Pages

 

Tuesday, July 9, 2013

AGNES MASOGANGE ANASWA NA MADAWA YA KULEVYA `SAUZI`

0 comments
HATIMAYE  wale Wanawake wawili walionaswa  na  madawa ya  kulevya  Afrika  kusini wametambuliwa kuwa  ni  mabinti  wa  KITANZANIA ..


Mabinti  hao  wanaodaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevya zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania.

Akizungumza na mwandishi wetu  jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.

Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Jerald (MASOGANGE)  ambaye alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24. Wawili hao bado wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.

Alisema Jeshi la Polisi Nchini kwa upande wake linaendelea kufanya uchunguzi kubaini kama dawa hizo walitoka nazo wapi na pia linawasaka watu ambao watakuwa ndiyo wamiliki wa dawa hizo.

Jumapili iliyopita mtandao huu  ulipata taarifa za kukamatwa kwa dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani hiyo nchini Afrika Kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania.

Taarifa hizo zilionyesha kuwa wanawake wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oriver Tambo uliopo eneo la Kempton Park siku ya Ijumaa wiki iliyopita wakitokea Tanzania.

Wanawake hao walikamatwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini wakiwa na masanduku sita ambayo yalipokaguliwa yalikutwa na takribani kilo 150 za dawa hizo ambazo pia zinajulikana kama ‘Tik’ zikiwa na thamani ya bei ya mtaani ya Randi milioni 42 sawa na Sh. bilioni 6.8.

Baada ya kukamatwa na dawa hizo wanawake hao walikabidhiwa polisi. Tukio hilo linatoka takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Juni 28, mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulenya hivi sasa ni janga la kitaifa nchini.

Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.

Pia alisema katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.

Pinda alisema mwaka huu pekee kumekuwa na ukamataji mkubwa wa dawa za kulevya katika eneo la kimataifa la Bahari ya Hindi karibu na Tanzania.
 


Alisema hivi sasa mikate, maandazi na askrimu zinazouzwa kwenye shule za msingi, zinawekwa dawa za kulevya.

Alisema vitendo hivyo vinafanya vijana wengi wa shule za msingi na hata sekondari kuwa na tabia za ajabu, ikiwamo kuingia darasani wakiwa na kiatu kimoja mguuni, mkufu wenye nyembe na kidani chenye nyembe kifuani.


CHANZO: LEWIS MBONDE
Read more...

SHULE ZIMEFUNGULIWA JANA, KIDATO CHA TANO BADO HAWAJATANGAZWA!

0 comments

Matokeo mabaya ya kidato cha nne ya mwaka 2012, yameendelea kuitikisa sekta ya elimu nchini baada ya shule kufunguliwa jana bila kutangazwa kwa waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu.


Kwa kawaida, wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ualimu, hutangazwa mapema ili kutoa fursa kwa wanafunzi na shule husika kufanya maandalizi ya mahitaji.


Lakini tofauti na ilivyozoeleka, wanafunzi wa kidato cha sita walianza masomo yao jana huku wale wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ualimu wakiwa hawajatangazwa.


Mkanganyiko huo pia unazigusa shule za sekondari za binafsi kwani baadhi zilishachukua wanafunzi wa kidato cha tano na nyingine ziliahirishwa kufunguliwa jana kutokana na kutokuwa na wanafunzi hao.


Hali hiyo imewaacha njia panda baadhi ya wakuu wa shule ambao waliwaambia waandishi wetu kwa nyakati tofauti kwamba wanasubiri maelekezo ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuhusu suala hilo, huku wengine wakitishia kufunga shule hizo na kuzigeuza kuwa vyuo vya taaluma nyingine.


Akitangaza matokeo mapya ya kidato cha nne Mei mwaka huu, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa aliahidi kwamba majina ya watakaojiunga na kidato cha tano yangetangazwa mapema ili wapate muda wa kujiandaa na kuripoti kwenye shule husika mapema kadri itakavyowezekana.


Jana, Dk Kawambwa hakupatikana kuzungumzia suala hilo na msemaji wa Wizara hiyo, Bunyanzu Ntambi alisema suala la kutangaza majina hayo lipo kwenye ngazi za uamuzi.


“Sababu hasa siwezi kujua, lakini kwa kuwa matokeo yenyewe yalichelewa kutangazwa ni rahisi hata mchakato wa kutangaza waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano uchelewe,” alisema Bunyanzu.


Wakuu wa shule

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Morogoro, Thomas Chihwalo alisema: “Ninachosubiri ni maelekezo ya wizara, nini kifanyike.”


