Pages

 

Tuesday, May 15, 2012

MAISHA YA LULU GEREZANI

0 comments
MAISHA ya msanii maarufu ya filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye yupo katika Gereza la Segerea, yamebainika
Lulu ambaye anadaiwa kuhusika na kifo cha aliyekuwa msanii maarufu wa filamu, Steven Kanumba ‘The Great’ kilichotokea Aprili 7, mwaka huu, imeelezwa kuwa maisha yake ya mahabusu yanasikitisha.
 Msanii huyo licha ya kuwa analetewa chakula kutoka nyumbani kila siku, huwa anakula baada ya kubembelezwa na baadhi ya mahabusu wenzake.
“Lulu siyo yule mnayemfahamu uraiani, humu gerezani amekuwa mtu wa kusikia kile anachoambiwa na wenzake, amekuwa msikivu sana na hupenda kulala mara kwa mara,” Mtu alie karibu na Lulu mahabusu alisema
Habari zinasema msanii huyo amekuwa akifundishwa aya kwa aya za Biblia na amekuwa mwepesi kushika baadhi ya mistari ya kwenye kitabu hicho kitakatifu kwa Wakristo.
“Bila shaka amekuwa akishika aya kwa kuwa alizoea kushika maneno yaliyokuwa yanaandikwa katika script za michezo ya filamu,” alisema askari mmoja wa magereza .
Alisema kinachosikitisha ni pale anapotembelewa na rafiki zake, kwani wakiondoka Lulu hushinda akilia mchana kutwa.
Aliongeza kuwa hali anayoishi nayo msanii huyo gerezani ni ya kutia huzuni na simanzi na haonekani kuzoea mazingira kama walivyo mahabusu wengine.
Hivi karibuni, ilielezwa kuwa Lulu amekuwa akivaa rosari na kusoma Biblia mara kwa mara kutokana na mafunzo anayopewa na baadhi ya walokole waliofungwa katika gereza hilo.
Read more...

EXCLUSIVE: A PNU cabinet Minister infected me with HIV/AIDS

0 comments
Disclaimer:
  Please sit down before reading this real life story ordeal narrated to the Kenya DAILY POST.
 
