Pages

 

Tuesday, June 19, 2012

INGIA HUMU UONE KOMPYUTA MPYA YA KIGANJANI ILIYOZINDULIWA LEO NA MICROSOFT

0 comments



Kampuni ya Microsoft leo imezindua kompyuta yake ndogo ya kiganjani katika jitahada za kuipiku iPad inayotengenezwa na kampuni ya Apple.Kompyuta hiyo wanayoiita Surface inatumika kwa kugusa kwenye kioo cha kompyuta hiyo kama ilivyo kwa iPad


Kompyuta ya Surface ina muundo ambao una kifuniko kinachokunjuka na kuunda keyboard na kioo chake ni cha widescreen.Kio hicho cha Touchscreen kinaendeshwa na mfumo mpya wa kompyuta Windows 8 ambao Microsoft wanatarajiwa kutoa hivi karibuni,na pia mtumiaji wakompyuta hiyo anaweza kutumia processor yoyote kati ya Intel au ARM
Microsoft hawajataja bei ya kompyuta hiyo wala tarehe ya kuingia sokoni

0 comments:

Post a Comment

 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797