Mkuu wa Sekondari ya Azania, Dar es Salaam, Benard Ngoyaye alipoulizwa alisema: “Nenda kwa Ofisa Elimu wa Wilaya, yeye anafahamu kwa nini majina yamechelewa kufika wakati walikwishachaguliwa.” 

Mkuu wa Shule ya Sekondari Arusha, Christopher Malamusha alisema walitarajia wizara ingetangaza majina hayo mapema lakini hadi jana walikuwa hawajapokea taarifa zozote.


Mkuu wa Sekondari ya Tambaza aliyejitambulisha kwa jina moja, Zuberi naye alisema wanasubiri maelekezo ya Ofisa Elimu Wilaya ya Ilala.

Hata hivyo, Ofisa Elimu ya Sekondari wa Manispaa ya Ilala, Germana Mng’aho alisema asingeweza kuzungumzia suala hilo na kwamba mhusika mkuu ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

 Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ilboru, Arusha, Julius Shula alisema hata majina ya wanafunzi wanaojiunga na shule yao hawayafahamu.

Mmoja wa walimu wa Shule ya Sekondari ya Jangwani, Dar es Salaam, alisema kwa kawaida wanafunzi wa kidato cha tano huripoti shuleni wiki mbili kabla ya wale wa kidato cha sita kitu ambacho mwaka huu kimekuwa tofauti. 
 
Msaidizi wa Mkuu wa  Shule ya Sekondari Bwiru Wavulana ya Mwanza, Malongo Charles alisema wanasubiri wanafunzi watakaopelekwa na Serikali.

Hata hivyo, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Moshi, Fanuel Angalo alisema anaamini wizara husika itatangaza wiki hii.

“Ni jambo jipya kidogo limetokea lakini tunaamini Waziri atatoa tangazo lake wiki hii halafu wanafunzi hao wa kidato cha tano waripoti shuleni wiki ijayo,” alisema Angalo.

Mkoani Tanga, walimu katika Shule za Sekondari za Tanga Ufundi, Gallanos na Usagara kwa nyakati tofauti, waliilalamikia wizara kwa kuwachelewa kuwapelekea wanafunzi wa kidato cha tano na kusema kuwa hiyo imevuruga utaratibu wa ufundishaji.

Hakuna athari
Baadhi ya wadau wa elimu walisema kilichotokea si kigeni kwani kimepata kutokea miaka ya nyuma na mihula ilirekebishwa na kwenda sawa na wenzao ambao walikuwa wameanza masomo.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Ushauri wa HakiElimu, Nyanda Shuli alisema kubadilika kwa muhula wa kuanza masomo si jambo kubwa ambalo linaweza kuathiri elimu na kwamba anaamini wizara itakuwa imetoa mwongozo.
 
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk Kitila Mkumbo alisema si mara ya kwanza kwa muhula wa masomo kubadilika kwani imewahi kutokea siku za nyuma na marekebisho yakafanywa ili kufidia muda ambao wanafunzi wanakuwa wamepishana na wenzao.

“Sidhani kama ni jambo kubwa sana ambalo linaweza kuathiri chochote katika masuala ya elimu, la msingi ni kuhakikisha kuwa waliochelewa kuanza masomo wanapata muda wa kumaliza mtaala (mtalaa) wa masomo kama inavyotakiwa.”

Kwa siku tatu mfululizo, kuanzia Juni 29, mwaka huu, wakuu wa shule za sekondari za Serikali walikutana katika Chuo cha Ufundi, Arusha kupitia majina ya waliochaguliwa na kuiachia kamati ya kukamilisha kazi hiyo.

Hata hivyo, habari kutoka ndani ya kikao hicho zinasema tatizo kubwa lilikuwa ni idadi ya wanafunzi kuwa ndogo ikilinganishwa na nafasi za kidato cha tano kutokana na kufeli kwa wanafunzi wengi katika matokeo ya kidato cha nne, 2012.

Hata baada ya matokeo hayo kufanyiwa marekebisho, idadi ya wenye sifa za kuchaguliwa ni ndogo ikilinganishwa na mahitaji halisi.

Mara nyingi, wanafunzi walio katika nafasi kubwa ya kuchaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano ni wale waliofaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu. 

Kwa sasa shule za Serikali zenye kidato cha tano zina uwezo wa kuchukua wanafunzi 45,000 kwa wakati mmoja.

Baada ya matokeo ya kidato cha nne kurekebishwa, wanafunzi waliofaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu ni 35,349; daraja la kwanza ni 3,242, daraja la pili ni 10,355 na  daraja la tatu ni 21,752.

