Pages

 
Showing posts with label sayansi. Show all posts
Showing posts with label sayansi. Show all posts

Monday, July 8, 2013

NYATI WA AJABU AONEKANA NGORONGORO

0 comments
Wakati magwiji wa Sayansi ya Maisha ya Viumbe hai duniani wakidhani wametegua vitendawili vyote kuhusu maisha ya Viumbe hai vya msituni,kimetokea kitendawili kingine katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro,ambako ameonekana aina ya nyati isiyowahi kuonekana  hapa duniani,mwenye rangi isiyozoeleka miongoni mwa nyati waliozoeleka

Kwa kawaida nyati huwa na rangi nyeusi,lakini huyu alieonekana Ngorongoro amepambwa kwa rangi nyeupe -maziwa,akiranda randa katika maeneo ya bonde maarufu duniani la Ngorongoro,na tayari ameshawavuta wanaharakati wa mazingira,wanasayansi wa maisha ya viumbe hai na watafiti wa tabia za wanyamapori ambao wako Ngorongoro kumfuatilia.

"Kwa kweli  aina hii ni adimu sana na ni tukio la ajabu kwa upande wa watu wanaoshughulika na maisha ya viumbe vya misituni,kwa hapa Ngorongoro na nchi nzima kama ninavyojua."Alikiri kiongozi wa watafiti wa maisha ya viumbe hai katika Hifadhi ya Ngorongoro Bw Patrice Mattay
 
Watu wa kwanza kumuona nyati huyo katika hifadhi ya Ngorongoro ni maafisa wa Polisi wa kituo cha hapo Ngorongoro,ambao mwanzo walidai mara kwa mara kuona aina ya wanyama wa ajabu katika eneo lao la kazi,hasa nyakati za alfajiri.

Afisa Polisi JJ Paul ambae alikuwa zamu amethibitisha kukiona kiumbe hicho,"mwanzo nilipata habari zakuonekana kwa mnyama wa ajabu kutoka kwa maafisa polisi wenzangu,na hivi karibuni nilimshuhudia huyu nyati akila majani akiwa amejichanganya na wanyama wengine kwenye ukingo wa bonde"

Inasemekana kuwa eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ina idadi ya nyati wa kawaida wapatao350 kati ya wanyama wapatao laki 3 wanaoishi ndani au kuzunguka bonde hilo kubwa na maarufu duniani.Lakini  huyu nyati mweupe ni aina ambayo haijazoeleka kuonekana katika jamii ya nyati ndani ya hifadhi hiyo.

Meneja anaehusika na hifadhi katika Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro Bw Amiyo T. Amiyo amesema kwamba ugunduzi huu wa nyati mwenye rangi nyeupe unahitaji wito wa kuanzisha aina mpya ya utafiti juu ya tabia za maisha ya wanyamapori.

Kawaida watafiti wengi waliegemea kwa jamii ya wanyama wanaokula nyama (carnivores) kama vile simba, mbwa-mwitu na cheetah,lakini sasa nyati wanaweza kuingia kwenye listi
Read more...

Tuesday, June 19, 2012

INGIA HUMU UONE KOMPYUTA MPYA YA KIGANJANI ILIYOZINDULIWA LEO NA MICROSOFT

0 comments



Kampuni ya Microsoft leo imezindua kompyuta yake ndogo ya kiganjani katika jitahada za kuipiku iPad inayotengenezwa na kampuni ya Apple.Kompyuta hiyo wanayoiita Surface inatumika kwa kugusa kwenye kioo cha kompyuta hiyo kama ilivyo kwa iPad


Kompyuta ya Surface ina muundo ambao una kifuniko kinachokunjuka na kuunda keyboard na kioo chake ni cha widescreen.Kio hicho cha Touchscreen kinaendeshwa na mfumo mpya wa kompyuta Windows 8 ambao Microsoft wanatarajiwa kutoa hivi karibuni,na pia mtumiaji wakompyuta hiyo anaweza kutumia processor yoyote kati ya Intel au ARM
Microsoft hawajataja bei ya kompyuta hiyo wala tarehe ya kuingia sokoni
Read more...