Elizabeth Wanjiru ‘Shiro’ is a young lady whose life history has unfolded in a way she never envisioned. 2007 was a big year for her. She was a young, beautiful, healthy, perfectly endowed and charismatic student at the University of Nairobi. Her zeal and ambition in life was overflowing.
Elizabeth was quite vocal and active in campus politics. An avenue that her fellow female mates refrained from. She pushed for agendas and actively participated in motions in the university’s political sphere. This made the then Secretary General of SONU, G.G Kariuki notice her.
 Kariuki approached her with a proposal. He wanted to have her in a project dubbed as ‘Vijana na Kibaki’ - an initiative aiming at conglomerating the youth in support of Kibaki’s second presidential bid. The young individuals were meant to advocate for the president to have a second term in office and in reward were flooded with hefty allowances. Shiro like many other University students survived on a shoe string budget. Making some cash outside the pocket money she received from home sounded like the ideal plot.
She was the only female in the 8 member group. Her presence in the group was meant to alter the composition of the group to seem like it was gender sensitive. The group kicked off with a lot of vigour. Days flew. Contacts were made. Her presence was felt….
*……*…..*……*…..*
One day, a youth meeting was held at the PNU headquarters bringing together diverse campus representatives. The meeting was only meant for those in PNU’s pay roll. In attendance were individuals such as Sylvester Kweyu , the then Kenyatta University Students Union (KUSA) chairman. Additionally, Mike who was a Secretary General of one of the Universities was also in the congregation.
The meeting went on well until KU’s Mwenda Gitobu noticed that Mike was in the congregation. He shot up halting the meeting, firing accusations that the meeting had been sabotaged by ODM snitches.
Note:  At the time, bad blood was precipitating between ODM and PNU. The situation was nasty with some individuals swearing to die to keep their partisan loyalty alive.
 A scuffle mushroomed between the two groups causing chaos in the area. The meeting was being held at a house next to the DOD (Department of Defence ) along Lenana Road, where the PNU HQ’s were located. Other executive officials of the party were in attendance and were situated in an office just opposite the press area where the youth were. A trail down the headquarters led to some rented external public toilets.
Having heard the noise made from the scuffle, a powerful PNU Cabinet Minister came to calm the situation down. Since time immemorial, the Minister has always held top respected positions in Government. His influential nature calmed the situation down.
Shiro in a bid to ease the chaos tension, walked down to the loos to relieve herself. Coincidentally, Mheshimiwa also headed to the ‘Public loos’ to take a breather. There, he met the beautiful Shiro and introduced himself. The two gave each other their compliments and exchanged numbers. A friendship bond was formed. Little did she know that this friendship would grow to something more.
*…..*……*……*…..
Shiro forged a head viewing that the meeting with the Minister was just but a contact she had created. The  following week she attended a PNU meeting at Manor house situated in Manor Lane in Karen.(Manor is a posh exclusive avenue where a fairy tale wedding was once conducted by Kiss 100 as a reward to its avid listeners. ) The group of 8 campus representatives spent the night there. However, on the day that the group was meant to leave, the PNU Cabinet Minister called up Elizabeth. He told her that he had sent his driver to pick her up as he longed to see her again.
True to his word, he sent an exquisite limousine that drove her to the Serena Hotel where the two had late lunch and spent some time getting familiar with each another.  They continued their rendezvous and sooner than later they became more than friends.
Years passed. Kibaki retained his position as the president of the Republic. The Post Election Violence almost consumed the country. By the time the situation had calmed down, Elizabeth was through with campus. Hungry for a job, she consulted the Mheshimiwa who through his influence got her a job at Kenya Re-Insurance. Shiro was not the type to date young men who she deemed to be immature. She now had herself a rich sponsor (Mheshimiwa) who bought her a lavish car and a beautiful apartment in Nairobi’s South B area. How to spend money was what the big question for her now. Her love life with Mheshimiwa flourished….
However, in 2010 she began falling ill. A cold wouldn’t leave her side. One day as she was driving from her parent’s house in Thika suburbs, she decided to check in St. Francis Hospital in Mwiki. The doctors carried tests on her and after taking her blood samples found out that she was HIV positive. She was shocked beyond belief. She had been faithful to Mheshimiwa, had he returned the favour? No. Intriguingly, he was quite aware of his health status and had kept it a secret. He had ruined her years of hard work and spiked her future.
Late last year she called Classic 105 Breakfast show and narrated her ordeal to Maina Kageni and King’ang’i in the morning. As she spoke one would tell that she was engraved in so much pain. Her conclusion in the show was simple, if she went back in time, she would never hook up with the Minister. In her words she says, “He gave me everything that mattered then, but took away everything that I need now…”
 
 
 
“We live and we learn….To take one step at a time. There’s no need to rush. It’s like learning to fly, or falling in love. It’s gonna happen when it’s supposed to happen. And we find the reasons why. One step at a time….” 
 
These are lyrics of a song by RnB artist Jordin Sparks that Shiro wishes she listened to years back.
Elizabeth Wanjiru has vowed to go public in 2013 (After elections) and tell her story even name the Minister. She aims at campaigning against the animosity that influential politicians subject innocent girls to.
We at the DAILY POST thank her for giving us the exclusive interview at 680 Hotel in town. We will continue supporting her emotionally.
All the best Shiro
courtesy of the : The Kenyan DAILY POST
Read more...

Wednesday, May 9, 2012

HAKUNA KUWAHURUMIA,MAWAZIRI LAZIMA WASHTAKIWE;CCM YATAMKA

0 comments



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema hakitakuwa na huruma kwa mawaziri ambao wamewajibishwa kutokana na wizara zao kutajwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwamba zimehusika na ufisadi, badala yake kitakuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanafikishwa mahakamani

Kauli hiyo imekuja kipindi ambacho tayari Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inafanya uchunguzi dhidi ya mawaziri sita ambao wametajwa kwenye ripoti hiyo ya CAG na ambao Rais Jakaya Kikwete aliwang’oa katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri.
William Mganga Ngeleja

Lucy Sawere Nkya
“Kama uchunguzi wa Takukuru utathibitisha tuhuma hizo, watapanda kizimbani kwa kuwa hakuna aliye juu ya sheria,” Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema jana.