 Ikiwa wanafunzi hao wote watachaguliwa kujiunga na kidato cha tano, bado shule hizo zitakuwa na upungufu wa zaidi ya wanafunzi 9,000.

Upungufu huo hautakuwa na athari kwa shule hizo pekee, bali hata kwa vyuo vya ualimu na vile vya kati ambavyo hupokea wanafunzi waliohitimu kidato cha nne na kufaulu. 

Mwaka jana, wanafunzi 31,516 walichaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika shule 201 za Serikali.

Idadi hiyo ni karibu asilimia 60 ya shule 495 ambazo kwa mujibu wa takwimu za Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), zilifanya mitihani ya kidato cha sita mwaka huu. Takwimu hizo pia zinaonyesha kuwa idadi ya watahiniwa wa shule waliosajiliwa kufanya mtihani huo ni  43,231.

 Kwa maana hiyo, ikiwa shule za Serikali zitachagua idadi sawa na ile ya mwaka jana, (31,516) kwa ajili ya kujiunga na kidato cha tano, shule binafsi 294 zitalazimika kugawana wanafunzi 3,833 watakaobaki.


Shaka ya wadau
Kutokana na idadi ya wanafunzi wanaofaulu mtihani wa kidato cha nne kuendelea kushuka kila mwaka, Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi Tanzania (TAMONGSCO), Mahmoud Mringo alisema asilimia 70 ya shule zenye kidato cha tano zimefungwa ama kupunguza idadi ya wanafunzi.

Mringo alisema matokeo ya hali hiyo yanaonekana kwenye yale ya kidato cha sita yaliyotangazwa Mei 31, mwaka huu ambayo baadhi shule kongwe zilizokuwa zinafanya vizuri miaka ya nyuma, zilishika nafasi za mwisho akisema hali hiyo imekuwapo kwa miaka minne mfululizo.

“Shule za private (binafsi) asilimia 70 ama wamefunga au wamepunguza udahili wa wanafunzi, kwa ufupi wameanza kujitoa kwenye hii bishara ya shule, shule kama ya Green Acres na St. Mary’s kushika nafasi za mwisho ni kiashirio cha kuwa walishaanza kujitoa kwenye hiyo biashara,” alisema.

Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Raida, Profesa Ruth Meena alisema wameamua kutochukua tena wanafunzi wa kidato cha tano kuanzia sasa na baada ya walio kidato cha sita kuhitimu, wanafikiria kuifanya taasisi hiyo kuwa chuo.

Meneja wa shule hiyo, Anneth Meena alisema: “Kila mwaka idadi ya ufaulu inashuka na wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano wanakosekana, sisi waliomaliza kidato cha sita mwaka huu walikuwa ni ishirini na kitu na wanaoingia kidato cha sita sasa hivi ni 21.”

Alisema wakati hali ikiwa hivyo miundombinu ya shule hiyo yenye kidato cha tano na sita pekee ina uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 400.


Hofu vyuo vikuu
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Profesa Gaudence Mpangala alisema kwa jinsi hali ilivyo siku zijazo kutakuwa na upungufu mkubwa wa wanafunzi wenye sifa za kwenda vyuo vikuu.

Alisema kutokana na matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012, alitegemea kuona bajeti ya elimu kwa mwaka 2013/14 inajielekeza kutatua matatizo yanayojulikana na yale yatakayoainishwa na Tume ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kitu ambacho hakijafanyika.

“Nilitegemea resources (rasilimali) nyingi zingeelekezwa kwenye kutatua matatizo ya elimu yanayojulikana na yale yasiyojulikana, lakini bajeti ya elimu ni ndogo kama miaka mingine, wakati ya Kenya ikiwa ni asilimia 18 na Uganda ikikaribiana na hiyo kwetu ni asilimia 10,” alisema na kuongeza:

Msemaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Edward Mkaku alisema kufeli kwa wanafunzi wengi ngazi za shule siyo sababu ya kufanya vyuo hivyo vifungwe kwani taasisi hizo zina kazi kuu tatu ambazo ni kufundisha, kufanya utafiti na kushauri.

Alisema pia kuwa, TCU imeanzisha programu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuruhusu hata watu walioishia darasa la saba na kufanya kazi muda mrefu kwenye maeneo mbalimbali kujiunga na vyuo vikuu.

“Kuna mtu alimaliza darasa la saba na akaenda kusoma cheti cha sheria, huyu mtu kafanya kazi kama karani wa Mahakama ya hakimu mkazi kwa miaka minane, huyu mtu ukimwingiza kusoma sheria na mwanafunzi aliyetoka kidato cha sita lazima afanye vizuri zaidi,” alisema.
CHANZO:GAZETI LA MWANANCHI
Read more...