Sunday, May 20, 2012

`DOGO` BOSI WA FACEBOOK,MARK ZUCKERBERG, AFUNGA NDOA KWA STAILI SIKU YA JUMAMOSI

0 comments
Mwanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Facebook, Mark Zuckerberg, amefunga ndoa siku ya Jumamosi na rafiki yake wa kike  wa siku nyingi msichana mwenye asili ya China, Priscilla Chan.
Zuckerberg kijana bilionea mwenye umri wa miaka 28 alitangaza rasmi tukio hilo kwa washabiki wake wa Facebook kupitia Timeline yake


Wawili hao walianza mahusiano wakiwa Chuo Kikuu cha Harvard na wamekuwan imara kwa takriban miaka 9 sasa.Walilishana kiapo katika sherehe isiyokuwa kubwa upande wa nyuma wa nyumba yao huko Palo Alto,California.Kitendo hicho kilileta hali ya mshangao kwa wageni waalikwa wasiopungua 100,kwa mujibu wa  jarida la People,kwa kuwa wengi wao walidhani ni sherehe za kuhitimu kwa Priscilla,ambae tarehe 14 mwezi huu alipata shahada ya chuo kikuu ya elimu ya afya ya watoto kutoka Chuo Kikuu cha California cha San Fransisco(UCSF)

Hii ni Historia yake

Inasemekana Zuckerberg ndie aliebuni pete ya Priscilla ambayo ni ya kawaida tu iliyonakshiwa kidogo na chembe chembe za madini ya ruby,hata mavazi aliyovaa yalionekana kuwa `simple`
Add caption
Zuckerberg kijana ambaye anasifika kwa kufanya mambo yake `simple` alitoa taarifa za tukio hilo katika hali ya kawaida sana kwa kubadilisha status ya kwenye Timeline yake kutoka `in relationship` na kuwa `married`,status ambayo watu zaidi ya laki 8 wame `like` kwa masaa 24 iliyokaa mtandaoni.Muda mfupi baadae dada wa Mark aitwae Arielle aliandika katika facebook yake "Balls.Now I`m the only unmarried Zuckerberg." Na bibi harusi Priscilla nae alimuweka Arielle kama `family member` wake mpya

Kijana Mark Zuckerberg ana hisa zenye thamani isiyopungua dola za kimarekani bilioni 20.Kampuni yake ya Facebook ambayo kwa mara ya kwanza kabisa imeingia katika biashara ya hisa,imeanza  katika mnada wao wa kwanza uliofanyika Ijumaa kwenye eneo lao la Facebook Silicon Valley.Mnada wao wa awali haukwenda vyema kama matarajio ya kampuni yalivyokuwa huku kila hisa zikipnda bei kidogo tu kutoka bei ya mnada ya dola 38 kwa hisa na kuuza asilimia 25 tu ya hisa zao zote.Zaidi ya hisa milioni 576 ziliuzwa na kubadili rekodi ya soko la awali la hisa nchini Marekani.Mwaka jana Facebook iliingiza mapato ya dola za kimarekani bilioni 3.7 na kuvuna faida ya dola za kimarekani bilioni 1.Facebook ina watumiaji wamtandao huo wapatao milioni 900 duniani kote


Kuibuka kwa Facebook na kuleta maajabu ya kiutamaduni duniani kulipelekea kutengenezwa kwa filam iitwayo `Social Network` mwaka juzi.Zuckerberg alianzisha mtandao wa Facebook akiwa bwenini katika chuo alichokuwa akisoma cha Havard miaka minane iliyopita.
\
Si Zuckerberg wala Chan ambao wameongezea chochote kwenye facebook zao kuhusu ndoa yao na watu wa habari wamekuwa wakituma e-mail kwa wahusika katika kampuni ya Facebook ili kupata ufafanuzi zaidi,lakini hazijajibiwa.

Read more...

Thursday, May 17, 2012

MAREKANI YARUHUSU DAWA MPYA YA KUZUIA UKIMWI IANZE KUTUMIKA

0 comments
MAMLAKA ya Chakula na Dawa ya Marekani (FDA), imeidhinisha dawa ya Truvada kuwa tiba ya kuzuia kuenea kwa Virusi Vya Ukimwi (VVU).Dawa hiyo ambayo awali ilikuwa katika kundi la zile zinazotumiwa kwa ajili ya Kupunguza Makali ya VVU (ARV), imepandishwa chati wakati ambapo tayari ipo sokoni ikiuzwa kama moja ya ARV za kawaida.