Akitolea mfano wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa kupanda kizimbani juzi kutoa ushahidi kwenye kesi inayomhusu aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, Nape alisema: “Hii inathibitisha kuwa hakuna aliye juu ya sheria za nchi.”

Nape alikuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa chama hicho, mjini Dodoma ambako pamoja na mambo mengine, alitangaza ratiba ya Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec).

“Katika hilo nasema kuwa hakuna aliye juu ya sheria, jana (juzi) Mzee Mkapa alipanda mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi, iweje hao wengine waachwe? Nasema kama walihusika na ikathibitika kweli hata kama wengine wamebaki katika baraza, ni lazima watawajibika,’’ alisema.

Mawaziri walioachwa katika baraza hilo jipya ni Mustafa Mkulo (Fedha), Mhandisi Omary Nundu (Uchukuzi), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara), Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii) na William Ngeleja (Nishati na Madini).

Lazaro Samuel Nyalandu
Wengine waliokuwa wakitajwa kuguswa katika ripoti ya CAG ni George Mkuchika aliyekuwa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tamisemi na Profesa Jumanne Maghembe aliyuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika. Mawaziri hao sasa wamehamishwa katika wizara hizo. Mkuchika sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Profesa Maghembe ni Waziri wa Maji.

Nape alikiri kupata taarifa za mawaziri hao wa zamani kuchunguzwa na Takukuru, lakini akasema katika mtego huo si wote ambao wanaweza kunaswa.
Dr. Cyril August Chami
Kuhusu wabunge wa CCM waliotia saini barua kutaka kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu ikiwa ni shinikizo la kutaka mawaziri hao wajiuzulu au wawajibishwe, Nape alisema chama chake hakifikirii na hakitathubutu kuwajadili.

Akizungumzia ratiba ya kikao hicho, alisema Kamati ya Maadili ya CCm itakutana Jumamosi ijayo chini ya Uenyekiti wa Rais Kikwete na baadaye siku hiyohiyo, Kamati Kuu itakutana.

Mustafa Haidi Makunganya Mkulo
Alisema Mei 13, itakuwa ni siku ya semina kwa wajumbe wa Nec ambayo pamoja na mambo mengine, watapata nafasi ya kuipitia Katiba mpya ya CCM pamoja na marekebisho.

Jumatatu ya Mei 14, kutakuwa na kikao cha Nec ambacho  kitajadili mustakabali wa siasa nchini pamoja na mabadiliko ya Katiba ya nchi.

Mawaziri waanza kazi
Mawaziri wapya jana walianza kazi baada ya kukabidhiwa na watangulizi wao ambao ama waliondolewa kwenye nafasi zao, au walihamishiwa wizara nyingine.

Mawaziri wapya waliokabidhiwa ofisi jana ni William Mgimwa (Fedha), Profesa Sospeter Muhongo (Nishati na Madini), Dk Abdallah Kigoda (Viwanda na Biashara), Dk Fenella Mukangara (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo) na Christopher Chiza (Kilimo, Chakula na Ushirika).

Omari Rashid Nundu
Katika makabidhiano hayo, Dk Mukangara aliwataka watendaji wa wizara hiyo kuhakikisha kuwa wanasimamia uwajibikaji na nidhamu ili kutimiza mpango wa miaka mitano.

Akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo, Dk Mukangara alisema kila mfanyakazi ana wajibu wa kuhakikisha kuwa anatimiza majukumu yake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kujua anachokifanya akiwa kazini.

“Suala la uwajibikaji ni muhimu kwa sababu kila mmoja anajua wajibu wake, hivyo basi hapaswi kusukumwa,” alisema Dk Mukangara.

Waziri wa Fedha, Willim Mgimwa pamoja na manaibu wake, Janeth Mbene na Saada Mkuya Salumu waliahidi kusimama imara kuhakikisha kodi za Serikali zinakusanywa kikamilifu.
Kwa upande wake, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda hakutaka kuzungumza lolote kwani alisema alikuwa na majukumu mengi ya kufanya katika ofisi yake hiyo mpya.

Wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria waliwapokea mawaziri wao kwa mbwembwe. Waziri wake, Mathias Chikawe alirejea tena wizarani hapo akitokea Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na jana aliingia akiwa na naibu wake, Angela Kairuki.

Wizara ya Maliasili na Utalii, imeandaa sherehe ya kumuaga aliyekuwa Waziri wake, Ezekiel Maige na kumkaribisha Balozi Khamis Kagasheki.

Msemaji wa wizara hiyo, George Matiko alisema  wataandaa sherehe hiyo kuonyesha upendo waliokuwa nao kwa waziri aliyepita.

Matiko alisema wasingependa kumuaga Maige kimyakimya hivyo kwa kuandaa sherehe ambayo itaonyesha ni jinsi gani walikuwa karibu naye.

Jana, Maige alifika wizarani hapo na kukabidhi ofisi kwa Balozi Kagasheki.
SOURCE :Mwananchi Communicatios
Read more...

Monday, May 7, 2012

MAHAKAMA YAKATAA KUTAMBUA CHETI CHA KUZALIWA CHA LULU

0 comments

Msanii wa kike wa filamu nchini Elizabeth Michael leo alifikishwa tena katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Dar Es Salaam kwa ajili ya kusomewa kesi mauaji inayomkabili.Elizabeth anahusishwa na kifo cha msanii mwenzake Steven Kanumba,baada ya msanii huyo kafariki ghafla wakiwa pamoja usiku wa  Aprili 7 mwaka huu

 Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Bi.Augustina Mmbado,Elizabeth alisomewa tena mashtaka na hakutakiwa kujibu chochote kuhusiana na kesi hiyo.Hata hivyo mawakili wanne wanao mtetea Elizabeth waliomba udhuru ambapo wakili Keneth Fungamtama kwa niaba ya wenzake,aliiomba mahakama itoe udhuru kwa mshtakiwa kesi ikasikilizwe kwenye mahakama ya watoto,kwani mshtakiwa bado ana umri mdogo ambao hauruhusu kushtakiwa kwenye mahakama za kawaida, huku akikabidhi cheti cha kuzaliwa cha mshitakiwa kikionesha kuwa ana umri wa miaka 17, na pia kesi yake isikilizwe INCAMERA,(faragha)ombi ambalo mahakama  ililikataa kwa kutumia kifungu namba 198 cha sheria,kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.Pia mahakama ilikataa kutambua cheti cha kuzaliwa cha mshitakiwa kwa madai kuwa cheti kiliandikwa jina la Diana, jina ambalo mshitakiwa hakuwahi kulitumia.Elizabeth anatetewa na mawakili Keneth Fungamtama,Fulgence Massawe,Peter Kibatara na Jackline De Melo.

 Kesi imehairishwa tena hadi  Mei 21 itakapotajwa tena na Elizabeth amerudisha rumande  
Read more...

BINT ALBINO WA MIAKA 15 ATEKWA NA KUUAWA KINYAMA NCHINI BURUNDI

0 comments
Kikundi cha watu wenye silaha wamemteka,kumuua binti wa albino mwenye umri wa miaka 15 na kisha kuukata kata mwili wake nchini Burundi ikiwa ni tukio la 18 ndani ya miaka minne kutokea nchini humo

Watu wenye ualbino,hali ya kibaiolojia ambayo huzuia kabisa utengenezwaji wa rangi ya ngozi,wamekuwa wakibaguliwa na baadhi ya jamii katika nchi kadhaa za kiafrika

Kutokana na imani za kishirikina zilizotawala katika jamii hizo kwamba albino wana uwezo wa ziada,hupelekea watu hao kuuawa na kisha viungo vyao kuuzwa kwa waganga wa kienyeji

Katika tukio la majuzi kundi la watu waliobeba mikuki,magobole na mapanga walivamia nyumba moja katika eneo lililo karibu na mji mkuu Bujumbura na kumteka msichana mwenye umri wa miaka 15

Kwa mujibu wa maafisa wa serikali,watu hao walimuua binti huyo na kisha kukata mikono na miguu na kutokomea navyo.

