Pages

 

Thursday, June 21, 2012

TAARIFA: KAGAWA KUFANYIWA VIPIMO OLD TRAFFORD KESHO

0 comments
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana,Shinji Kagawa anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya kesho Ijumaa pale Old Trafford ili dili lake la kujiunga na Manchester United kwa paundi milioni 17 liweze kukamilika.

Endapo Kagawa atathibitishwa kuwa fiti,Manchester United watakuwa na jukumu la kumtafutia kibali cha kufanya kazi nchini Uingereza,na baada ya hapo kila kitu kitakuwa kimekamilika.

 Lakini, ili kibali kipatikane, Kagawa anatakiwa awe ameshaichezea Japan asilimia 75 ya mechi za kimataifa kwa mwaka uliopita,lakini Kagawa hana sifa hiyo,hivyo basi sifa pekee ambayo Manchester United wanaweza kuitumia kupata kibali ni ile ya kipaji cha ziada,ambayo hata Arsenal waliitumia kwa Miyachi,mchezaji mwingine kutoka Japan.

Shinji Kagawa amaepata mafanikio katika misimu miwili iliyocheza kwenye ligi kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga.Ameichezea Borussia Dortmund mechi 71 na kufunga magoli 29,amechangia magoli 15,amebeba kombe la ligi kuu (Bundesliga) mara mbili na kombe la Ujerumani mara moja. 

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797