Pages

 

Friday, June 1, 2012

DIAMOND NA NYUMBA YA MILIONI 69

0 comments

Hapa ni kwenye nyumba aliyopanga Sinza
.
Inawezekana ukawa una taarifa kwamba Diamond Platnums ni msanii mwenye mkwanja sana hapa Tanzania kutokana na show za bei gali na nyingi anazozifanya.
Inawezekana ukawa unataarifa kwamba Diamond Platnums ndio msanii ambae yuko juu kwa sasa Tanzania, na kwamba ndio msanii aliepiga show nyingi za bei ghali mwaka jana.
siyo hayo tu… kuna uwezekano ukawa una taarifa zake nyingi tu lakini hili ninalotaka kukwambia mimi ndio kwanza unalisoma kutoka hapa.
Kwenye show ya Big Brother Stargame Afrika Kusini akiimba wimbo wake `MAWAZO`
Akiongea na millardayo,Platnums amekubali kuzungumzia nyumba yake anayoijenga Tegeta Dar es salaam kutokana na pesa za muziki.
Amesema 
“ninapopata huwa najaribu kutengeneza vibanda vyangu vinisitiri manake ninazo nyumba tofauti tofauti, nyumba ya Tegeta nimetumia milioni 69 mpaka sasa, leo wanapiga plasta nyumba imekaribia kuisha kabisa, ni ya vyumba vinne; vitatu ni Master, kuna jiko kubwa tu, choo cha public, studio, dining room, sitting room… ni nyumba ya kisasa.Kiwanja nilikinunua mwezi wa tisa, 2011. Zipo nyingine ninazojenga, ila huwa sipendi kuzizungumzia”


0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797