Idadi ya maalbino waliouawa kwa staili hiyo imefikia 18 tangu mwaka 2008 na kasi ya mauaji hayo ilpungua baada ya mwezi Agosti 2009 ambapo watu wanane walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya mauaji ya albino

Lakini Kassim Kazungu ambae ni Rais wa kikundi kinachotetea maalbino cha Albinos Sans Frontieres anasema kuwa serikali ya nchi hiyo imeshindwa kulinda maisha ya maalbino nchini humo kwani kila mtu aliehukumiwa kifungo kwa mauaji ya albino ametoroka gerezani.

Read more...

Saturday, May 5, 2012

SAGNA AVUNJIKA TENA MGUU,ATAIKOSA MICHUANO YA EURO 2012

0 comments
Beki wa kulia wa timu ya taifa ya Ufaransa anaechezea klabu ya Arsenal amevunjika mguu katika  mechi ya sare ya 3-3 dhidi ya Norwich City na atazikosa fainali zaKombe la Mataifa ya Ulaya yanayoanza tarehe 8 mwezi ujao.Sagna mwenye umri wa miaka 29 alivunjika mguu huo huo mwezi Oktoba na kuwa nje kwa miezi mitatu.

"Amevunjika mfupa wa nyuma ya ugoko.kwemye mguu ule ule ..ni lazima atakuwa amepigwa daruga sio hivi hivi tu.Kuna mchezaji amemwangusha na kisha akaukanyaga mguu wake...sijui ni bahati mbaya au vipi"Kocha wa Arsenal amewaambia waandishi wa habari.

 Yalikuwa ni matarajio ya wengi Sagna angejumuishwa katika kikosi kitakachokwenda kwenye fainali za Euro zitakazofanyika  kwenye nchi za Ukraine na Poland.Sagna hajachezea `Les Bleus` tangu mechi waliyotoka sare ya bila ya kufungana dhidi ya Romania mwezi Septemba wakati wa mchujo wa mashindano hayo makubwa  kabisa ya kimataifa barani ulaya.

Lakini kocha Laurent Blanc ana uchaguzi mpana wa mchezaji atakaeziba pengo la Sagna .Anthony Reveillere wa Olympique Lyon uwezo wa kucheza pande zote,kulia au kushoto na Mathieu Debuchy alionyesha kiwango kikubwa kwenye mechi dhidi ya Ujerumani mjini Bremen mwezi February.Blanc anatarajiwa kutaja vikosi viwili vya awali kabla hajachagua watakaounda timu. itakayoenda Euro.

Katika kikosi atakachokitangaza Jumatano hii,kitajumuisha wachezaji wanaocheza nje ya Ufaransa tu na Mei 15 atatangaza kikosi chenye wachezaji wanaocheza kwenye ligi za nyumbani

Blanc tayari alishamkosa beki wake wa kushoto Eric Abidal ambaye alifanyiwa upasuaji wa kubadilisha ini na pia kiungo Abou Duiaby naye ameumia nyama ya kiazi cha mguu

Ufaransa imepangwa kundi D pamoja na Uingereza,wenyeji Ukraine na Sweden
Read more...

MWANASOKA RASHID YEKINI AFARIKI DUNIA

0 comments
Mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria Rashid Yekini amefariki dunia jana jioni kwa ugonjwa ambao taarifa zinasema ni wa ajabu, mjini Iraa, jimbo la Kwara,Nigeria.

Yekini alirejea kutoka nje ya nchi katikati ya wiki hii alikokuwa akipata matibabu,mchezaji mwenzake wa zamani Mutiu Adepoju aliwaambia wanahabari

Ndugu wa marehemu Yekini wamesema kuwa Yekini alikuwa akisumbuliwa na maradhi ambayo hawakuyaelewa.Yekini inasemekana alikuwa akiishi maisha ya kawaida sana tangu alipostaafu kucheza soka mwaka 2005 na kurudi Nigeria akitokea kucheza soka ulaya.

Alipokuwa ulaya alichezea timu za Vitoria Setubal yaUreno,Sporting Gijon ya Hispania na Olympiakos ya Ugiriki.Aliporudi Nigeria aliendelea na soka kwa kucheza katika ligi ya nyumbani ,NPL.Aliogopa umaarufu na hakupenda kujiweka mbele ya kamera na kalamu za waandishi wa habari na mara kadhaa alikataa vyeo mbali  mbali alivyopewa katika soka la Nigeria.