ALINUSURIKA KUFUNGWA KWA KUMCHEKESHA RAIS HADI AKAANGUKA!

0 comments

Muasisi wa TANU Mustafa Mohammed Songambele amesema aliwahi kunusrika kufungwa kwa sababu ya kumchesha rais, Mwalimu Julius Nyerere.

Akizungumza na baadhi ya wafanyakazi katika Idara ya Itikadi na Uenezi, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam jana, Songamebele (88), alisema, mwaka 1970, wakati huo akiwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na pia Katibu wa TANU wa mkoa huo, alienda nyumbani kwa Mwenyekiti wa Chama, Mwalimu Nyerere, kwa ajili ya mazungumzo maalum.

Alisema, wakiwa katika mazungumzo alitamka maneno ambayo yalimfanya Mwalimu Nyerere kucheka hadi kudondoka sakafuni huku akibubujiwa machozi kwa kicheko.

Mzee Songambele alisema, baada ya rais kuondoka kwenda ofisini kwake, maofisa usalama walimsogelea na kumhoji kwa nini umemchekesha rais mpoaka amedondoka chini? Yaani ulitaka Rais afe halafu tupate tatizo la kutoa maelezo kwamba wewe umemchekesha hadi kufa? inabidi tukukamate uwekwe ndani.

Alisema, baada ya Walinzi kusema, hayo alilazimika kujitetea akisema "Mimi nilizungumza tu, sikuwa najua kwamba Mwalimu atacheka sana kiasi kile, sasa hili siyo kosa langu naomba mnisamehe".

"Nilipoona wanatafakari kidogo nilipanda ngazi hadi ofisini kwa rais, nikamkuta, akasema, 'bwana nimeshacheka sana inatosha basi", nikamwambia Mwalimu mimi sikuja kukuchekesha tena, lakini tazama hawa walinzi wanataka kuniweka ndani kwa sababu wewe umefurahi ukacheka, sasa nimefanya kosa gani?", aliseleza Mzee Songambele.

Alisema, baada ya Mwalimu kusikia malalamiko hayo, aliwaita walinzi na kuwaamuru wamwache huru ndiyo ikawa salama yake, akaondoka.

Akizungumza na wafanyakazi hao, Songambele alikitabiria Chama Cha Mapinduzi kuendelea kutawala kwa muda mrefu licha ya kuwepo kwa vyama vingi, akisema uhakika huo unatokana na CCM kuwa na historia ambayo kufutika kwake si rahisi.

Songambele aliwataka CCM kujiimarisha zaidi ili kuendeleza misingi hiyo ya Chama kwa ajili ya kuhakikisha hakiyumbi wala kuyumbishwa kwa namna yoyote na wimbi la upinzani na kwamba kujenga misingi hiyo, vijana wana nafasi kubwa zaidi.
Read more...

Monday, July 8, 2013

BAYERN YATANGAZA RASMI MARIO GOMEZ KUJIUNGA NA FIORENTINA

0 comments
Mabingwa Soka Barani Ulaya kwa ngazi ya vilabu,Bayern Munich imetangaza rasmi kuachana na mshambuliaji Mario Gomez na kwamaba wamefikia makubaliano na timu ya Forentina ya Italia ambao wamekuwa wakimfuatilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kwa muda sasa.Mchezaji huyo alipokonywa nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza cha Mabingwa hao wa Ujerumani na mshambuliaji mwingine Mario Mandzukic.

Wiki iliyopita Bayern walisema kuwa mpango wa Gomez kwenda Fiorentina umekufa huku ikiripotiwa kuwa Fiorentina hawakuwa tayari kutoa kitita cha euro milioni 20 walizotaka Bayern.

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Bayern amesema uhamisho wa mchezaji huyuamabao unatajwa kuwa utakuwa hadi 2017, utasainiwa katika wiki moja au mbili zijazo na katika mkataba wake Gomez anatarajiwa kuvuna kitita cha euro milioni 4 kila msimu Gazeti moja la Italia Gazetta Dello Sport limandika kuwa Fiorentina watatoa euro milioni 15 kumnyakua mchezaji huyo

Mkataba wa Gomez na Bayern ulikuwa unaenda hadi 2016,lakini katika kile kilichoelezwa kukasirishwa kwa fowadi huyo na kitendo cha kutopangwa mechi nyingi za msimu uliopita.Kocha Jupp Heynckes alikuwa akimtumia Mandzukic mara kwa mara.Aliomba auzwe timu nyingine ili apate nafasi ya kucheza na kujihakikishia nafasi ya kwenda Kombe La Dunia Brazil 2014 .