Kwa mujibu wa maelezo ya FDA, mwathirika anayetumia dawa hiyo anaweza kujamiiana na mwenza wake ambaye hana VVU bila kutumia kondomu na hatomuambikiza.

Matokeo ya utafiti huo yaliwahi kuchapishwa kwenye gazeti hili toleo la Februari 12, mwaka huu na sasa kilichofanyika ni FDA kuidhinisha Truvada ambayo ilionyesha kufanya kazi vizuri ikilinganishwa na ARV nyingine.

Uidhinishaji wa dawa
Jopo la wanasayansi 22 wa FDA waliokutana Jijini Washington wiki iliyopita, walipitisha Truvada baada ya kupitia ripoti ya utafiti kuhusiana na ufanyaji kazi wa dawa za ARV.

Wanasayansi hao waliisifu dawa hiyo baada ya kuonekana kufanya kazi vizuri kwa watu waliopo kwenye hatari ya kuambukizana VVU kwa kasi zaidi.

Kwa namna dawa hiyo inavyofanya kazi, mwathirika akiitumia hawezi tena kumwambukiza mtu mwingine ambaye atashiriki naye tendo la ndoa bila kutumia kondomu.

Lakini, dawa hiyo masharti yake hayatofautiani na yale ya ARV kwani mtumiaji atapaswa kuitumia maisha yake yote ili kumwekea kinga asiwaambukize wengine na yeye aishi muda mrefu.

Kulingana na ripoti ya utafiti uliofanyika Marekani, dawa hiyo ina uwezo wa kuzuia maambukizi ya VVU hadi asilimia 90.Hata hivyo, kwa watu ambao wamekuwa wakitumia dawa holela hasa za ARV, hali imekuwa tofauti kwani Truvada imeonekana ikifanya kazi kwa kiwango cha asilimia 44 tu.

"Hii ni ishara kwamba kuna kundi la watu ambao dawa hiyo haitafanya kazi kikamilifu kutokana na mazingira ya matumizi ya dawa holela,"ilisema sehemu ya ripoti.

Hata hivyo, wanasayansi wanasema  tatizo hilo linafanyiwa uchunguzi ili kupata njia bora ya kukabiliana na tatizo hilo.

Faida ya Truvada
Wataalamu wameeleza kwamba itasaidia watu ambao wana VVU lakini, hawapendi kufanya tendo la ndoa kwa kutumia kondomu."Leo ni siku ya tukio la kuwasisimua wengi katika kuzuia maambukizi ya HIV,” alisema mmoja wa wataalamu kutoka Taasisi ya kujitolea kusaidia jamii ya Fenway, Dk Kenneth Mayer ambaye alikuwa miongoni mwa wajumbe wa FDA walioipitisha dawa hiyo.

"Ingawa (Truvada) haikuweza kuonyesha uwezo wa asilimia 100 kuzuia maambukizi ya VVU, namna inavyofanya kazi itakuwa na matokeo mazuri ya kupambana na Ukimwi duniani,” alisema Dk Mayer.

Tahadhari
Hata hivyo, wataalamu hao walihimiza kuwepo kwa uchunguzi zaidi wa kitafiti ili kujua kama Truvada itafanya kazi vizuri duniani kote.Mtaalamu wa Dawa kutoka Taasisi ya Taifa ya Saratani nchini Marekani (NCI),  Dk Lauren Wood alilalamika akisema kuwa utafiti huo haukuzingatia matatizo ya figo.

Alisema matatizo ya figo yamekuwa yakijitokeza kwa waathirika wengi wa Ukimwi hasa barani Afrika."Mimi sikufurahishwa sana kwa sababu utafiti huu haukuzingatia maeneo ambayo watu wengi wako kwenye hatari ya maambukizi,” alisema Dk Wood.

Lakini, alisema utafiti uliofanyika nchini Marekani umeonyesha wazi kwamba ni dawa inayoweza kupunguza kwa kiwango kikubwa kasi ya kusambaa kwa VVU.