Wakati wa pilika pilika za kombe la dunia 2010 alikataa alipoombwa kuwa balozi wa Nigeria katika michuano hiyo na nafasi yake alikabidhiwa golikipa wa zamani wa Nigeria Ike Shorunmu

Mwezi uliopitan mchezaji mwenzake ambae walichezea timu ya taifa pamoja,kiungo Segun Odegbemi alikanusha taarifa juu ya hali mbaya ya afya mbaya Yekini.Na katika makala yake kwenye gazeti moja la nchi hiyo,Odegbemi aliwahakikishi wasomaji wake kuwa amefanya mazungumzo na Yekini na yuko mbioni kurudi katika ulimwerngu wa soka na mradi wa kuendeleza vipaji vya vijana katika soka

Mwandishi wa habari ambaye alifika ilipo nyumba ya Yekini mjini Ibadan, alielezwa kuwa mama wa Yekini ambae ni mtu mzima sana na mke wa pili wa Yekini walifika Ibadan kumchukua wiki mbili zilizopita, baada ya kupata taarifa kutoka kwa majirani kuwa Yekini alikuwa akifanya mambo ya ajabu

Nyumbani kwake kulikuwa kimya wakati huo na hakukuwa na dalili ya kuishi mtu kwani geti lilikuwa limefungwa na uwanjani zilipo nyumba zake nne kila kitu kilionekana ovyo na majani marefu yameota.Magari yake yalikuwa yameondolewa, na wapangaji wa Yekini waliokuwa wakiishi katika nyumba tatu walishahama kwa kile kilichoelezwa kuwa waliondolewa na Yekini mwenyewe.Watu wa kanisa lililopakana na nyumba ya Yekini walisema kuwa hawajamuona Yekini kwa mwezi mzima.

Yekini ambaye mwezi Oktoba angetimiza miaka 49 ya kuzaliwa  aliisaidia Nigeria katika michuano ya kombe la dunia 1994 Marekani.Goli lake ndio lilipeleka Nigeria kwenye hatua ya robo fainali,ikiwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kufikia mafanikio hayo.Na alitunukiwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Afrika
Yekini anazikwa  kijijini kwao Offa leo Jumamosi kwa taratibu zote za kiislam
Read more...

Friday, May 4, 2012

RAIS KIKWETE ATANGAZA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI

0 comments
Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete




Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Jakaya Mrisho Kikwete amefanya marekebisho baraza la mawaziri na kulitangaza leo jioni huko ikulu.Na hii ni orodha ya baraza zima la mawaziri alilolitangaza 

 OFISI YA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,
Ikulu

OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H.  Suluhu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

OFISI  YA WAZIRI MKUU
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,

Dr. Cyril Chami  (kaachwa)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

WIZARA
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,

Waziri wa Ujenzi
Dr.  John P. Magufuli, Mb.,

William Ngeleja (kaachwa)
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,

Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,
Dr Hadji Mponda (kaachwa)

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,

Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof.  Makame M. Mbarawa, Mb.,

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof.  Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Mustafa Mkulo (kaachwa)

Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe,  Mb.,

Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,

Waziri wa  Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,

Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,

Waziri wa Maliasili na Utalii
Dr Lucy Nkya (kaachwa)
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,

Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,

Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,

Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,


Hii ni orodha ya Manaibu Waziri:

OFISI YA RAIS
Omari Nundu (kaachwa)
HAKUNA NAIBU WAZIRI

OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,

WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,

Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,

Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,

Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,

Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,

Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.
Read more...

NANI KASEMA KAMANDA KOVA LEGELEGE?MCHEKI AKIPITA JUU YA MOTO BILA VIATU MAZOEZINI JANA

0 comments
Hii ilikuwa jana kwenye maeneo ya Bwalo la Polisi Oyster bay. Zoezi lilifanyika baada ya makamanda kupata mafunzo ya kujenga ujasiri na kujiamini katika utendaji wa kila siku.
Read more...
 
Said Nuhu © 2012 SAID NUHU BLOGS. BLOG IMETENGENEZWA NA BongoClan blog designer nipigie 0658184797