Ingawaje hakupngwa mechi nyingi Gomez alifanikiwa kufikisha idadi ya magoli 19 msimu ulioisha yakiwamo mawili aliyofunga kwenye fainali ya Kombe la Ujerumani

Mchezaji huyo amebatizwa jina la Super Mario,linalotokana na kikaragosi cha kwenye mchezo wa kompyuta.Alijiunga na Bayern Miunich mwaka 2009 akitokea VfB Stuttgart kwa ada ya uhamisha ya euro milioni 35.Ameifungia timu ya taifa ya Ujerumani magoli 25 katika mechi 58 alizocheza.
Read more...

TAHADHARI:USINYWE MAFUTA YA UBUYU NI HATARI

0 comments
  Mamlaka inayosimamia ubora wa Vyakula na Madawa nchini TFDA imeutahadharisha umma wa Watanzania juu ya hatari inayoweza kuwakuta watu wanaokunywa mafuta ya ubuyu kama tiba.

Mbuyu ambao kisayansi unajulikana kama Adansonia Digitata,Nimmea wa jamii ya miti na umetapakaa sehemu nyingi duniani na watu hutumia matunda ya mti huu kuburudisha mdomo,kuanda juisi na hivi karibuni umeingia kwenye dawa za asili zenye uwezo wa kutibu maradhi mbalimbali kwa wakati mmoja.

Pia mamlaka hiyo imeonya watu dhidi ya tabia ya kutumia dawa bila kupata ushauri wa kitaalam kutoka kwa mtaalam aliesomea mambo ya dawa za binadamu

Mamlaka hiyo iliyopewa dhamana ya kusimamia ubora wa chakula na dawa nchimi,imetahadharisha juu ya matumizi holela ya dawa za aina ya Diclopa na Diclofenac,ambazo watu wengi hutumia kukabiliana na maumivu,kwa kuwa huwa zinasababisha matatizo mwili kwa baadhi ya watumiaji.

TDFA pia imeshauri watanzania kuendelea kutumuia mafuta ya ubuyu kama vipodozi tu na sio kunywa.

Akiongea katika maonesho ya 37 ya Kimataifa ya Biashara jijini Dar Es Salaam,msemaji wa TDFA Bi Gaudensia Simwanza amesema watanzani waache kunywa mafuta ya ubuyu

Baadhi ya wachuuzi wa mafuta hayo wanadai kuwa dozi ya mafuta hayo ambayo hupimwa kwa kijiko kidog cha chai inauwezo wa kutibu maradhi tofauti,ikiwemo Shinikizo kubwa la damu,kisukarina matatizo ya tumbo.

Bi Simwanza amesema baada ya kufanyia vipimo mafuta hayo,imegunduliwa kuwa yana kemikali hatari ambazo hazitakiwi ziingie ndani ya mwili wa binadamu na hivyo kufanya mafuta hayo yasifae kunywa hadi kemikali hizo zitakapokuwa zimeenguliwa kutoka kwenye mafuta hayo.

Amesema teknolojia ya kuondoa kemikali kutoka kwenye mafuta hayo kwa sasa haipo hapa nchini,hivyo watu waache kunywa mafuta hayo hadi teknolojia hiyo itakapopatikana

"Hivi karibuni taifa limekuwa likishuhudi a kukua kwa biashara ya mafuta ya ubuyu.Wafanyabiashara wamekuwa wakizunguka kila kona wakiyatangaza kuwa yana uwezo wa kutibu maradhi mengi kwa dozi moja.Tunataka umma utambue kuwa anaekunywa mafuta hayo ana hatarisha maisha yake..kuna aina ya acid ambayo ina chechembe zinazosababisha maradhi ya kansa."Alisema

Nae Naibu wa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr Seif Rashid amepemdekeza serikali ianzishe kampeni ya kuelimisha watu juu ya madhatra ya kutumia dawa bila ushauri wa wataalam.

"Matumizi ya Diclopa ,Diclofenac au na zingine zote zile lazima yafanywe kwa uangalifu mkubwa ,kwa kuwa hakuna dawa ambayo ni salama kwa asilimia 100"

Dr Rashid amesema taifa bado linakabiliwa na uhaba wa wataalam wa kutoa dawa na wahudumu ili dawa ziweze kusimamiwa na kutolewa kitaalam

Amesema juhudi zinaendelea kuhakikisha vituo vya kutoa dawa vilisajiliwa vinaongezeka nchi nzimaikiwa ni pamoja na kuwanoa vya kutosha wahudumu wa kwenye vituo hivyo.