Wataalamu kadha nao walisema pamoja na Truvada kupitishwa na FDA, ni lazima maelezo ya kitaalamu yatolewe kwa madaktari ili wawe na uelewa wa kutosha kuhusu matumizi yake.

Mabingwa hao walipendekeza kwamba, wanaotumia kabla ya kuruhusiwa kutembea na wenzi wao bila kondomu lazima wachunguzwe kitaalamu ili wajulikane kama dawa iyo imewakubali au la.

Mwanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Afya cha Cincinnati, Dk Judith Feinberg alikosoa ripoti ya uchunguzi akisema ilipaswa kwenda mbali zaidi katika kuchunguza madhara yanayoweza kujitokeza kwenye matumizi ya dawa hiyo.“Tusipokuwa makini katika hilo, tunaweza tukawa tumepitisha jambo ambalo litasababisha madhara zaidi kuliko faida,” alionya Dk Feinberg.


Utafiti wa ARV
Wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Johns Hopkins ni miongoni mwa wale ambao walifanya uchunguzi juu ya ARV, kuwa moja ya dawa zinazopunguza maambukizi ya VVU.

Watafiti hao walibainisha kuwa wale wanaotumia ARV baada ya muda fulani, huweza kushiriki tendo la ndoa bila ya kutumia kondomu na mtu ambaye hana VVU na asimwambukize kwa asilimia 95.

Mkuu wa Mtandao wa Maabara za Kuchunguza VVU katika chuo hicho, Profesa Susan Eshleman alisema kwenye ripoti ya ugunduzi huo, wamebaini dawa za kurefusha maisha kwa waathirika wa HIV, sasa zinaweza kutumika kama sehemu ya kuzuia maambukizi.

Profesa Eshleman alisema kwamba, mwathirika wa VVU anayetumia ARV kikamilifu, anaweza kujamiiana na mtu ambaye hana virusi bila kondomu na asimwambukize.

“Huu ni ugunduzi wa kustajabisha,” alisema Profesa Eshleman akifafanua: “Matokeo haya yameleta mapambazuko mapya katika sayansi ya kuzuia maambukizi na inawaweka watafiti kwenye mazingira mazuri zaidi ya kupata suluhisho la kukabiliana na maradhi haya.”

Walivyogundua
Profesa Eshleman anasema utafiti huo walioupa jina la HPTN 052, walifanya kupitia maeneo mbalimbali ya dunia.

Kwenye ripoti hiyo ambayo pia ilichapishwa kwenye jarida maarufu la kisayansi linaloitwa Science, watafiti hao walisema mtu anapotumia ARV, hufikia wakati fulani wingi wa virusi mwilini hupotea kiasi kwamba anakuwa karibu sawa na yule ambaye hajaambukizwa.

“Jambo la msingi katika utafiti huu ni kwamba dawa hizi za kurefusha maisha zinapotumiwa kikamilifu, hupunguza mzigo wa virusi mwilini kwa zaidi ya mara 200. Ni sawa na kusema inapunguza hadi kufikia karibu na sifuri,” inaeleza ripoti hiyo.

Ni katika mazingira hayo, ripoti hiyo inasema kuwa damu ya mwathirika inakuwa haina virusi na hivyo uwezekano wa kumuambukiza mpenzi wake unakuwa haupo.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa ARV inafanya kazi mbili, kwanza kurefusha maisha ya mwathirika kwa kupunguza virusi mwilini na pili ni kumkinga asiambukize wengine.Sifa nyingine ya ARV, alisema ni kupunguza uwezekano wa waathirika kupata ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) kutokana na kiwango cha kinga za mwili kuongezeka.
SOURCE: mwananchi.co.tz
Read more...

