo Locco Luka Magnotto aliondoka jijini Montreal kwa  ndege kwenye uwanja wa Trudeau,lakini polisi wameshindwa kujthibitisha alielekea wapi,lakini polisim wanasema kuna uwezekano alirudi jijini humo na kujibadilisha


Tarehe 29 Mei ubalozi mdogo wa China  jijini Montreal uliweka tangazo  juu ya kutoweka kwa Lin kwenye mtandao wao na siku hiyo hiyo vifurushi vyenye vipande vya mwili wa Lin viliokotwa huko Ottawa na baadae sanduku lenye vipande vingine vya Lin lilikutwa nje ya  jengo la apartment mjini Montreal

Kwa mujibu wa taarifa za ubalozi huo Lin Jun ni mwenyeji wa jiji laWuhan nchni China, na alifika Kanada mwezi Julai mwaka jana kwa ajili ya kuchukua masomo ya uinjinia na sayansi ya kompyuta katika chuo kikuu cha Concordia.

Kwa mujibu wa watu waliomfahamu jijini Montreal, Lin mara nyingi alipenda kutumia majina ya Justin au Patrick kama ya ukoo muda wote aliokaa Kanada.


Msako wa kimataifa umeanzia nchini Ufaransa kumsaka mcheza picha za ngono Locco Luka Magnotto ambae inahisiwa kuwa ndie alieukatakata mwili wa mwanafunzi huyo na kisha kutuma vipande  vya mwili posta katika vifurushi


Nchini Ufaransa polisi wamesema wana uhakika Magnotto ametua nchini humo akitokea Montreal mwisho wa wiki iliyopita.Tayari kikosi maalum chenye wataalam wa kusaka wahalifu kimepewa amri ya kumsaka Magnotto.

Polisi jijini Montreal wanaamini Magnotto ndie aliemuua Lin,mtu ambae alikuwa na mahusiano nae,na kisha kuukatakata mwili wake na kuutia kwenye vifurushi kabla hajavituma vifurushi hivyo kwa njia ya posta hadi kwenye ofisi za vyama vikubwa viwili vya siasa nchini Kanada.


Polisi walitumia picha ya Lin kuwauliza watu wanaoishi kuzunguka jengo aliloishi Magnotto iwapo waliwahi kumuona Lin hapo.


Nao polisi wa kimataifa Interpol wameweka picha ya Magnotto kwenye mtandao wao juzi Alhamisi,ikiambatanishwa na picha za wahalifu wengine wa kimataifa wanaotafutwa kwa makosa ya mauaji,utekaji nyara na  kujihusisha na makundi ya uhalifu.

Interpol imekuja kushirikishwa katika sakata hili baada ya polisi wa Montreal kutoa kibali dunia nzima cha kukamatwa Magnotto.Ushahidi uliopatikana kutoka eneo la mauaji mjini Montreal umefanya polisi wapanue wigo wa msako kuwa wa kimataifa

Kamanda wa polisi wa Montreal, Ian Lafreniere.amesema "Kuna ushahidi tumeupata.Na pia tumepata barua ambayo iliwekwa kwenye mtandao wa kompyuta ambayo inatufanya moja kwa moja tuamini kuwa muhalifu amekimbilia nje ya nchi"



Kamanda Lafreniere pia amesema polisi wamekuwa wakishirikiana na maafisa wa uwanja wa ndege wa Montreal kupata taarifa zaidi, lakini amekataa kuweka wazi taarifa hizo."Hakuna nchi duniani ambayo hajatajwa" Lafreniere aliongeza,"Kwa hiyo ni lazima awe kwenye wakati mgumu"
Huyu ndie Locco Luka Magnotto mshukiwa wa mauaji ya Lin Jun
Read more...

DIAMOND NA NYUMBA YA MILIONI 69

0 comments

Hapa ni kwenye nyumba aliyopanga Sinza
.
Inawezekana ukawa una taarifa kwamba Diamond Platnums ni msanii mwenye mkwanja sana hapa Tanzania kutokana na show za bei gali na nyingi anazozifanya.
Inawezekana ukawa unataarifa kwamba Diamond Platnums ndio msanii ambae yuko juu kwa sasa Tanzania, na kwamba ndio msanii aliepiga show nyingi za bei ghali mwaka jana.
siyo hayo tu… kuna uwezekano ukawa una taarifa zake nyingi tu lakini hili ninalotaka kukwambia mimi ndio kwanza unalisoma kutoka hapa.
Kwenye show ya Big Brother Stargame Afrika Kusini akiimba wimbo wake `MAWAZO`
Akiongea na millardayo,Platnums amekubali kuzungumzia nyumba yake anayoijenga Tegeta Dar es salaam kutokana na pesa za muziki.
Amesema 
“ninapopata huwa najaribu kutengeneza vibanda vyangu vinisitiri manake ninazo nyumba tofauti tofauti, nyumba ya Tegeta nimetumia milioni 69 mpaka sasa, leo wanapiga plasta nyumba imekaribia kuisha kabisa, ni ya vyumba vinne; vitatu ni Master, kuna jiko kubwa tu, choo cha public, studio, dining room, sitting room… ni nyumba ya kisasa.Kiwanja nilikinunua mwezi wa tisa, 2011. Zipo nyingine ninazojenga, ila huwa sipendi kuzizungumzia”


Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797