Ni pale watanzania watakapozifahamu sheria na taratibu zinazosimamia uuzaji na ugawaji wa dawa,ndipo watakapokuwa makini na ununuzi na utumiaji wa dawa husika
Read more...

NYATI WA AJABU AONEKANA NGORONGORO

0 comments
Wakati magwiji wa Sayansi ya Maisha ya Viumbe hai duniani wakidhani wametegua vitendawili vyote kuhusu maisha ya Viumbe hai vya msituni,kimetokea kitendawili kingine katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro,ambako ameonekana aina ya nyati isiyowahi kuonekana  hapa duniani,mwenye rangi isiyozoeleka miongoni mwa nyati waliozoeleka

Kwa kawaida nyati huwa na rangi nyeusi,lakini huyu alieonekana Ngorongoro amepambwa kwa rangi nyeupe -maziwa,akiranda randa katika maeneo ya bonde maarufu duniani la Ngorongoro,na tayari ameshawavuta wanaharakati wa mazingira,wanasayansi wa maisha ya viumbe hai na watafiti wa tabia za wanyamapori ambao wako Ngorongoro kumfuatilia.

"Kwa kweli  aina hii ni adimu sana na ni tukio la ajabu kwa upande wa watu wanaoshughulika na maisha ya viumbe vya misituni,kwa hapa Ngorongoro na nchi nzima kama ninavyojua."Alikiri kiongozi wa watafiti wa maisha ya viumbe hai katika Hifadhi ya Ngorongoro Bw Patrice Mattay
 
Watu wa kwanza kumuona nyati huyo katika hifadhi ya Ngorongoro ni maafisa wa Polisi wa kituo cha hapo Ngorongoro,ambao mwanzo walidai mara kwa mara kuona aina ya wanyama wa ajabu katika eneo lao la kazi,hasa nyakati za alfajiri.

Afisa Polisi JJ Paul ambae alikuwa zamu amethibitisha kukiona kiumbe hicho,"mwanzo nilipata habari zakuonekana kwa mnyama wa ajabu kutoka kwa maafisa polisi wenzangu,na hivi karibuni nilimshuhudia huyu nyati akila majani akiwa amejichanganya na wanyama wengine kwenye ukingo wa bonde"

Inasemekana kuwa eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ina idadi ya nyati wa kawaida wapatao350 kati ya wanyama wapatao laki 3 wanaoishi ndani au kuzunguka bonde hilo kubwa na maarufu duniani.Lakini  huyu nyati mweupe ni aina ambayo haijazoeleka kuonekana katika jamii ya nyati ndani ya hifadhi hiyo.

Meneja anaehusika na hifadhi katika Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro Bw Amiyo T. Amiyo amesema kwamba ugunduzi huu wa nyati mwenye rangi nyeupe unahitaji wito wa kuanzisha aina mpya ya utafiti juu ya tabia za maisha ya wanyamapori.

Kawaida watafiti wengi waliegemea kwa jamii ya wanyama wanaokula nyama (carnivores) kama vile simba, mbwa-mwitu na cheetah,lakini sasa nyati wanaweza kuingia kwenye listi
Read more...

MOS DEF ATOA VIDEO MAALUM YA MWEZI WA RAMADHAN JUU YA WAFUNGWA GUANTANAMO BAY

0 comments

Wakati mwezi mtukufu wa Ramadhan unazidi kusogea,zaidi ya wafungwa 100 wanaoshikiliwa katika gereza la Guantanamo Bay wamekuwa wanaendelea na mgomo wao wa kula.Katika  taarifa za siri iliyovuja kutoka gerezani hapo,zaidi ya wafungwa 40 wamekuwa wakilishwa kwa kutumia mabavu,kwa maagizo ya jeshi la nchi hiyo

Katika video hii ya dakika 4 iliyoandaliwa na taasisi ya haki za binadamu,muongozaji wa filam Asif Kapadia na Yasin Bey ambae anajulikana zaidi kama Mos Def muigizaji na mwanamuziki  kutoka Marekani inaonesha jinsi wafungwa hao wanavyolazimishwa kula kwa kutumia nguvu.

Viongozi wa Jumuia ya Kiislam wameitaka serikali ya Rais Barack Obama kufikiria upya juu ya uamuzi huo wa kuwalisha wafungwa kwa kutumia mabavu,hasa wakati huu wa mfungo wa Ramadhan.