Friday, May 4, 2012

RIPOTI ILYOKWENDA SHULE;MADHARA YA KUTUMIA OVYO FACEBOOK HAYA HAPA:

0 comments
Watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii hawajui madhara ya matumizi holela ya mitandao hiyo au hawataki kujihadhari na hatari zinazowakabili,ripoti imetolewa jana mjini Washington katika jarida la taasisi isiyo ya kiserikali, Consumer Reports

Ripoti hiyo inasema watumiaji wapatao 13 milioni wa Marekani hawajui au hawataki kutumia nyenzo za kujiweka salama kwenye mtandao wa facebook.Uchunguzi unaonesha kuwa wamarekani wapatao 4.5 milioni huwa wanaandika kwenye facebook wapi watakwenda na muda gani katika siku fulani na hii ni njia mojawapo ya kuwataarifu watu wabaya wanaoweza kudhuru,na pia kuna idadi nyingine ya wamarekani 4.7 milioni ambao wame `like` page zinazohusu mambo ya afya na tiba na kutoa taarifa za afya zao,bila ya kutambua kuwa kufanya hivyo ni kuyanufaisha makampuni ya bima.

Ripoti inaendelea kudokeza kuwa ni asilimia 37 tu ya watumiaji wa facebook ndio waotumia nyenzo za usalama wa taarifa zao kwenye facebook
"Facebook kwa kweli ni mtandao ambao kwa kiasi kikubwa umebadilisha namna watu wanavyoweza kuwasiliana duniani, na imekuwa huduma ambayo inafanikisha kwa kiwamgo kikubwa usambaaji wa taarifa binafsi za mtumiaji kwa umbali ambao hata mtumiaji mwenyewe hawezi kuamini"
Ripoti hiyo inaendelea kusema kuwa mwaka jana familia zipatazo 7 milioni zinazotumia mtandao wa facebook zimeripotiwa kuingia kwenye matatizo kutokana na facebook,matatizo kama vile watu wengine kuingia kwenye akaunti zao bila wao kujua,kusumbuliwa na kutishwa

"Uchunguzi wetu umegundua mambo ya kustaajabisha ambayo si ya kuyakalia kimya-lakini ni vyema wale wanaotaka kuziweka taarifa zao salama zaidi wajue"
Uchunguzi unaonesha kuwa facebook inakusanya taarifa nyingi za watumiaji pengine bila watuimiaji wenyewe kujua

Mtumiaji atashangaa kufahamishwa kuwa facebook wanakusanya taarifa kila anapoingia kwenye website yenye alama ya `like` bila kujali iwapo amebonyeza  alama au la...au ana akaunti ya facebook, au hata kama haja log in

Wachunguzi hao wamewashauri wamiliki wa facebook kulichukulia suala la usalama wa taarifa za watumiaji kwa umakini kwa kuweka nyenzo zitakazo dhibiti watumiaji wajanja.Pia wametahadharisha kuwa taarifa za watumiaji zinapochukuliwa ni jambo la hatari

Watumiaji walioulizwa mikakati yao katika kuweka salama taarifa zao kwenye facebook walitoa majibu ya kustaajabisha,robo yao huwa wanaweka taarifa  za uongo kwenye akaunti zao za facebook,ikiwa ni pamoja na  majina na tarehe za kuzaliwa

Idadi ya watu waliokiri kutumia taarifa za uongo imeongezeka maradufu ukilinganishwa na miaka miwili ilyopita swali hilo hilo lilipoulizwa,ingawa kisheria kitendo hicho ni kinyume na mkataba wa matumizi ya facebook

Mtandao wa facebook unasubriwa kwa hamu kubwa utakapoingia kwenye soko la hisa kwa mara ya kwanza wiki chache zijazo na kutarajiwa kuuza hisa zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 10,ikiwa ni kiasi kikubwa zaidi kuwahi kuuzwa na kampuni za internet katika soko la hisa la Wall Street

Idadi ya watumiaji wa facebook duniani imeongezeka na kufikia milioni 901 hadi ilipofika robo ya mwaka kwa mujibu wa nyaraka za kampuni hiyo.
Kwa taarifa zaidi tembelea link hii  http://www.consumerreports.org/cro/magazine/2012/06/facebook-your-privacy/index.htm
Read more...

Tuesday, May 1, 2012

MWEZI KUSOGEA KARIBU NA DUNIA JUMAMOSI HII

0 comments


Taswira kubwa kabisa ya uso wa mwezi kwa 2012 itaonekana Jumamosi hii.Kwa mujibu wa wataalam wa mambo ya anga za mbali mwezi utaonekana kuwa karibu zaidi usiku wa tarehe 5 mwezi huu na  kwa sababu
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797