Serikali ya Marekani ilisema kuwa ili kuzuia dharura inayoweza kutokea hapo baadae au matatizo katika wajibu wao, itaheshimu funga ya mchana  kwa kuwalisha kwa nguvu wafungwa 45 wakati wa usiku.Lakini vikundi mbalimbali vya kiislam vimesema kuwa kuendelea kutumia mtindo huo wa kulazimisha kula wakati wa mwezi wa Ramadhan ni sawa na kutia chumvi kwenye kidonda.

"Katika imani yetu ni kosa kumlazimisha mtu kula wakati wowote ule,lakini inaumiza kuona mambo haya yanafanywa hata mwezi wa Ramadhan"Amenukuliwa akisema Ibrahim Hooper msemaji mkuu wa kikundi kinachosimamia haki za Waislam nchini Marekani.The Council On American-Islamic Relations(CAIR).

"(Ni kosa) sio tu kwa mujibu wa imani za kiislam bali pia kitendo hiki kinakiuka misingi ya haki za binadamu kimataifa na hata kanuni za kitabibu"

Dakta Azzam Tamimi kiongozi wa jamii ya Waislam nchini Uingereza amesema "Tunatarajia serikali ya Marekani italifikiria upya suala hili.Mwezi wa Ramadhan unavyoanza suala hili litazidi kuleta fedheha kwa watawala wa Marekani.Ni wakati muafaka Rais Obama afanye maamuzi ya kijasiri kulishughulikia katika njia ambayo itaeleweka na jumuia za kiislam duniani kote.

Wafungwa wanne kati ya 106 waliogoma kupinga kitendo cha serikali ya Marekani kuwaweka kizuizini muda mrefu bila ya kuwafungulia mashtaka, wamefungua kesi katika mahakama za huko Marekani, kupinga kulishwa kwa nguvu.

Kesi iliyofunguliwa katika mahakama ya Washington wiki iliyopita inapinga kulishwa kwa nguvu usiku kwani mgomaji anaweza asinywe maji na kuhatarisha maisha ya alielishwa kwa nguvu.

Katika kuadhimisha mwanzo wa mwezi mtukufu,kikundi cha Haki za Binadamu kimetuma video maalum kwa gazeti la The Guardian la Uingereza.

Ndani ya video hiyo Repa na Muigizaji maarufu wa Marekani Mos Def ambae alisilimu na sasa anaitwa Yasin Bey anaonekana kama mfungwa akiingia kwenye chumba maalum cha Guantanamo Bay kwa ajili ya kwenda kulishwa na madaktari ambao wanatumia mirija ya kulishia wagonjwa mahututi.

MosDef katika video hii anaonesha taabu wanayoipata wafungwa wanaopitia zoezi hili la kulishwa kwa nguvu.

Nyota huyo wa filam za kimarekani,anasema alijitolea kukubali kuingizwa mirija hiyo, kama inavyoonekana, kwa kushirikiana na madaktari wawili ambao nao walijitolea kukamilisha igizo hilo.

Video hiyo inayodumu kwa dakika nne inajaribu kutoa taswira halisi ya kinachotokea ndani ya gereza hilo lililopo kisiwani, katika bahari ya Atlantiki jirani na nchi ya Cuba,kufuatia taarifa za siri ya kufanyika kwa zoezi hilo kuvuja kwa televisheni ya al-Jazeera.

Katika nyaraka za kijeshi zilizovuja kutoka gerezani hapo na kutumwa kwa al-Jazeera ambayo ina kichwa cha habari`Medical management Standard Operating Procedure `inafafanua kuwa ili mfungwa aitwe mgomaji,anatakiwa awe hajala angalau milo tisa na awe amepungua uzito kwa asilimia 85 ya uzito wake wa kawaida.

Iwapo mfungwa analazimika kulishwa kwa nguvu,madaktari wanajeshi walio ndani ya gereza hilo watamfunga minyororo na mdomoni atawekewa kifaa maalum katakachomdhibiti mfungwa huyo asing`ate au kutema mate.Na baada ya hapo,mirija ya chakula huzamishwa tumboni kwa kupitia matundu ya pua.

Zoezi hili huchukua takriban dakika 20 hadi 30,lakini mfungwa analazimika kubaki kwenye kiti huku kafungwa,kwa masaa hadi mawili hadi atakapopigwa X-Ray kifuani ili kufahamu iwapo chakula kimetua tumboni mwa mfungwa.

Baada ya hapo mfungwa huku akiwa na minyororo anapelekwa kwenye chumba kidogo `kikavu`ambako ataendelea kuchungwa na mlinzi kwa saa nzima ili asitapike au kujaribu kujitapisha.Endapo atatapika,anarudishwa tena kwenye kiti kuanza tena zoezi la kumlisha.

Na endapo mfungwa atang`ata mrija wa chakula,madaktari watakibana kicwa chake bila kuachia hadi pale mfungwa atakapo legeza mdomo wake

Makundi ya waumini wa dini zingine pia wamelaani zoezi hilo.Mwezi uliopita mchungaji Richard Pates mwenyekiti wa Kamati ya Sheria za Kimataifa na Amani katika Muungano wa Wachungaji wa Kikatoliki nchini Marekani,alimuandikia barua Waziri wa Ulinzi wa Marekani Chuck Hagel kumkumbushia malalamiko ya  Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu dhidi ya kitendo cha kuwalisha wafungwa kwa kutumia mabavu

Sehemu ya barua hiyo inasema;"Badala ya kutumia mbinu hizo,kwanza taifa letu lifanye kila liwezalo kushughulikia adha inayopelekea mgomo huo kufanyika" 

Read more...

WATANO WAANGAMIA MGODINI MERERANI

0 comments
Watu watano wamefariki dunia katika vilima vya mgodi wa Mererarni, na mtu wa sita alikimbizwa hospitali ya KCMC Moshi akiwa mahututi,baada ya kuangukiwa na kifusi cha shimo walilokuwa wakifanya kazi.
Tukio hilo lilitokea alfajiri ya jana Jumapili,katika Wilaya ya Simanjiro ,Mkoa wa Manyara,ambapo inadaiwa kuwa watu hao sita walikuwa wakifanya kazi katika shimo la mgodi wa Tanzanite,linalomilikiwa na Bwana Onesmo Mbise  mkazi wa mjini Arusha.
Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara Bw.Akili Mpwapwa,alithibitisha kutokea kwa tukio hilo,na kusema kuwa ni kawaida wafanyakazi katika mgodi huo kuendesha shughuli zao nyakati za usiku,na kuongeza kuwa polisi  wanaendelea kulifuatilia tukio hilo.
Kamanda Mpwapwa,alithibitisha vifo vya watu hao ambao aliwataja kwa majina kuwa ni Jackson Kavishe,Noel Kilwa-Kitui,Emmanuel John,Godlove Zebhlon na Emmanuel Joshua,ambao walikwenye eneo la tukio baada ya kuangukiwa na kifusi cha shimo walilokuwa wakifanya kazi.
Mfanyakazi wa sita ametajwa kuwa ni Siphael Simba,ambae alikutwa hai na waokoaji waliofika kwenye shimo hilo lililosajiliwa kwa jina la kampuni ya madini ya Fanon.
Simba alikimbizwa katika Hospitali ya KCMC mjini Moshi ambako alikuwa akiendelea kupigania maisha yake.
Wachimbaji kwenye mgodi huo wamekiri kuwa wanapenda kufanya shughuli zao usiku kwa kuwa hali ya hewa huwa tulivu isiyo na joto kali,tofauti na mchana,ambayo joto huwa kali hasa katika eneo linalokabiliwa na ukame wa mvua.
Matukio ya kuporomoka kwa mashimo ya mgodi ni ya kawaida huko Mererani,ambapo matukio mawili ya kutisha yalitokea mwaka 1998 na 2008 na watu 100 kuangamia katika kila tukio.
Hata hivyo matukio hayo yalisababishwa na maporomoko ya maji yaliyotoka na mvua kubwa za masika katika miezi ya Machi na Aprili
 .
Read more...

Sunday, July 7, 2013

BEYONCE APATA MAMA WA KAMBO

0 comments
Wanamuziki Beyonce na Solange ambao ni mtu na dada wamepata mama wa kambo baada ya baba yao kufunga ndoa na mwanamke mwingine,kufuatia kuachana na mama yao mzazi akina Beyonce
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AP, Mathew Knowles,baba wa akina Beyonce,ambae pia alikuwa meneja wa Beyonce alifunga ndoa na rafiki yake wa kike,mwanamitindo Gena Charmaine Avery huko Houston Texas,mwishoni mwa wiki iliyopita.Mathew Knowles mwenye umri wa miaka 61 na Gena Avery mwenye umri wa miaka 48,walikuwa wameshachumbiana mwaka mmoja na nusu uliopita.Beyonce na Solange hawakuhudhuria harusi.
Mathew Knowles alitalakiana rasmi na mama mzazi wa akina Beyonce,Tina Knowles,mwaka 2011 baada ya mama huyo kufungua kesi ya kudai talaka mwaka 2009.Ndoa yao ilidumu kwa miaka 29.
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797